Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo


Alafu kitu kingine upo safari safarini unakula kula ili iweje? Si unywe hata soda na biskuti ukifika unapokwenda utakula vizuri
Kwa nini, ulazimishe mtu aishi unavyotaka wewe?,

Binafsi ninapo safiri huwa nanua tende,maji na soda Basi mpka nafika silagi kitu kingine.
• Hivyo vyakula ulivyo taja hapo ni hobby yako wewe siyo mtu mwingine,
• Waache Abiria wachague wanacho taka, Siyo kupelepelekwa kama mfungwa.
 
na ndiyo aina ya viongozi tulionawo hawajali wananchi zaidi ya kushindana kupiga madili na kurishana madaraka
• So sad, binadam mwenzie anavyo teseka yeye ndo anafurahia, Kweli Africa is dark content.
• muafrika yupo tayari kumpa ardhi mzungu/muarab, alafu anamnyima muafrika mwenzie.
 
Muwe mnavumilia, njaa ya siku moja haiwezi kukuua.
Kusafiri sio mateso kuvumilia kitu gani?ile ni adventure tu.
Tunachoongea hapa mtu unafika stendi unakula na dereva anapumzika.
Tuliopanda ma Leyland enzi hizo ni saa nzima injini inapoa.
Mnakimbilia wapi?
Singida-Dom masaa 8 hapo njiani mshabondwabondwa sana kwenye mashimo.
Dom-Ira kupitia mtera kipindi cha mvua njiani siku 2.
Mbeya-Dar barabara yao nzuri tu ila ndo hivyo kufika usiku tu hata afanyaje.
Ndo wakaja,kina Zainab,tawaqal,southern comfort fujo zikaanza.
Siku hizi hizo Scania na yutong wanabet huku wamebeba maisha ya watu.
Kuna siku ndani ya bus kwenda Mbeya.
Dereva tumeanza nae vizuri tu.
Kufika iringa kapotea,bus yule konda kapewa.
Likawa linapepezwa km ndege ile inaenda kupaa.
Ndio niliacha kupanda Mabus.
Madereva ni wahuni tu siku hizi.
Zamani walikua watu wazima wenye kujitambua.
Sio sasa
 
Hili tatizo limezungumzwa sana hapq ila serikali imeweka pamba masikioni. Angalau ujio wa safari za usiku utapunguza tatizo hili kwani unajilia nyumbani jioni kabla ya kusafiri.
 
Kipindi chenu, mulisafiri kistaarabu sana, ila kwa Sasa ni changamoto kubwa sana.
Kabisa,gari ikikwama ndo mnachimba dawa,mnarudi mnasukuma wenyewe.
Likitoka na matope yetu.dere atangoja tu mjae wote maana mbele hajui kitachotokea.
Mkijaa mnaanza tena,ni pori kwapori njia mbaya.
Hamuachi mtu njiani
Maana kiwaacha huko mbele nani atasukuma bus?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…