Madaktari wengi ni misukule walio hai

Ngoja nikupe elimu kidogo kwanza daktar,nesi, hawahusiki kabisa na kuvumbua dawa za magonjwa sugu yanayotusumbu huwezi kuelewa sababu upo out of this field.
Acha porojo bwana, ungekuwa makini ungeelewa tafsiri niliyoitoa ya neno "DAKTARI".

Hata ukifungua kitabu chochote unakutana na GLOSSARY inayotoa tafsiri ya maneno husika yaliyotumika katika muktadha wa kitabu husika.

Tafsiri ya neno daktari katika muktadha wa andiko langu inajumuisha hizo kada zingine sijui za utafiti na makorokocho mengine unayoyajua sana.

Sasa unijibu swali, kwanini mmegeuka kuwa misukule?
 
Mwanzo wa andiko langu nimetoa TAFSIRI ya neno DAKTARI.
 
Alafu wengi siku hizi wanatumia google search kutibu wagonjwa. Hata mambo madogo tu ambayo yanahitaji logic ya kawaida, ukimpiga maswali anashindwa kujibu.

Kimsingi, na ukweli wa mambo ni kwamba uponyaji unatoka kwa Mungu tu, haya mengine ni process tu.
 
Full ukanjanja.
 
Umeeleza kisanii zaidi, haujatoa majibu.

Lengo langu sio kutaka kujua AINA ZA VITENGO, lengo langu ni kutaka kujua kwanini kuna misukule nchini katika sekta ya afya!

Sasa unijibu swali, Kwanini kansa haina dawa?
Mkuu BICHWA KOMWE -
Sitaki sana Kuingilia Maisha yako halisia ila inaonekana Ugonjwa wa kansa umekukera sana Inaonekana Umewahi kupoteza Mtu wa karibu kwa ugonjwa huo, Uliofanya Uchukie Watu wote wanaofanya kazi afya..
Naelewa hisia zako..

Maaana kwa kumbukumbu zangu hii sio Conversation ya kwanza kukujibu kwanini kansa haitibiki..Ila leo nitajitahidi kujibu kwa Undani zaidi..
  • Kansa Sio ugonjwa Mmoja: kuna magonjwa zaidi ya 200 ya Cancer na yote yakiwa na aina zake. kwa mfano cancer inaweza ikatokea kwenye ngozi lakini ikawa inavariaty (Utofauti) wa Tabia, Mutation (Jinsi ya kuathirika) na hata different characteristics kwenye same disease patten.. kwa mfano zaidi cancer ikitokea kwenge Epithelial huwa wanaita carcinoma na ikitokea kwenye Tissue au Muscle wanaita Sarcoma sasa inaweza ikatokea mkononi lakini ikawa na Different disease with diferent feature.....
  • Complexity ya Carcinogenic cells au cancer cells: .moja ya Properties ya Cancer cells ni kuacquire mutations ambayo itafanya cells kukua uncontrollably (Bila kizuizi), Na hiyo husababisha ku evade the immune system,na hapo sasa Bichwa ndo hutokea resistance to treatment (Au tunaita Usugu wa Matibabu).. Na hapa ndo huwa ngumu hasa kwamba tutarget ipi cells iliyi nzima au iliyokufa na ukumbuke Inakuwa kwa haraka sana.
  • adaptation: Cancer cells are constantly evolving, acquiring new mutations kila siku ambayo inafanya ziweze ku resist matibabu..Yaani tuseme kwa mfano wamegundua Dawa leo ya matibabu labda kwa ajili ya mutants A wanamaliza kutengeneza Dawa wanakuta cancer ina Mutants C..Kwahyo ni very challengig..
  • Heterogeneity within tumors hii nimezungumzia sana unaweza kuta Tumor moja tu ina diversity kibao na ina aina zaidi ya 100 ya cancer cells na ukiangalia ni kauvimbe kadogo tu ila kukacontrol inabidi utafute dawa 500 kwa wakati mmoja na ndo maana ubora ukawa ni chemotherapy na Radiotherapy kuziua hizo cells kabla hazijaharibu cells zingine..
KUtibu cells inayobadilika kila saa ni vigumu sana sawa na kutibu ugonjwa usioJua hasa unasababishwa na nini..

Kumbuka kwanza cancer sio ugonjwa unaotokana na Mdudu wala Bacteria wala virus..
Ila unatokana na mabadiliko ya cells za mwili ..
Ukiwahi mapena matbabu kabla haijafika kwenye advance stage unaweza ukapona lakini ikifika stage 3 mpaka stage 4 hakuna ujanja..

Nakukaribisha kwa swali jingine
 
Utakuwa ulikosa nafasi ya kusoma u-daktari! Pole sana kwa kweli!
 
Likiugua hapo litajambajamba kwenda hospitali! Sijui litatibiwa na nani?
 
Una taaluma gani mkuu... Tuanzie hapa
 
Unaweza ukawa na ukweli kidogo. Ila nadhani andiko lako limejaa chuki. Wasije wakawa wamekuumiza kimapenzi. Yaani madaktari wote waliopo bongo wanaookoa ndugu zetu wako hivyo? Wapi madaktari wazuri zaidi tukawachukue na kuwaweka Tanzania, ambako hata consultation fee ya daktari ya shilingi 8,000/= serikali inataka iiondoe kwa sababu wananchi hawawezi afford? Tanzania ni kati ya nchi za Africa ambazo mifumo yake ya afya ni mozuro sana. Usisikilize story za vijiweni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…