Mabeberu, Vibaraka wa Mabeberu, Wazalendo wa Hayati Magufuli, na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo

Ngoja nikupuuze kimada wa Deusdedit Kakoko coz' hauelekei kuwa na uwezo wa ku-argue!
Ujinga wa kuwapa nchi nyingine sehemu nyeti kama bandari eti waijenge na kuindesha haiwezi kukubalika. Kama ni viwanda wajenge lakini kwa nini wang'ang'anie bandari? Magufuli alipokataa huu ulaghai mlisema tumepoteza fursa kubwa sana na inakwenda kwingine 🤣 🤣 🤣 🤣. Nashangaa mpaka sasa hawajaanza huko kwingine ila bado wanawatumia nyie vibaraka kuanzisha thread za kuuza nchi hapa. Mradi wao si ni mzuri? Ina maana muda wote hawakupata sehemu ya kuupeleka?
 
Wanaamini mwendazake hakukosea wala kupotoshwa!!!
 
Issues sio Biashara mpya n.k issue ni uwepo wa mizigo utakayoweza kuihudumia
 
Wanaamini mwendazake hakukosea wala kupotoshwa!!!

..mwendazake alikuwa MUONGO wa kupindukia.

..alikuwa akidanganya hata mahali pasipohitaji kudanganya.

..kwa mfano, aliwahi kwenda bandarini halafu akadai amekuta vichwa vya treni vimetelekezwa na mwenye mali hajulikani.
 
Mkuu watu wenye roho ya kimaskini wana tabia zinayofanana "KUPENDA UMASKINI, KUCHUKIA WENYE MAFANIKIO, UVIVU WA KUSOMA - KUFIKIRI NA KUJADILI... Hupenda kukurupuka na kuhemkwa hata kwa wasiyoyaelewa!!"
 
Mkuu mbona unajikanganya? Kakonko au kakoko ni sahihi sana au alimpotosha mwendazake? Je kwanini anatuhumiwa ufisadi? Je miradi mingapi imebainika kuwa chini ya kiwango na kwanini CAG atishwe? Mwendazake alifanya alichoona kinafaa kwa upande wake kama watangulizi wake walivyofanya na huyu aliyepo aachwe atekeleze anachoona kinafaa kwa mustakabali wa Taifa. Ikiwa mlimpenda sana kwanini hamkuzikwa nae au ninyi ni wale "mla nawe...?"
 
Mkuu,ikiwa uyasemayo haya ni true...basi umenifungua macho sana

Shukran Bro
Shukran sana
Unafaa pongezi
 
Sijasoma hadi mwisho ila hata tukitaka kusingizia wengine, je China katika nchi ilizoenda kuwekeza ni kipi kizuri ambacho tunajifunza zaidi ya mbinu zao za kutawala dunia kama ilivyokuwa Europe enzi zile za karne ya 18? Tofauti ni science tu lakini nia na matunda tunayoyaona kwetu ni yale yale....Sasa utawatetea kwa lipi? Tupe mfano wa nchi iliyopata faida hadi sasa kwenye bara letu ili na sisi tuhamasike...Kwani sisi ndiyo akina nani atupe mteremko kinyume na wengine?

Mifano ya hizo bandari ulizotoa ni chambo tu kwa africa, maana China inajua fika haiwezi kuinyonya Europe kirahsi ila inaitumia kuwapa matamanio akina sisi ambao katika equation ya dunia kila mtu katuweka chini ya miguu yake...Ifike sehemu na sisi tufurukute basi....China ianze kuonyesha mifano chanya kwanza ndipo tutakubaliana nao; so far kwa mikataba ile ambayo tumeambiwa mambo wanaotakakufanya ni faida kutofanya mradi huo kwakua ardhi yetu na bahari yetu itatumika hata kwa hicho kidogo kuliko hasara watakayotusababishia ki hali na ki mali watakapotekeleza mradi huo kulingana na mkataba ule tuliohadithiwa na hayati JPM...Wale wenzetu kitumbua chenu kimetiwa mchanga na mwenda zake kwa hakika haiwezekani ni bora kufikiria njia nyingine!
 
Kwanza tupongeze mtoa mada kwa kuleta mada nzuri yenye hoja nzito zinazopaswa kujadiliwa kwa hoja.
Bila kujali hoja ya mtoa mada, tunakubaliana au siyo, niseme tu hizi ndo mada zinapaswa kuletwa kwenye jukwaa hili tuzijadili.
Tumpinge kwa hoja au tumuunge kwa hoja zenye maslahi kwa taifa letu, pia tukubali kwamba tunatofoutiana uono na upeo na uelewa was Jambo fulani fulani , Yale ambayo tunayajua kwa undani na kwa uelewa mpana tunayaeleze kwa faida ya wote Bila kupotosha, lakini Yale ambayo hutuyajui kwà upana tuongeze nguvu kuyajua na kusikiliza wengine , hapo tunaweza kusaidia kuboresha hili jukwaa kujadiliwa hoja, na kuruhusu watu wengine hata viongozi wakubwa was serikali kutoa hoja zao lakini pia kuchukua hoja humu za kusaidia taifa, asanteni tuendelea na mada mezani
 
Mkuu mimi sipendi siasa ila hili linanishawishi kusema kitu.
Kuna uwezekano mkubwa bandari za piraeus na hambantota zimehujumiwa na mchina ili yeye azikamate kwa maslahi yake.
Kuna uwezekano mkubwa china akijitoa piraeus na hambantota zikarudi kudorora kiufanisi maaana zinaendeshwa kwa influence ya mchina na si umuhimu wao kijiografia.

Endapo miaka ya umiliki wao ikiisha kuna uhakika gani kuwa hawatatengeneza mazingira shindanishi ili bandari ishindwe na wao warudi kuimiliki kama hambantota au kutafuta malisho bora zaidi kwa ajili yao?

Ni matumaini yangu serikali inatafuta namna bora zaidi ya kuvuna wakati hawa jamaa wakiwa ndio wamiliki wakuu kwa mategemeo kuwa yajayo hayatabiriki ndio maana inakomaa na kodi kuliko kutegemea kuachiwa mradi usiojua mwisho wake.
Tujipemuda tu.
 
Kwahakika kama yangekuwa ni maslahi ya taifa kila mtu angepigana kuona yanapatikana, tatizo ni wale wanaousemea mradi hawana moral authority ya kufanya hivyo kutokana na track records zao za nyuma ndiyo sababu ya wengi wetu kuhofu...Kwanini basi kama ni maslahi ya taifa wasiweke wazi kila kitu ili taifa lijue kunani?

Huo ujanjaujanja wa watu hao na background zao ndizo zinazotufanya tuogope...Wengi wao walihusika ku sign mikataba mibovu na dhalili leo hii wanakipi jipya la kutueleza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…