Mabadiliko ya Sheria: Rais, Makamu wake, Jaji Mkuu, Waziri Mkuu na Spika wa Bunge kutofunguliwa kesi Mahakamani

Mabadiliko ya Sheria: Rais, Makamu wake, Jaji Mkuu, Waziri Mkuu na Spika wa Bunge kutofunguliwa kesi Mahakamani

Msitishike. Siku ya siku UNA SUSPEND KATIBA, UNAUNDA MAHAKAKAMA MAALUMU UNAWASHITAKI NA KUWAFUNGA. Ni ujinga mchana kweupe kujitungia sheria za kuwadhulumu, kuwakandamiza wengine and then zisimame after you! Common sense, reason and justice dictate that katika udhalimu kama huu you act that way to make sure that Justice is done after them!

Lex malla, lex nulla. A bad law is no law
Malalamiko yako yako too general. Unalalamikia kitu gani? Sheria gani? Kama ni mswada wa ma mabadiliko ya Basic rights and duties enforcement Act. Sio kwamba haya mabadiliko yanakataza viongozi kama Rais,makamu wake, waziri mkuu,spika na makamu wake wasishitakiwe.
Ila imewekwa taratibu lazima uwe na kiapo kuonyesha namna gani umeathirika wewe unaefungua kesi. Yaani namna gani haki yako imeathirika.
Pili kama unawashitaki wakiwa wanatekeleza majukumu yao atakayekuwa anashitakiwa ni AG. Jambo ambalo ni la kawaida kabisa.
 
Haya marekebisho vipi siku yskiwageuka wakawa wao ndio wapinzani?
 
Nimetoka kusoma kitabu cha state of blood kilichoandikwa na Henry Kyemba aliyekuwa waziri kwenye serikali ya Idd Amini kuna mambo mengi yanayofanana na kinachoendelea sasa.
Mkuu hebu tutajie basi na tena kwa ulinganisho na utawala huu.
 
Malalamiko yako yako too general. Unalalamikia kitu gani? Sheria gani? Kama ni mswada wa ma mabadiliko ya Basic rights and duties enforcement Act. Sio kwamba haya mabadiliko yanakataza viongozi kama Rais,makamu wake, waziri mkuu,spika na makamu wake wasishitakiwe.
Ila imewekwa taratibu lazima uwe na kiapo kuonyesha namna gani umeathirika wewe unaefungua kesi. Yaani namna gani haki yako imeathirika.
Pili kama unawashitaki wakiwa wanatekeleza majukumu yao atakayekuwa anashitakiwa ni AG. Jambo ambalo ni la kawaida kabisa.
I guess I am more knowledgeable about the law than you think! All dictators are like that, there is no wonder with that! Time will tell!
 
Makamu rais bendera fuata upepo tumeambiwa hana maamuzi/power sasa hiyo kinga ya nini? Kukaa kimya na kumwakilisha boss wake kwenye misiba na dhifa mbalimbali anahitaji kinga?

Waziri Mkuu pia bendera fuata upepo tumeambiwa hana maamuzi/power ndiyo maana kila anakokwenda anasema nimeagizwa na muheshimiwa, mwishoni lazima amalizie na kale kapambio. Je kumwakilisha rais pia anahitaji kinga. Pinda alikwenda mbali zaidi alilia bungeni akasema angekuwa na maamuzi ... sasa kinga ya nini kwa kuagiza kibaya au ukakubali kuagiza kibaya?

Kinga inamaana kwa mtu wenye maamuzi ya mwisho sio waagizwa baada ya maamuzi.

Tanzania inarudi nyuma!!

Mungu ibariki Tz, Mungu ibariki Afrika.
 
Our freedoms are vanishing. If you do not get active to take a stand now against all that is wrong while we still can, then maybe one of your children may elect to do so in the future, when it will be far more riskier — and much, much harder.
I hear you sister!!!
 
Nimetoka kusoma kitabu cha state of blood kilichoandikwa na Henry Kyemba aliyekuwa waziri kwenye serikali ya Idd Amini kuna mambo mengi yanayofanana na kinachoendelea sasa.
Mkuu hauna pdf ya Hiki kitabu unisaidie? Nmejaribu kukicheki net nimekosa
 
Kwahiyo tunaitafuta Nazi Germany au Korea ya Kim au mseto?
Sikutegemea Tanzania ya Mwl.Nyerere kuna siku itakuwa na sheria katiri na kandamizi huko tuendapo.
Hivi huku ndio kumuenzi Baba wa Taifa?
 
MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) kwa kushirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wamepinga muswada wa sheria wa marekebiaho ya sheria mbalimbali nchini namba 3 wa mwaka 2020.

THRDC na LHRC wametoa tamko la kupinga muswada huo leo Alhamisi tarehe 4 Juni 2020 mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa amesema katika mswada huo kuna marekebisho ya Sheria ya utekelezaji wa Haki za Kimsingi na Wajibu ya 1994 (BRADEA).

