Madhara ya kumdanganya Mwanamke wakati Unamtongoza

Madhara ya kumdanganya Mwanamke wakati Unamtongoza

hakuna mwanamke anaependa mwanaume mkweli , amini na waambieni wanaume wenzangu..

Kama unataka mwanamke akuelewe sana wewe changanya changanya ukweli na uongo uongo.. ila usifake maisha.

sasa jifanyeni ni wa kweli mtakuja kulia kilio cha uchungu mkali sana. shauri yenu
 
Watu hawajuagi tu, wanaambizana mwanamke bila kumdanganya humpati asa yote hayo ya nini unamdanganya mtu una hela kumbe mwenzangu na mie mwisho wa siku uje kuumbuka. Ukweli humuweka mtu huru siku zote. Na ukiona umemuambia ukwel mwanamke kachomoa ujue kabisa sio fungu lako usilazimishe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Upo sahihi kbsa mkuu,sema watu ckuiz hawataki kushindwa[emoji23]
 
Kuna jamaa mmoja mbongo anaishi South alikutana na demu mkali bank (FNB). Jamaa alikuwa anatoka demu anaingia, mshkaji alikuwa amevaa Tshirt ya bank ya promotion.

Baada ya kuomba namba na kuanza mawasiliano, akamwambia demu kuwa anafanya kazi bank. Demu akaamini na mahusiano yakaanza.

Ikabidi jamaa aingie gharama za kijinga ili kubalance maisha yake na uongo aliotoa. Kama ilivyo kwa wabongo wengi South jamaa alikuwa anaishi geto kwa mafungu (chumba kimoja watu wengi), ikabidi aanze kuazima ghetto la mshkaji, vizinga vya demu vilikuwa vikubwa akiamini jamaa ni banker ikabidi aanze kukopa maana hakutaka kuonekana mnyonge kwa demu pisikali.

Alikuja kuumbuka siku moja yupo kazini, alikuwa anafanya kazi petrol station. Daladala (wanaziita taxi) ikaingia kuweka mafuta, ilikuwa hiace quantum na demu kakaa siti ya nyuma kabisa dirishani karibu na tank.

Jamaa hana hili wala lile na gwanda lake la Shell anaweka mafuta kwenye gari hiyo hiyo kuinua jicho ana kwa ana na demu wake. Mbaya zaidi kwa ndani ya fulana ya kazini ile flana ya bank ilikuwa inaonekana.

Kwa kipindi hicho demu ilikuwa anaelekea kwa mshkaji maana jamaa alikuwa anamalizia shift akajlie mzigo geto kwa rafiki yake.

Demu hakupokea tena simu na ndio ukawa mwisho wa mahusiano.

Kwa vile demu aliacha vitu vyake kwa alipodhani ni kwa mshkaji, siku anaenda kuvichukua akakutana na mwenye ghetto wa kweli. Muuza ngada mwenye hela zake.

Muuza ngada akapindua meza na kujichukulia demu yeye. Jamaa aliedanganya ilikuwa akienda kwa swahiba yake anamkuta demu wake ambae kwa sasa ilibidi amuite shemeji tena.
Hii Ngumu Nyeusi..
 
Kuna jamaa mmoja mbongo anaishi South alikutana na demu mkali bank (FNB). Jamaa alikuwa anatoka demu anaingia, mshkaji alikuwa amevaa Tshirt ya bank ya promotion.

Baada ya kuomba namba na kuanza mawasiliano, akamwambia demu kuwa anafanya kazi bank. Demu akaamini na mahusiano yakaanza.

Ikabidi jamaa aingie gharama za kijinga ili kubalance maisha yake na uongo aliotoa. Kama ilivyo kwa wabongo wengi South jamaa alikuwa anaishi geto kwa mafungu (chumba kimoja watu wengi), ikabidi aanze kuazima ghetto la mshkaji, vizinga vya demu vilikuwa vikubwa akiamini jamaa ni banker ikabidi aanze kukopa maana hakutaka kuonekana mnyonge kwa demu pisikali.

