Quote:Kama unaona jkt itamdhalilisha mwanao mpeleke akapate mafunzo ya ukakamavu taliban kwenye misingi ya kidini akimaliza arudi kuendelea na chuo au kaa nae nyumbani kwako muda wa chuo ukifika mpeleke shule
Hivi mko dunia gn ninyi vijanaHuyu jamaa bana kanishangaza mno, kingine namwambia ulimwengu wa kijani yeye anawaza vyama sijui kuna mafunzo ya awali ya jeshi hufanyikia mjini kashindwa kujiongeza naamanisha pori hiyo.
Kwa muislam kuvaa mavazi ya stara ni kuabudu.Kinyume na Katiba sawa. Ebu tupe ni kifungu gani cha Katibai ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinazungumzia uvaaji wa bukta JKT? Au umejichanganya ulikuwa unamzungumzia Katiba ya BAKWATA? Ahahahahaha!!!
Jeshi la nchi ni kama Familia moja. Kila Familia ina utaratibu wake. Usitake utaratibu wa Familia yangu ufanane na Utaratibu wa Familia yako. Dini ni masuala ya kiroho au Imani na ni ya kudumu hadi ufe.. Jeshi ni masuala ya kimwili i.e. Ukakamavu na Uzalendo. Mafunzo ya Kijeshi ni ya muda mfupi sana na yataisha na kukuacha ubaki na dini yako. Jeshi haliendekezi sana mambo ya Udini.Waukize wamarekani, malawi, south Africa, uk wanafanyaje.
Unaweza kugoogle mwongozo, type maneno haya.
GUIDE ON RELIGION AND BELIEF
IN THE
ARMED FORCES
Kuna tofauti ya maana ya dhana ktk serikali.Taratibu na kanuni za jeshi hazina dini, rangi wala kabila. Nidhamu ya jeshi ni tofauti kabisa na uraiani. Vivyo hivyo fikra. Waliopita jeshini wanalijua hilo.
Wacha vijana watembee kwa mwendo wa kunyakua wapate ukakamavu kimwili na kifikra.
Kuna waislam na waislam jina jitafakar uko kundi ganiWafanye mafunza na mahijabu na manikab sio????
Mnafanya waislamu wote tuonekane hamnazo...
Any way kutopiga kelele si mwongozo ktk katiba iliyojipambanua haina dini.Kwa taarifa yako, ni kwamba kuna sheria na taratibu nyingi za serikali ambazo ni kinyume cha mafunzo ya ukatoliki lakini wakatoliki hawapigi kelele kwa vile wanatambua mafunzo yanayosema kuwa "Ya Kaizari mpe Kaizari na ya Mungu mpe Mungu." Wanajua kutengansiha imani zao binafsi na mambo ya serikali.
Jeshi na taasisi zote zinatuongoza kwa kufata sheria mama. Katiba.Taratibu na kanuni za jeshi hazina dini, rangi wala kabila. Nidhamu ya jeshi ni tofauti kabisa na uraiani. Vivyo hivyo fikra. Waliopita jeshini wanalijua hilo.
Wacha vijana watembee kwa mwendo wa kunyakua wapate ukakamavu kimwili na kifikra.
Ndo mana Jeshini hakuna Kanisa wala Msikiti au Kilinge. Kule utakutana na smart area, Qt- guard(armoury), Mahanga, Dispensary, viwanja vya gwaride, Wimbo mkali, Mapipa ya jikoni n.k. n.k.Kwa muislam kuvaa mavazi ya stara ni kuabudu.
Na katiba yetu imetumka kuwa kila raia hatozuiliwa kuabudu.
Kwanini jkt wabunge kanuni zinazopingana na katiba ktk nchi ambayo nusu ni waislam
Kwanini nchi zenye waislam wachache wanazinfatia na kuwalinda watu wa dini.
Mkuu; Bado hujaelewa, kutambua na kukubali kwamba hapa tulipo ni Tanzania na sio huko ulikotaja? Hata hivyo hujazuiwa kwenda kuishi huko.Jeshi na taasisi zote zinatuongoza kwa kufata sheria mama. Katiba.
Mbona nchi nyingi za kidemokrasia zina uelewa huo. Watz tumerogwa na nani. Kwanini hatuna uvumilivu na kuheshimiana value za kila kundi.
Minnesota’s first hijab wearing police woman: how cool is she? - MVSLIM
Police Scotland uniform to include Muslim hijab
Malawi Defence Force allows Muslim soldiers to wear hijab Malawi 24 | Latest News from Malawi
SOUTH AFRICA ARMY ALLOW MUSLIM WOMAN TO WEAR HIJAB - Google Suche
Serikali haifuati dini yoyote, kwa hivyo hatutegemei serikali isome vitabu vya dini zote duniani ili kutunga sheria zake.Any way kutopiga kelele si mwongozo ktk katiba iliyojipambanua haina dini.