Olengurumwa amesema, marekebisho ya kifungu Kifungu namba 4 cha BRADEA kinarekebishwa na kusomeka kwamba, maombi ya kufungua kesi Mahakama Kuu hayatakubaliwa endapo hayajaambatanishwa na kiapo cha mlalamikaji kuelezea jinsi alivyoathiriwa na uvunjifu wa haki na wajibu katika ibara ya 12 hadi 29 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977.

“Tumekuwa tukipeleka kesi ya kulalamika ukiukwaji wa haki za binadamu uliopo katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 12 mpaka 29, sasa kwa mujibu wa mabadiliko ambayo yanakuja sasahivi ni lazima uwe na cheti cha kiapo cha kuonyesha kiasi gani wewe mwenyewe umeathirika na ukiukwaji huo,” amesema.

Amesema, Kifungu namba 7(4), ikiwa malalamiko ya uvunjifu wa haki unaelekezwa kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania au, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika wa Bunge, au Jaji Mkuu wa Tanzania, malalamiko hayo yatafungliwa dhidi ya mwanasheria mkuu wa serikali ikiwa na maana hakutakuwa na uwezekano wa kufungua kesi dhidi ya viongozi hao.

View attachment 1468939

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa (wakwanza kulia), Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga (Wapili kulia).

“Sasa hivi, tuna kesi nyingi tumefungua dhidi ya Spika na kuna kipindi Rais alifunguliwa kesi na akina Fatma Karume na Ado Shaibu hizo zote zitaondolewa maana yake Tanzania hatutaweza kumshtaki mtu kama yeye kwa kukiuka Katiba,” amesema.

Aidha, Olengurumwa amesema sheria nyingine ambayo inaelekea kufanyiwa mabadiliko ni sheria ya uongozi wa Mahakama namba nne ya 2011.

Amesema, kifungu namba 64 (a) cha sheria hiyo kimerekebishwa na kuandikwa kuwa mfanyakazi yoyote wa mahakama hatoshtakiwa kwa jambo lolote atakalolifanya au kutolifanya kwa nia njema atakapikuwa anatekeleza majukumu yake.

“Hii inaweka kinga kwa mtu yoyote alioko mahakamani hata kama si Jaji au Hakimu na madhumuni ya marekebisho hayo ni kuipa mahakama nguvu ya kukataa maombi ambayo hayajakidhi matakwa ya ibara wao ndio wanadai hivyo.”

“Madhumuni ya marekebisho haya yanakwenda kuondoa nguvu za mtu mmoja mmoja au taasisi kama zakwetu kufungua kesi kwa sababu ya kulinda haki zozote zinazokiukwa Tanzania na hii ni kinyume na ibara ya 26 ya Katiba ya Tanzania ambayo imemruhusu mtu yoyote kwenda mahakamani kudai haki,” amesema.

Kwa upande wake, Anna Henga, Mkurugenzi Mkuu wa LHRC, amesema mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya utekelezaji wa haki za msingi na wajibu yanapingana na ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Baada ya Tanzania kujitoa kwenye mahakama ya Afrika sasa Azaki hatuwezi kwenda huko sasa hata kwenye mahakama za ndani hatutaweza kwasababu sheria hii inaweza kuzuia haki hiyo,” amesema.

Hata hivyo, Henga amesema marekebisho anayaona kama ni muendelezo wa kutaka kunyima haki kwasababu hata sababu za Tanzania kujitoa katika mahakama ya Afrika hazijajulikana hadi sasa.

“Ni kitu cha ajabu sana kwamba Afrika Mahakama ipo nyumbani kwako kama inakuletea heshima wewe ndo unayeitunza halafu unajitoa kwanini? hata hii, unaweza ukashangaa ni kwanini wazuiwe watu ambao wanataka kutetea haki za watu? Ukitafsiri kikawaida maana yake haki itavunjwa zaidi,” amesema.

THRDC na LHRC wametoa wito kuwa mapendekezo hayo ya mabadiliko ya Sheria ya Utekelezaji wa Haki za Kimsingi na Wajibu yaondolewe kabisa Bungeni kwakuwa maandalizi ya mapendekezo hayo hayakuhusisha
kabisa wadau mbalimbali wakiwemo wadau wa haki za binadamu tangu mwanzo.

Aidha, wamesisitiza kuwa kifungu cha mapendekezo ya sheria kinachotaka kutoa kinga kwa wafanyakazi wote wa Mahakama kutokushtakiwa kirekebishwe na kinga hiyo iendelee kuwepo kwa Majaji na Mahakimu pekee kwa mujibu wa Katiba.

