Mabadiliko ya mwonekano JamiiForums - Juni 2022

yani zamani nilizoea kuperuzi jamiiforums hata lisaa,,,, ila kwa huu muonekno hata hamu ya kingia humu ndani imeisha,

tangu mabadilko haya yafanyike watu wengi wanalalamika ila ndugu yetu Maxence Melo hajabadili chochote, yani imekuwa kama ubabe flani hivi kisa hatuna mbadala wa jamiiforums.

hadi hapa nachoona kuna mbinu ya kibabe inatumika kutulazimisha watumiaji tuzoee huu muonekano mbovu hivyo hivyo kwa lazima hata kama hatuupendi maana hatuna mbadala wa jamiiforms.
 
Kinachoikera zaidi ni kuondoa ule mfumo wa links peke yake na badala yake kuongeza maelezo mafupi chini hali inayopelekea watu kuumiza vidole kwenye kuscroll sijui akina Maxence Melo wao wanaona raha gani au pengine wanatumia PC ama hawaitumii kabisa jamii forum bali waliianzisha kwaajili ya mapopoma kama GENTAMYCINE KISIWAGA
 
na hili ndilo tatizo kubwa, pia hii wauwezi kusoma thread nyingi kwa wakati mmoja kwenye display, yaan display nzima inajaa thread mbili tu
 
Ni tangu mabadiliko hayo yalipofayika alhamisi wiki iliyopita usiku wa manane, mabadiliko hayo yanayodaiwa ni maboresho yamekuwa ni kero wa watumiaji wengi.

Kwenye muonekano, malalamiko mengi yamelenga mtindo mpya wa kuweka post zinazotrend badla ya ukurasa wa mbele kuwa sehemu ya kuchagua majukwaa, pia kumekuwa na vitu vya zamani vilivyozoelka ambavyo kwa sasa havipo.

Kwenye utumiaji pia yamekuwepo mabadiliko, watumiaji wengi wakilalamika mtandao umekuwa mgumu kutumika kirahisi, wengi wakidai haupo "User Friendly" utumiaji usio rafiki.
 
Melo anafanya kama vile tuko youtube unakuta zinaanza zinazotrend kwanza
 
Kupitia mmiliki wa jamii forums ndiyo nimegundua uongozi ni kalama yaani unakuta mtu anamsema Maxence Melo unaweza kudhani ni kaka yake au mtoto wa baba yake mkubwa

Maoni yangu

Siku kama mbili ilikuwa ni ngumu kwangu ila kwa sasa naona hata ile ya mwanzoni ni ya kiboya sana
 
Tutazoea tu si kila siku unakula kifo cha mende siku ingine jaribu Chuma mboga uone raha yake.
tutazoea kwa hiari ama kulazimishwa kama hizi tozo mpya za waziri aliesema tukishindwa tuhamie burundi? 🙄
 
Malalamiko FC jifunzeni kukubali mabadiliko bila kulazimishwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…