This is...
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 5,050
- 5,204
Kikwete piaMkapa ndiyo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kikwete piaMkapa ndiyo
Wanajeshi wakipindua huwa wanabaka wake kwa waume...Acha wang'ang'anize yatokee ya Gabon
Angalau nimeona comment yako maana nilitaka ku-type kuuliziaStergomena Tax amerudishwa kuwa Waziri wa Ulinzi. She is faithful and dedicated elite.
Katika Teuzi na haya mabadiliko yako uliyoyatangaza,Nafasi ziko 16,waislam ni wawili tuh na wakristo wako 14.
Nawahakikishia laiti hili lingekuwa vice versa hii nchi kila kona ungeskia kelele na kusingekalika.
1. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko (MKRISTO)kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Awali alikuwa Waziri wa Madini.
2. Amemteua January Makamba (MUISLAM) kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali alikuwa Waziri wa Nishati.
3. Amemhamisha Balozi Pindi Chana (MKRISTO) kuwa Waziri wa Katiba na Sheria. Awali alikuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo.
4. Amemhamisha Steven Byabato (MKRISTO)kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali, Byabato alikuwa Naibu Waziri wa Nishati.
5. Amemteua Jerry Silaa (MKRISTO)kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Silaa ni Mbunge wa Ukonga, Dar es Salaam.
6. Rais amemteua Anthony Mavunde(MKRISTO) kuwa waziri wa madini, mwanzo alikuwa naibu waziri wa kilimo.
7. Prof Makame Mbarawa (MUISLAM) aliyekuwa waziri wa ujenzi na uchukuzi amekuwa waziri wa uchukuzi.
8. Innocent Bashungwa (MRISTO)amekuwa waziri wa ujenzi, mwanzo alikuwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa.
9. Godfrey Kasekenya (MKRISTO) aliyekuwa Naibu waziri wa Ujenzi na uchukuzi ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Ujenzi
10. Alexander Mnyeti (MKRISTO) ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Kilimo
11. David Mwakiposa (MKRISTO)Kihenzile ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Uchukuzi. Ni mbunge wa Jimbo la Mufindi
12. Judith Kapinga (MKRISTO) ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa nishati, ni mbunge wa viti maalum Ruvuma.
13. Dunstan Kitandula (MKRISTO)ameteuliwa Naibu Waziri wa maliasili na Utalii, ni mbunge wa Mkinga
14. Stergomena Tax (MKRISTO)amehamishwa wizara ya mambo ya Nje kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
15. Angellah Kairuki (MKRISTO)amehamishwa kutoka TAMISEMI na kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii
16. Dkt. Damas Ndumbaro (MKRISTO) amehamishwa kutoka Wizara ya Katiba ba Sheria na kuwa Waziri wa Utamaduni
Hongera sana kwa kuwa na moyo wa ujasiri na uthubutu.
Akili za tik tok hiziKaondoka wizarani 1990 na hakwenda kuwa Rais direct acheni kukariri
Kina Malecela,Asha Rosé na wengine wengi walikuwa maRais?
Hoja ya direct imetoka wapi? Mbona unashupalia vitu vidogo?Lakini hakutoka direct akawa Rais
Mkuu utapata kesi ya uhaini hujui yule ndio mpakwa mafutaHalafu hivi yule Makamba Jr havuti bangi yule jamaa. Maana alivyokaa kaa kama teja me huwa simuelewi hata kidogo.
Niliandika hapa ikaungwaHeshima sana wanajamvi,
Nayatazama mabadiliko madogo baraza la mawaziri kama sehemu ya mkakati wa kumwinua January Makamba kuelekea kileleni (IKULU) baada ya Wizara ya Nishati kumshinda.Kuendelea kumbakiza wizara hiyo hiyo ilikuwa ni kumharibia kisiasa.
Najua watu wengi wamekimbilia kushangaa nafasi ya Naibu Waziri Mkuu Mh Dotto Biteko,lakini nyuma ya pazia WAZEE wa Msoga Camp safari hii hawataki kukosea kama ilivyokuwa kipindi kileeee cha 2015.Mzee Magufuli hakuwa chaguo lao mazingira au kivumbi cha Lowassa kiliwasababishia kufanya maamuzi bila hesabu sahihi.