Muswada huo unaopendekeza mabadiliko makubwa ya sheria mbalimbali ambayo THRDC na LHRC wanalaani wakieleza kuwa yanalenga kuondoa haki ya kufungua kesi za kikatiba kwa niaba ya wananchi, uliwasilishwa bungeni na umepangwa kujadiliwa kwenye mkutano wa 19 wa Bunge (Mkutano wa Bajeti) ambao ulianza tarehe 05 Mei na utamalizika
Juni 19 mwaka 2020.


KWANI KINA OLENGURUMWA HAWAJUI KUWA DAWA YA SHERIA NI SHERIA?? ACHA DAWA IWAINGIE
 
Watu wanachukulia masihara sana, hii hali ni ya hatari! Tz bado mimi siichukulii poa! Kama wapo watu wanaojiunga na makundi ya kigaidi mojawapo linalosumbua Msumbiji hii inaonyesha raia wenye uthubutu wapo! Ni suala la muda tu.

Naamini kuna watu wapo kwenye mfumo na ni wazalendo! Kuna wana ulinzi na usalama wa nchi na mipaka bado ni wazalendo. Masihara yao kwenye hii nchi watu watakuja kutafutana humu!
 
Malalamiko yako yako too general. Unalalamikia kitu gani? Sheria gani? Kama ni mswada wa ma mabadiliko ya Basic rights and duties enforcement Act. Sio kwamba haya mabadiliko yanakataza viongozi kama Rais,makamu wake, waziri mkuu,spika na makamu wake wasishitakiwe.
Ila imewekwa taratibu lazima uwe na kiapo kuonyesha namna gani umeathirika wewe unaefungua kesi. Yaani namna gani haki yako imeathirika.
Pili kama unawashitaki wakiwa wanatekeleza majukumu yao atakayekuwa anashitakiwa ni AG. Jambo ambalo ni la kawaida kabisa.

Hivi wewe ni Mwanasheria? Kama jibu ni ndiyo basi ulipoteza muda wako bure na iwapo jibu ni hapana waachie Wataalamu wa sheria waongee!

Unajua maana ya SHERIA NI MSUMENO kuwa inakata kotekote?

Rais Magufuli tangu ameingia kwenr Utawala amekuwa ni mwenye kutengeneza sheria kandamizi huku yeye akijihami ili sheria isimshughulikie! Kifupi huyu ni dikteta perce.

Kwa akili ya kawaida tu, haiwezekani afanye makosa Rais Magufuli, Makamu Suluhu Hassan, PM Msjaliwa, Spika Ndugai na Naibu wake Tulia Ackson, lakini ATI atayeshtakiwa ni Mwanasheria Mkuu! Wapi na wapi?

Huu ni uvurugaji mkubwa Sana wa mfumo wa Sheria na Mahakama zetu za Tanzania.
 
Nimekuwa najiuliza kwanini Serikali inapeleka Muswaada wa kuwakinga Viongozi kwani wanataka kufanya nini ili Wakingwe?
 
MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) kwa kushirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wamepinga muswada wa sheria wa marekebiaho ya sheria mbalimbali nchini namba 3 wa mwaka 2020.

THRDC na LHRC wametoa tamko la kupinga muswada huo leo Alhamisi tarehe 4 Juni 2020 mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa amesema katika mswada huo kuna marekebisho ya Sheria ya utekelezaji wa Haki za Kimsingi na Wajibu ya 1994 (BRADEA).

Olengurumwa amesema, marekebisho ya kifungu Kifungu namba 4 cha BRADEA kinarekebishwa na kusomeka kwamba, maombi ya kufungua kesi Mahakama Kuu hayatakubaliwa endapo hayajaambatanishwa na kiapo cha mlalamikaji kuelezea jinsi alivyoathiriwa na uvunjifu wa haki na wajibu katika ibara ya 12 hadi 29 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977.

“Tumekuwa tukipeleka kesi ya kulalamika ukiukwaji wa haki za binadamu uliopo katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 12 mpaka 29, sasa kwa mujibu wa mabadiliko ambayo yanakuja sasahivi ni lazima uwe na cheti cha kiapo cha kuonyesha kiasi gani wewe mwenyewe umeathirika na ukiukwaji huo,” amesema.

Amesema, Kifungu namba 7(4), ikiwa malalamiko ya uvunjifu wa haki unaelekezwa kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania au, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika wa Bunge, au Jaji Mkuu wa Tanzania, malalamiko hayo yatafungliwa dhidi ya mwanasheria mkuu wa serikali ikiwa na maana hakutakuwa na uwezekano wa kufungua kesi dhidi ya viongozi hao.

View attachment 1468939

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa (wakwanza kulia), Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga (Wapili kulia).

“Sasa hivi, tuna kesi nyingi tumefungua dhidi ya Spika na kuna kipindi Rais alifunguliwa kesi na akina Fatma Karume na Ado Shaibu hizo zote zitaondolewa maana yake Tanzania hatutaweza kumshtaki mtu kama yeye kwa kukiuka Katiba,” amesema.

