Machinga wasilete siasa waondolewe haraka miji yote Tanzania

Machinga wasilete siasa waondolewe haraka miji yote Tanzania

Fremu leo zimedoda mikoa yote, ina maana Machinga wanashindwa kujiunga hata watatu watatu wakachukua fremu wakaripa Kodi?

Nchi imekuwa ya kipuuzi sana mama ntilie wanashindwa kujiunga wakatengeneza taasisi inayolipa Kodi na wakafanya derivali ya chakula kwenye maofisi mida ya mchana?

Mpaka wakae kila Kona ya mtaa. Ebu tuache ushamba basi

Nashauri Machinga wathibitiwe Kama wanagoma vibanda vyao vyote vichomwe hatuwezi kuwa na taifa la watu wasiolipa Kodi, kufuata Sheria na katiba ya Nchi .

Mbaya zaidi kupoka haki za wengine hii haikubaliki hata kidogo lazima tuwe taifa la mfano.

Na mikoa yote ondoeni Machinga wenye mitaji mikubwa wakapange fremu wauze online bidaa zao wafanye derivali.

Wenye mitaji midogo watengewe viwanja vikubwa viwe Kama minada wafanye uko mbona kila mkoa unayo maeneo?

Makala nakushauri vunja kabisa kila kitu maana wabongo Ni wabishi Sana bila kuwavunjia hawataondoka kwa heri.

Tujenge Nchi tuache kufanya kila kitu siasa. Siasa ndio imetufikisha hapa tulipo.
Usisahau Mmawia kaanzisha uzi wa kuwatetea
 
Hayo ni maisha ya watu na ni wapi huko frem hazina watu kama kkoo mbona frem zimejaa tatizo mnataka watu wahangaike wakati wamejiajiri kutafuta riziki.Kama serikali ingekua imewekeza kwenywe viwanda na kilimo vijana wengi wangekua wako kwenye ajira.Hili ni bomu kubwa sana linaandaliwa

Sent from my SM-M305F using JamiiForums mobile app
Hakuna bomu, watengewe maeneo yaliyo bora na watafanya biashara bila shida... tatizo siasa za JPM ndio zimesababisha wakae mabarabarani na kufanya misongamano isiyo na maana. Kuchafua miji.
 
Sawa, warudishieni kwanza fedha za vitambulisho! Wengine walilipia wakiamini serikali italinda biashara zao wasibughudhiwe !
 
umeambiwa usifanye kiki wewe ukakaidi basi utapigwa. ni kuda wa virungu sasa muda wote mji umesongamana kumbe wengi machinga
 
Hali ilikuwa mbaya sana, na waendelee hadi mikoani!
Barabara za mijini siku hizi zinajengwa na sehemu za watembea kwa miguu ili watu tusipate shida ya kupigwa na side-mirror za wenye magari, ajabu sehemu zote wamachinga wametandaza vitu vyao. Ujinga mtupu!!!
 
Yani naona wanapiga siasa tuuu, lazima wafuate utaratibu tuache kudanganyana. Kila lakheri Makala, usirudi nyuma, songa mbeleeeee
Mkuu, hao ndio wanarudi kitaa kutafuta pesa kwa ngeta!
Hivyo tukae mkao wa kutulia, tusubiri yajayo.

Nadhani kungekuwa na smooth transitiin ya maeneo wanayopaswa kufanyia biashara zao, na si kibabe kama ilivyokuwa leo vingunguti.
 
Mjini Kampala ukienda luwum street utaamini hili
Machinga wanajiunga wanne mpaka watano wanakodisha frame ila ndani ya fremu kila mtu anauza chake
Pia hapa Tanzania
ifike mahali machinga waungane wakodi fremu na sio kuhodhi brbr za watembea kwa miguu
Wapi tunafeli kuwapanga machinga kila wakati makundi ya machinga yanaongezeka
Tusitumie nguvu kubwa kuwapeleka kwenye masoko la hasha wapewe elimu ya namna ya kupanga frame kwa watu wanne watano ili nao walipe kodi
 
Dar ni kichafu jamani, embu tutembelee miji ya wenzetu tuone jinsi walivyo wasafi. Kwa hili naiunga mkono ya Mama yetu Rais Samia kuchukua hatua. Huu ujinga huwezi kuukuta hata kwa majiranj zetu hapo bondeni.
 
Mjini Kampala ukienda luwum street utaamini hili
Machinga wanajiunga wanne mpaka watano wanakodisha frame ila ndani ya fremu kila mtu anauza chake
Pia hapa Tanzania
ifike mahali machinga waungane wakodi fremu na sio kuhodhi brbr za watembea kwa miguu
Wapi tunafeli kuwapanga machinga kila wakati makundi ya machinga yanaongezeka
Tusitumie nguvu kubwa kuwapeleka kwenye masoko la hasha wapewe elimu ya namna ya kupanga frame kwa watu wanne watano ili nao walipe kodi
Ukiangalia machinga walivyojaa barabarani unajiuliza nchi hii tuna viongozi wa namna gani! Ikifika jioni barabara nyingine zinafungwa kabisa unakuta nyanya, vitunguu,viazi n.k ndio vimetandazwa chini barabara haipitiki! Halafu bado kuna watu wanatetea! Hivi miaka ya nyuma kulikuwa hamna machinga!??

Prime areas zote zimejaa vibanda, tuache siasa kwenye kila kitu machinga warudi walikokuwa Period.
 
Fremu leo zimedoda mikoa yote, ina maana Machinga wanashindwa kujiunga hata watatu watatu wakachukua fremu wakaripa Kodi?

Nchi imekuwa ya kipuuzi sana mama ntilie wanashindwa kujiunga wakatengeneza taasisi inayolipa Kodi na wakafanya derivali ya chakula kwenye maofisi mida ya mchana?

Mpaka wakae kila Kona ya mtaa. Ebu tuache ushamba basi

Nashauri Machinga wathibitiwe Kama wanagoma vibanda vyao vyote vichomwe hatuwezi kuwa na taifa la watu wasiolipa Kodi, kufuata Sheria na katiba ya Nchi .

Mbaya zaidi kupoka haki za wengine hii haikubaliki hata kidogo lazima tuwe taifa la mfano.

Na mikoa yote ondoeni Machinga wenye mitaji mikubwa wakapange fremu wauze online bidaa zao wafanye derivali.

Wenye mitaji midogo watengewe viwanja vikubwa viwe Kama minada wafanye uko mbona kila mkoa unayo maeneo?

Makala nakushauri vunja kabisa kila kitu maana wabongo Ni wabishi Sana bila kuwavunjia hawataondoka kwa heri.

Tujenge Nchi tuache kufanya kila kitu siasa. Siasa ndio imetufikisha hapa tulipo.
Haya ni mawazo yako, hebu tuwasikie na wao huenda wana hoja zenye mashiko zaidi ya wewe
 
Back
Top Bottom