January Makamba anaandaliwa maandalizi kabambe bila WAZEE wa Kanda pendwa kushtuka.Mchezo unaochezwa ni kuanzisha cheo kisichokuwepo kikatiba cha NAIBU WAZIRI MKUU kwa lengo la kuwazubaisha WAZEE wa Kanda pendwa kwamba kumbe wao ni sehemu ya walamba asali,hawana haja ya kulalamika wametengwa, hawapendwi, si sehemu ya watoto pendwa.
Vurugu za chama kileeeee kule kanda pendwa hakika kuwastua wapanga mikakati umuhimu wa kumwandaa mwanasiasa kutokea huko kwa lengo la kumtumia baadae kutimiza malengo yao hasa ahadi ya kuhakikishiwa nafasi ya Mzee wa Korosho.
January Makamba kapelekwa pale Foreign Affairs kupata uzoefu baada ya kushindwa vibaya sana Nishati.Katuachia mgao wa umeme,kashindwa kupanga na kupangika mfumo mzima wa manunuzi ya mafuta.Kaondoka Nishati hali ikiwa tete.
Mtangulizi wake Kalemani kasambaza umeme wa REA karibu vijiji vyote kaingia January REA hakuna kila kitu shabala bagala.NISHATI ilimshanda Makamba hana ujuzi zaidi ya kubebwa na mfumo wa walamba asali.
Akachambie majani ya mkorosho huko, mpakwa mafuta atakuwa yule, kichwa kama cylinder head ya Rumion na komwe kama goti la ngamia.Mkuu utapata kesi ya uhaini hujui yule ndio mpakwa mafuta
Hicho mnachotaka kiwe hakitakuwa niondolee zero brain hapaHoja ya direct imetoka wapi? Mbona unashupalia vitu vidogo?
Soma tu kwa kuelewa!
Hata Membe alipita hakuwaAkili za tik tok hizi
Watu wanazungumzia kwamba Mkapa, JK walipitia kwenye diplomasia.
Unaleta utoto,umekaza fuvu km vile una hoja!
Membe hakuwa na dogo janja kipara ngoto hatakuwa mark my words na muache ujinga wa kukariri mambo 😏Akili za tik tok hizi
Watu wanazungumzia kwamba Mkapa, JK walipitia kwenye diplomasia.
Unaleta utoto,umekaza fuvu km vile una hoja!
Tena hii mijadala ife Kwa sababu hawezi kuwa kamwe mnampaisha bureHii mijadala ya wasi wasi wenu na hisia zenu ndivyo vitakavyomfikisha Makamba kwenye hicho kiti na wala sio hao wazee.
Ninyi ndio mnamtengenezea njia kwa kumjadili kila mara maana ndani ya mijadala hiyo mbinu na ramani za ushindi vinatandazwa, bahati mbaya ama makusudi ila matokeo ni maamuzi yenu.
You create the truth you want to inhabit.
Uko sahihi kabisa huyo jamaa ameshakataliwa hadi mbinguni tuombe uzima tutarudi hapa kuwaambia si tulisemaMkuu habari,
Issue hapa ipo hivi ngoja nikueleze ukweli.
Sio kwamba January anatafutiwa nafasi ya kiwa rais, hapana bali Samia anatafuta waungaji mkono kwaajili ya uchaguzi mkuu wa 2025 kwasababu tayari mambugi wanae mtu ambae inabidi achukue nafasi hiyo 2025, huyu mtu hatoki katika familia pendwa za waramba asali.
Lakini issue ya January makamba kuhamishwa hamishwa wizara ni kwasababu ya kwenda kutumika,
1.Kutafuta pesa kwa kuingia mikataba nyonyaji (yaani makamba hapa natumika kama master kiraka)
2.Kwenda kutafuta waungaji mkono wa Samia
Kwa sababu hizi nilizozieleza hapo juu January anaweza kujitafutia mwenyewe uungwaji mkono na ndio anachofanya kumzunguka na kuwazunguka mabosi zake. Lakini amini kwamba January hata kuja kuwa rais wa nchi hii hata afanyaje.
Kukurukara zote hizi ni za dying horse.
Yangu ni hayo kwasasa.