Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo

Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo

Usichojua ni kwamba dereva sio kwamba anapaki kwa bahati mbaya, hapana kuna vigezo na masharti umpelekea kupaki kwenye hotel hiyo, sharti la kwanza mwenye hotel lazima atoe hela kwa dereva nadhani ni sh 10,000 au 20,000 pili sahani moja bure ya dereva, tatu toileti ziko sawa, nne anauwezo wa kuhudumia watu 50+ kwa muda mchache yaani dk 15? , tano parking.Uzuri na bei ya chakula sidhani kama wanazingatia, vigezo ni hivyo hapo.
Maelezo mazuri sana mkuu, changamoto ipo hapa 👇👇.

parking.Uzuri na bei ya chakula sidhani kama wanazingatia, vigezo ni hivyo hapo.
 
Pamoja na hayo maeneo na bei zao na chakula kisicho na radha.

Mm nakereka sana na dakika 10 za kupata HUDUMA. HII ni nini? Utakuta abiria wanakimbizana kama Swala Pala.

Mahoni hovyo hovyo NO ustaarabu, japo kidogo tujaribu ustaarabu HAKUNA uchelewaji kwa kupata huduma dk 20 safari itakuwa vilevile.
 
Kama hakuna parking? au mwenye hotel hataki kutoa cha juu kwa dereva na sahani 1 ya bure unadhani dereva atasimama hapo?
😄😄, Sahani 1, Aise sisi Waafrika ni taabu sana,
 
Pamoja na hayo maeneo na bei zao na chakula kisicho na radha.

Mm nakereka sana na dakika 10 za kupata HUDUMA. HII ni nini? Utakuta abiria wanakimbizana kama Swala Pala.

Mahoni hovyo hovyo NO ustaarabu, japo kidogo tujaribu ustaarabu HAKUNA uchelewaji kwa kupata huduma dk 20 safari itakuwa vilevile.
Mkuu zamani mnakaa saa nzima maana na dereva kachoka kufukia mashimo anapumzika.
Siku hizi ni mbio tu
 
Mimi nachangia tu kuwa
Zile hoteli wanazopaki ni safi, na huduma nyingine za kijamii ni nzuri (Usafi umeboreshwa)
Pendekezo; waweke pia vyakula vya watu wa kawaida
mfano: Wali maharage au wali mboga mboga, (maandazi/Chapati/chai) Chips kavu za buku au pengine
viazi vya kukaanga vya 500/buku nk nk
Ni sahihi mkuu, mambo yataenda vizuri kabisa, Biashara siyo kuweka bei vitu juu, Biashara ibebe hela kuazia 100 kwenda mbele.
 
Usichokikumbuka ni kuwa kipindi cha uchaguzi hela inamwagwa kwa maskini huko kuwapumbaza pamoja na hizo kofia na tsheti.
😐😐, Viongozi ni watu waajabu sana,, Na wa Tz tulivyo mambo yote tunasahau kabisa kabisa.
 
😐😐, Viongozi ni watu waajabu sana,, Na wa Tz tulivyo mambo yote tunasahau kabisa kabisa.
Shida ya watanzania ni ukosefu wa akili sababu ya njaa inayopelekea unafiki na ubinafsi. Mtanzania ni mwepesi sana kugeuka chawa na kuwasaliti wenzie endapo akisogezewa kamrija kadogo ka kulamba asali.

Yani kwenye kundi la wabongo 100 wenye lengo moja ukichagua viherehere kumi tu na kuwaweka kwenye payroll yako utashangaa hao kumi watakuwa upande wako na kukupa ushirikiano wa kuwahujumu wale wenzao 90 kwa namna yeyote ile wawezayo huku wakijifanya wako pamoja nao.

Hio ndio tabia halisi ya mtanzania na kwakuwa tunajuana kila mtu anaona ni upuuzi kuwa protestant. Wanayaacha mambo kama yalivyo alimradi kila mtu anakula na kushiba na familia yake.
 
Pamoja na hayo maeneo na bei zao na chakula kisicho na radha.

Mm nakereka sana na dakika 10 za kupata HUDUMA. HII ni nini? Utakuta abiria wanakimbizana kama Swala Pala.

Mahoni hovyo hovyo NO ustaarabu, japo kidogo tujaribu ustaarabu HAKUNA uchelewaji kwa kupata huduma dk 20 safari itakuwa vilevile.
Dakika 10, kwa ajili ya kula ni ndogo sana, Abiria wanapelekeshwa utadhani, tunaenda kuwahi vitu vya maana tunakoenda.
 
Shida ya watanzania ni ukosefu wa akili sababu ya njaa inayopelekea unafiki na ubinafsi. Mtanzania ni mwepesi sana kugeuka chawa na kuwasaliti wenzie endapo akisogezewa kamrija kadogo ka kulamba asali.

Yani kwenye kundi la wabongo 100 wenye lengo moja ukichagua viherehere kumi tu na kuwaweka kwenye payroll yako utashangaa hao kumi watakuwa upande wako na kukupa ushirikiano wa kuwahujumu wale wenzao 90 kwa namna yeyote ile wawezayo huku wakijifanya wako pamoja nao.

Hio ndio tabia halisi ya mtanzania na kwakuwa tunajuana kila mtu anaona ni upuuzi kuwa protestant. Wanayaacha mambo kama yalivyo alimradi kila mtu anakula na kushiba na familia yake.
Hii ni huzuni sana, maana kwa style hii, hata nchi kuipeleka mbele inakuwa ngumu sana, wanafiki ni wengi kuliko wenye Nia njema na uelewa wa kutatua mambo.
 
Utabadilishaje gari, wakati magari yote yaendayo Mikoani inafanya huo upuuzi!


Usafiri upi, Ndege? Kama chakula tu shida hizo garama za choppa anatoa wapi?
Option zipo tatu

1. Badili basi
2. Badili usafiri
3. Badili ulaji wako

Zamani sisi tulikuwa tunaandaa chakula chetu wenyewe kwa ajili ya safari, kuepuka huo upuuzi
 
Back
Top Bottom