Serikali zinaundwa kwa ridhaa ya makundi tofauti ya dini. Kama chadema na ccm ktk hili munaungana tutaunda chama kitachoaccomodate value za makundi yote ya dini
Kule Afghanistan, Taliban wanaheshimu haki za wakristo?Jeshi na taasisi zote zinatuongoza kwa kufata sheria mama. Katiba.
Mbona nchi nyingi za kidemokrasia zina uelewa huo. Watz tumerogwa na nani. Kwanini hatuna uvumilivu na kuheshimiana value za kila kundi.
Minnesota’s first hijab wearing police woman: how cool is she? - MVSLIM
Police Scotland uniform to include Muslim hijab
Malawi Defence Force allows Muslim soldiers to wear hijab Malawi 24 | Latest News from Malawi
SOUTH AFRICA ARMY ALLOW MUSLIM WOMAN TO WEAR HIJAB - Google Suche
Quote:Unapoliongelea Jeshi basi hakikisha kwanza umeelewa misingi ya uendeshaji wake.
Kuna kitu unasahau mkuu. Katika Social status kuna baadhi ya mambo hayatathiminiwi kwa hali ya kawaida.
Mfano; Kijamii Mwanamme kumpiga mwanamke sio jambo linalokubalika na wengi, haijalishi kosa gani kalifanya kwani kufanya hivyo jamii huona ni ukatili. Ndio maana utasikia watu wakisema
"Haikuwa na haja ya kumpiga angemwacha tu aende kwao"
Walakini akitokea jambazi wa kike basi hata akatokea mwanamume akapambana naye na kumuua basi sifa huenda kwa mwanaume kuwa amefanya kitendo cha kishujaa licha ya kuwa mwanamke yule ameuawa.
Namaanisha kuwa Ipo misingi ya kijeshi ambayo ukiitathimini kwa maisha ya kawaida kwenye jamii utakuta ni Ukatili, Udharirishaji, Unyanyasaji, Upotofu wa mila na desturi au Kutoheshimiwa kwa misingi ya dini. Lakini kumbe misingi hiyo ndiyo yenye kuongeza utendaji bora wa majeshi pamoja na usalama
Najua unaweza waza ina maana gani kwa wanafunzi wanaoenda kuchukua mafunzo kwa mda mfupi?
Kikubwa katika mafunzo haya sio mda bali yale wanayoenda kujifunza. Haitakuwa bora kubadirisha taratibu za jeshi eti kwa sababu ni mambo ya mda kwani kwa kufanya hivyo itakuwa haina thamani kuwepo kwa mafunzo hayo.
MUHIMU ZAIDI NI KUWA yote hayo yanafanyika kwasababu kadha wa kadha, miongoni mwao ni
1. Usalama na Usafi
2. Kutokuwepo kwa Upendeleo wa Kidini
3. Ufanisi wa Mafunzo
4. Kushirikiana na Kujenga Udugu
Wazazi na walezi wanapaswa kutambua jeshi halifanyi hivyo kwa kukinzana na misingi ya kitamaduni au dini bali inatokana na sababu mbalimbali za kiutendaji na kijeshi ambazo zinalenga kuhakikisha usalama, utendaji bora, na umoja wa kikosi.
Ndio maan baadhi ya sheria hazizingatiwi.
Dah! Tanzania watu wengi wa dini zote wana Uelewa wa kiwango cha juu sana kuhusu Imani tofauti zinazopatikana ndani ya nchi hii na ndo mana hawababaishwi na wale wachache wenye Itikadi kali ww ukiwa ni mmoja wapo. Siku zote waTz wanaishi pamoja kwa utulivu na Amani, wakishirikiana pamoja bila kubaguana eti huyu ni kafir, huyu ni nn cjui n.k.n.k. Hata nyie wenye Imani kali bado waTz wanawavumilia na maisha yanaendelea. Watanzania hatutaki na hatutakubali mihemko ya Udini ituvurugie amani yetu.Kuna tofauti ya maana ya dhana ktk serikali.
Ktk nchi za kijamaa serikali kutokuwa na dini ina maana serikali inawadhibiti baadhi ya dini.
Ktk nchi za kiliberari serikali kutokuwa na dini manake inakulinda wenye dini.
Tz eitha watu hawana uelewa au kwa makusudi wameamua kudhibiti wenye dini