Aidha, Olengurumwa amesema sheria nyingine ambayo inaelekea kufanyiwa mabadiliko ni sheria ya uongozi wa Mahakama namba nne ya 2011.

Amesema, kifungu namba 64 (a) cha sheria hiyo kimerekebishwa na kuandikwa kuwa mfanyakazi yoyote wa mahakama hatoshtakiwa kwa jambo lolote atakalolifanya au kutolifanya kwa nia njema atakapikuwa anatekeleza majukumu yake.

“Hii inaweka kinga kwa mtu yoyote alioko mahakamani hata kama si Jaji au Hakimu na madhumuni ya marekebisho hayo ni kuipa mahakama nguvu ya kukataa maombi ambayo hayajakidhi matakwa ya ibara wao ndio wanadai hivyo.”

“Madhumuni ya marekebisho haya yanakwenda kuondoa nguvu za mtu mmoja mmoja au taasisi kama zakwetu kufungua kesi kwa sababu ya kulinda haki zozote zinazokiukwa Tanzania na hii ni kinyume na ibara ya 26 ya Katiba ya Tanzania ambayo imemruhusu mtu yoyote kwenda mahakamani kudai haki,” amesema.

Kwa upande wake, Anna Henga, Mkurugenzi Mkuu wa LHRC, amesema mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya utekelezaji wa haki za msingi na wajibu yanapingana na ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Baada ya Tanzania kujitoa kwenye mahakama ya Afrika sasa Azaki hatuwezi kwenda huko sasa hata kwenye mahakama za ndani hatutaweza kwasababu sheria hii inaweza kuzuia haki hiyo,” amesema.

Hata hivyo, Henga amesema marekebisho anayaona kama ni muendelezo wa kutaka kunyima haki kwasababu hata sababu za Tanzania kujitoa katika mahakama ya Afrika hazijajulikana hadi sasa.

“Ni kitu cha ajabu sana kwamba Afrika Mahakama ipo nyumbani kwako kama inakuletea heshima wewe ndo unayeitunza halafu unajitoa kwanini? hata hii, unaweza ukashangaa ni kwanini wazuiwe watu ambao wanataka kutetea haki za watu? Ukitafsiri kikawaida maana yake haki itavunjwa zaidi,” amesema.

THRDC na LHRC wametoa wito kuwa mapendekezo hayo ya mabadiliko ya Sheria ya Utekelezaji wa Haki za Kimsingi na Wajibu yaondolewe kabisa Bungeni kwakuwa maandalizi ya mapendekezo hayo hayakuhusisha
kabisa wadau mbalimbali wakiwemo wadau wa haki za binadamu tangu mwanzo.

Aidha, wamesisitiza kuwa kifungu cha mapendekezo ya sheria kinachotaka kutoa kinga kwa wafanyakazi wote wa Mahakama kutokushtakiwa kirekebishwe na kinga hiyo iendelee kuwepo kwa Majaji na Mahakimu pekee kwa mujibu wa Katiba.

Muswada huo unaopendekeza mabadiliko makubwa ya sheria mbalimbali ambayo THRDC na LHRC wanalaani wakieleza kuwa yanalenga kuondoa haki ya kufungua kesi za kikatiba kwa niaba ya wananchi, uliwasilishwa bungeni na umepangwa kujadiliwa kwenye mkutano wa 19 wa Bunge (Mkutano wa Bajeti) ambao ulianza tarehe 05 Mei na utamalizika
Juni 19 mwaka 2020.


Kichwa cha habari kinapotosha kabisa. Mabadiliko haya ya sheria hayazuii Rais,makamu wa rais,spika na waziri mkuu kufunguliwa mashitaka. Ila ukitaka kufungua mashitaka lazima uwe
, , Spika Ndugai na Naibu wake Tulia Ackson lakini Aslakini ashtakiwe Meanasheia Mkuu!

Hivi wewe ni Mwanasheria? Kama jibu ni ndiyo basi ulipoteza muda wako bure na iwapo jibu ni hapana waachie Wataalamu wa sheria waongee!

Unajua maana ya SHERIA NI MSUMENO kuwa inakata kotekote?
Rais Magufuli tangu ameingia kwenr Utawala amekuwa ni mwenye kutengeneza sheria kandamizi huku yeye akijihami ili sheria isimshughulikie! Kifupi huyu ni dikteta perce.
Kwa akili ya kawaida tu....haiwezekani afanye makosa Rais Magufuli, Makamu Suluhu Hassan, PM Majaliw
Mh Chadema imejaa vilaza. Spika anashitakiwa akiwa anafanya kazi za bunge unataka nani akasimame mahakanani? Hujui hata nini maana ya government liability
 
Back
Top Bottom