Amani Msumari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,830
- 972
Piga picha una familia na kipato chako ni kidogo lakini unataka ujenge nyumba yako. Utaiambia familia tunafunga mkanda, kama mlikuwa mnakula nyama mara nne kwa wiki inaweza kushuka kuwa mara mbili au moja kwa wiki. Utabana matumizi ili lengo litimie.
Kumbuka katika kufanya hivyo sio kweli kuwa wanafamilia wote watakuelewa. Unaweza kuta hata mkeo hakuelewi. Hapa busara na msimamo vyote vinahitajika.
Tukumbuke kuwa msingi wa taifa unaanzia kwenye familia. Rais Magufuli amechukua njia hii. Wapo watanzania wasiomuelewa. Wanataka kila kitu kiende vilevile, mishahara minono, barabara nzuri, huduma za kiafya Bora na orodha inaendelea. Hawa wanasahau kuwa ni lazima kwanza tufunge mkanda ili tufikie huko.
Sifa moja kubwa ya Rais Magufuli ni kuwa muwazi na mkweli. Yeye hajali itakuwaje ila anasimamia falsafa hiyo ya kunyoosha rula, hapindishi. Katika muda huu ambao kama taifa tumegundua tulikosea wapi na kuamua kwa makusudi kujirekebisha, Kuna watu wameibuka kutaka kutukwamisha. Wenyewe ni kupinga kila kitu na sasa wameona haitoshi wanaanza kuhubiri chuki na mafarakano. Hawa tuwakatae.
Rais Magufuli amekuwa na msimamo wa kuhakikisha sheria zinafuatwa na maadili na utamaduni wetu vinalindwa. Haya yakifanyika, maadui na wasaliti wanaibua maneno, oooh! serikali inaogopa. Hebu fikirieni mfano mmoja tuu. Watia nia wengi wa nafasi za ubunge walikuwa watumishi wa umma. Karibu wote walitia nia kupitia CCM. Leo tunaona panga la mshahara. Kama kweli kuna upendeleo hawa si wangeachwa? Kama sio kusimamia sheria na kuwa na msimamo haya yangeachwa uchaguzi upite lakini wapi, sheria ni msumeno.
Rais Magufuli amethubutu na ameweza. Tunamuunga mkono.
#2020 kura yangu kwa John
Amani
Kumbuka katika kufanya hivyo sio kweli kuwa wanafamilia wote watakuelewa. Unaweza kuta hata mkeo hakuelewi. Hapa busara na msimamo vyote vinahitajika.
Tukumbuke kuwa msingi wa taifa unaanzia kwenye familia. Rais Magufuli amechukua njia hii. Wapo watanzania wasiomuelewa. Wanataka kila kitu kiende vilevile, mishahara minono, barabara nzuri, huduma za kiafya Bora na orodha inaendelea. Hawa wanasahau kuwa ni lazima kwanza tufunge mkanda ili tufikie huko.
Sifa moja kubwa ya Rais Magufuli ni kuwa muwazi na mkweli. Yeye hajali itakuwaje ila anasimamia falsafa hiyo ya kunyoosha rula, hapindishi. Katika muda huu ambao kama taifa tumegundua tulikosea wapi na kuamua kwa makusudi kujirekebisha, Kuna watu wameibuka kutaka kutukwamisha. Wenyewe ni kupinga kila kitu na sasa wameona haitoshi wanaanza kuhubiri chuki na mafarakano. Hawa tuwakatae.
Rais Magufuli amekuwa na msimamo wa kuhakikisha sheria zinafuatwa na maadili na utamaduni wetu vinalindwa. Haya yakifanyika, maadui na wasaliti wanaibua maneno, oooh! serikali inaogopa. Hebu fikirieni mfano mmoja tuu. Watia nia wengi wa nafasi za ubunge walikuwa watumishi wa umma. Karibu wote walitia nia kupitia CCM. Leo tunaona panga la mshahara. Kama kweli kuna upendeleo hawa si wangeachwa? Kama sio kusimamia sheria na kuwa na msimamo haya yangeachwa uchaguzi upite lakini wapi, sheria ni msumeno.
Rais Magufuli amethubutu na ameweza. Tunamuunga mkono.
#2020 kura yangu kwa John
Amani