Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo

Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo

Jali afya yako unapoondoka nyumbani una hakikisha una vyakula vya kukaanga kama kuku au nyama na chapati zako kabisa na chupa za maji
Hapo utaishinda njaa na safari

Kula hovyo tatizo hao wanauza mpaka vilivyolala na ukianza kulalamika tumbo unalaumu tena
Kiukweli hoteli za vyakula barabarani huwa bei kubwa sio Bongo tu ni kila mahali duniani
Ukienda hata Ulaya ni hivyo hivyo tena utashangaa wanavyopandisha bei mpaka unanunua kwa shingo upande
Kwa bongo huwa najipanga toka nyumbani, sio kwa sababu ya bei hapana bali naogopa kuanza kumsumbua konda
 
Mkuu ndio maana kuna mikate na soda/juice za kopo. Kama ukigundua madreva wanapaki basi sehemu za gharama ya juu dawa ni kusafiri na mikate, viazi au mabumunda uwe unakula njiani taratibu bila shuruti mkuu.
Mkuu, we unahisi haiwezekani kubeba vitumbua kwenye Rambo?

• Lengo ni kutatua tatizo, Yani siku zima ushindie mikate na juice, ?
 
Kabisa mkuu, Hili suala liangaliwe upya,
Sijui wanatuchukuliaje wasafiri sababu hatuna option nyingine🤔 ila kuna siku nilienda Moshi na Kilimajaro Express sijui ni hotel yao ile atleast wanajitahidi chips safii nikashangaa maana nishazoea Mbeya kwetu mwendo mdundo chips zimepoaa 😀(sijui ni ulafi ila lazima nile njiani)
 
Serikali yetu - mamlaka husika tunaomba mtusaidie sisi wanyonge na hii tabia ya madereva inayozidi kushamiri kila kukicha, hasa kwa wale ndugu zetu wanaosafiri mikoa ya mbali wanapata tabu sana kuhusu masuala ya chakula.

• Dar - - mwanza
• Dar - - mbeya
• Dar - - kigoma
• Dar -- Arusha
• Dar -- Ruvuma

Kuna tabia na utaratibu wa mabasi walio jiwekea bila kuhofia abiria wao, sio rafiki kabisa, wanapaki mabasi yao sehemu ya chakula bei zao ziko juu sana bila kujali abiria mifukoni mwao/kipato walicho nacho. Karibia vituo vyote wanavyo paki hawa madereva unakuta Chakula cha bei ya chini ni kuazia elfu Tsh7000/- hadi elfu Tsh8000/- na kuendelea, na ukiangalia hicho chakula hakina hadhi ya kuuzwa bei kwa hiyo, alafu chakula kinakuwa ni kidogo ikiwa mtakua watu wawili hamuwezi kushiba.

Jana nilikuwa natoka Dar kuja Mbeya tulipofika sehemu ya chakula, niliongozana na mama mmoja mwenye watoto wa 3 alivyo ambiwa chakula bei ya mwisho ni elfu Tsh7000 alikuwa mnyonge sana, na kiasi alichokuwa nacho taslimu alikuwa na elfu Tsh5000 tu, ikambidi anunue soda na biscuit, roho iliniuma sana.

1. Madereva mnadhani kila mtu anapesa ya kununulia hicho chakula cha bei ya juu?

2. Au sehemu mnazopaki kwa ajili ya watu kula ni za viongozi wa ngazi za juu huko serikalin?


Ombi langu kwa Serikali tunaomba mtoe tamko/sheria kwa mabasi yote, yawe yanasimama kwenye mji ulio na huduma kamilifu ili abiria wote wapate huduma stahiki
Wapande ndege dkk 45 to 60 wapo kwao hizo expenses za misosi wataziepuka
 
Jali afya yako unapoondoka nyumbani una hakikisha una vyakula vya kukaanga kama kuku au nyama na chapati zako kabisa na chupa za maji
Hapo utaishinda njaa na safari

Kula hovyo tatizo hao wanauza mpaka vilivyolala na ukianza kulalamika tumbo unalaumu tena
Kiukweli hoteli za vyakula barabarani huwa bei kubwa sio Bongo tu ni kila mahali duniani
Ukienda hata Ulaya ni hivyo hivyo tena utashangaa wanavyopandisha bei mpaka unanunua kwa shingo upande
Kwa bongo huwa najipanga toka nyumbani, sio kwa sababu ya bei hapana bali naogopa kuanza kumsumbua konda

Jali afya yako unapoondoka nyumbani una hakikisha una vyakula vya kukaanga kama kuku au nyama na chapati zako kabisa na chupa za maji. Hapo utaishinda njaa na safari

Upo sahihi kabisa mkuu, lakini Madereva wastulazimishe tukale sehemu fulani.. Basi lisimame sehemu ambayo kila mtu awe na uhuru wa huduma.
 
Sijui wanatuchukuliaje wasafiri sababu hatuna option nyingine🤔 ila kuna siku nilienda Moshi na Kilimajaro Express sijui ni hotel yao ile atleast wanajitahidi chips safii nikashangaa maana nishazoea Mbeya kwetu mwendo mdundo chips zimepoaa 😀(sijui ni ulafi ila lazima nile njiani)
😄 Siyo ulafi mkuu, safari ya masaa kumi na mbili kwenye basi, njaa lazima uipate tu.
 
Back
Top Bottom