Madai kwamba Magufuli alimpiga Ben Saanane risasi pale Ikulu isichukiliwe kihisia; hizi hapa ni sababu za msingi kuamini kwamba ni ukweli

Hatuwezi kuvumilia uongo na ulipizaji visasi na kuzusha madai bila ushahidi. Kesho, ataibuka mwingine na utopolo kama huu. Sheria iko wazi kuwa anayedai lazima athibitishe. Ni rahisi na wazi hivyo mwanangu.
Serikali haipo hapa kuchunguza nani kasema uongo adaiwe ukweli mahakamani. Kama unaona Kabendera hajasema ukweli nenda mahakamani kamfungulie kesi kama mtu mwenye interests na Magufuli. Ila kumbuka, wewe unaeshitaki ndio una jukumu la kuonyesha Ben Saanane yuko hai hakuuawa na Magufuli, ili uthibitishe Kabendera kasema uongo. Na ukishindwa kesi utalipia gharama za kesi za Kabendera.
 
kwamba kwa wanaomfahamu Magufuli watakuambia wazi alikuwa hayuko sawa kichwani na kuua mtu kwa risasi ingewezekana kabisa kwake. Huyu ni Magufuli ambae alimpiga sana mtoto wake karibu kumuua kwa kosa la kufeli mitihani tu;
Umenikumbusha ule msiba wa Mtoto wake, mnakumbuka ilisemekana kuwa alikufa kwa kipigo? Wakasema ni malaria! Duh
 
Takataka...


Ni jayo tu!!
 
Sio kila jambo linahitaji kuletewa ushahidi. Kwa mfano wewe, una ushahidi gani kwamba baba yako ndie kweli baba yako? Kuna siku umewahi kumhoji mama yako na kudai ushahidi? Kama hapana, kwa nini hujafanya hivyo?

Sasa tumeshasema, Kabendera kaandika Magufuli alimuua Ben Saanane. Kama unapinga basi andika kitabu uweke ushahidi kwamba Ben Saanane haukuuwawa na Magufuli
 
Kwahiyo na soka naye anaweza kuwa kafanyiwa hivyo hivyo😓😓
Kuna jamaa huko kasema 90% ya taharifa za utekaji na mauaji ni za uongo 🤣🤣🤣 akifikiri ndio kamaliza kuitetea serikali.

Swali ni Je!!? HIZO ASILIMIA 10% ZA TAARIFA HIZO NI ZA KWELI!!? AU ALITAKA KUTHIBITISHA NINI!!?

KAPULIZA AKIWA NA LENGO LA KUZIMA, MATOKEO YAKE KAKOLEZA

Sijui hua hawasomi presentation zao kabla hawaja zi announce au hua hamna washauri wa kupitia report zao
 
Mwezi mchanga ata mimi nimeona hivo

Yaani kuuwa mtu live wanachukulia kama kuchinja kuki sijui [emoji23][emoji23]
"kuuwa mtu live"
Ili mtu auawe anatakiwa asiwe live?
 
Hamna hoja hapa.
 
Wakati magufuli anampiga mke wake ulikua nae?wakati anapiga watoto wake ulikuepo???hakua mkamilifu ila kuchafua legacy yake haitatosha,huyu mwamba ana legacy nzuri kwa taifa hili,alifanya alivyojaaliwa kufanya,aliwaamiisha africa tunaweza.ilikua magufulisation of africa hukuona?ona sasa mali,niger na burkina fapo wamejimagufuli mambo yanaenda.kwahio magufuli na huyu mama yako tukiweka kwenye minzani si utainama upande mmoja.muache mwamba amelala alifanya alichofanya kwan vp
 
Huna hoja zaidi ya kufanyakile kile unachoshauri wenzako wasifanye. Mwache Kabendera ajitetee mwenywe kw akuleta ushahidi. Vinginevyo unatupotezea muda au kutafuta kiki tu. kwa kuanzisha uzi huu
Unajuaje kama alieandika huu uzi sio kabendera
 
Mwandishi au mleta hoja huwa naheshimu maandishi yake sana. Lakini kwa hili, ni hisia zaidi na personal attack kwa JPM, kwamba alikuwa anampiga mke wake, kuna RB yoyote polisi? Au ndiyo hisia tu! Au hoja za kumchapa mwanae alieshindwa mtihani, mbona hata sisi tulichapwa sana na wazazi wetu, na hata walimu tu shule tulizosoma, na leo tunawashukuru.

Kabendera, angelisema kwa mfano, kwa maelezo ya aliyekuwa IGP, CDF wa wakati huo, au mkurugenzi wa Tiss etc, credible sources, wamethibitisha tukio hilo lilitekelezewa Ikulu ya magogoni, kutowataja ni makusudi, alijua angefuatwa.
Kwa namna alivyoliandika ni kama chuki binafsi tu!
 
Kimantiki bado kuna shida katika hii hoja! So many questions remain unanswered. Kwa mfano:
1. Je, hakuwa vizuri kichwani only baada ya kuwa Rais?
2. Kama hakuwa vizuri kichwani hata kabla hajawa Rais, kwanini hakuwahi kupiga risasi watu wengine (katika umri wake wa miaka 60)? Ditopile hakuwa Rais, lakini alimuua driver wa daladala mchana kweupe!
3. Rais anao uwezo wa kumpoteza mtu yeyote kwa kutoa tu maelekezo. What was he trying to accomplish kwa kuamua kumuua yule bwana mdogo kwa mkono wake mwenyewe? Obviously, hakufanya hivyo ili iwe fundisho kwa wengine, kwa sababu umma haukujua juu ya hili. Au alitaka kutoa fundisho kwa victim mwenyewe, which is completely meaningless?
4. Je, kuhojiwa kwa PhD yake kulikuwa more painful kwake (Magufuli) kuliko kuhojiwa kwa legitimacy ya urais wake?
 
Reactions: Cyb
Je Kuna Uwezekano Mkubwa kuwa Rais wetu mpendwa Magufuli aliuliwa?

Watu wengi wamesema na wengine kuandika kuwa huenda Rais Aliuliwa ikasingiziwa Corona.

Je tuwaamini bila ushahidi wa namna alivyouliwa?
 
Hadithi tu hizi, hazina ukweli
 
Kwa hiyo sasa mnatakaje nendeni mkafufue mzimu wa magufuli muulipishe kwa yote uliyofanya

Au ndo mnaleta mada za kupoteza mda uchaguzi uwahi kufika?

Vipi sativa alitekwa na magu?
Vipi tarimo magu ndo alituma watu wakamteke
Na vipi kuhusu nondo?

Hebu mtuletee ushahidi haraka kwamba ni nani aliyetoa amri kuhusu hawa watu maana serikali yote iko madarakani msije baadae mkaanza kujaza servers za JF kusemq sijui blah blah baada ya serikali iliyopo kupita.
"kuuwa mtu live"
Ili mtu auawe anatakiwa asiwe live?
May be
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…