Alikuja kuumbuka siku moja yupo kazini, alikuwa anafanya kazi petrol station. Daladala (wanaziita taxi) ikaingia kuweka mafuta, ilikuwa hiace quantum na demu kakaa siti ya nyuma kabisa dirishani karibu na tank.

Jamaa hana hili wala lile na gwanda lake la Shell anaweka mafuta kwenye gari hiyo hiyo kuinua jicho ana kwa ana na demu wake. Mbaya zaidi kwa ndani ya fulana ya kazini ile flana ya bank ilikuwa inaonekana.

Kwa kipindi hicho demu ilikuwa anaelekea kwa mshkaji maana jamaa alikuwa anamalizia shift akajlie mzigo geto kwa rafiki yake.

Demu hakupokea tena simu na ndio ukawa mwisho wa mahusiano.

Kwa vile demu aliacha vitu vyake kwa alipodhani ni kwa mshkaji, siku anaenda kuvichukua akakutana na mwenye ghetto wa kweli. Muuza ngada mwenye hela zake.

Muuza ngada akapindua meza na kujichukulia demu yeye. Jamaa aliedanganya ilikuwa akienda kwa swahiba yake anamkuta demu wake ambae kwa sasa ilibidi amuite shemeji tena.
[emoji23][emoji23] vijana wanapata tabu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati unajifunza kutongoza unaweza danganya. Utadanganya kwa vile vitu vinavyokufanya uonekane una thamani. Nyumba, pesa, gari au unajuana na watu wakubwa.

Lakini haina maana ndo ukalie njia hiyo hiyo miaka yote. Ni muhimu ujifunze kumvutia na kumtunza mwanamke kwa mfumo unaosema ukweli na unaomfanya mwanamke akutake zaidi ye mwenyewe.

Hizi ni baadhi ya sababu kwanini usitegemee mfumo wa kudanganya kwenye kumvutia mwanamke.

Ni mfumo dhaifu.
Ni njia rahisi na ya haraka kumpata mwanamke. Lakini haina misingi mizuri.
Haina matokeo kwa muda mrefu. Hata maneno yako yanakua hayatoki moyoni.

Utapata urahisi kwa wanawake wasio na uzoefu wa wanaume, ila wale wenye uzoefu wataona uongo wako. Ni heri ujifunze kumvutia mwanamke bila kumdanganya kuliko kudanganya na kutumia muda mwingi kukumbuka uongo/ kukwepa uongo.

Utajisikia ushindi zaidi kwa kumpata mwanamke bila kumdanganya. Na utapa kujiamini zaidi.

Inaharibu mahusiano ya muda mrefu
Kwa mapenzi ya haraka haraka uongo utakusaidia. Lakini mahusiano ya muda mrefu atagundua tu ulipodanganya.

Ataona maisha yenu yote mliyoishi ni uongo. Na hatakua na haja ya kuendelea kuishi kwenye uongo. Na itakua ngumu kuweka mipango naye ya maisha. Hivyo, kama unataka mahusiano ya muda mrefu jiepushe na uongo.

Uongo unazaa uongo
Shida kubwa ya uongo ni kuutunza.
Ukisema uongo mmoja, inabidi uufiche na uongo mwingine mara mbili. Na uongo uongo marambili inabidi uufiche na uongo mara tatu. Mwisho wa siku unajikuta umejaa uongo.

Kitu kitakachozuia kujenga mahusiano imara kwa muda mrefu. Uongo pia unazaa na kuchochea tabia zingine zisizofaa.

Utavutia waongo wenzako
Ndege wafananao huruka pamoja.
Utajikuta kila mwanamke unayekua naye anakudanganya danganya tu. Kitu kitakachokufanya uamini zaidi kwenye uongo. Na kurudia mzunguko huo huo kwa kila mwanamke unayekua naye.

Cha msingi ni kujiepusha na uongo usio na maana. Na ili kuepuka uongo kirahisi, usijiweke kwenye mazingira yatakaokufanya useme uongo baadaye. Yaani jiepushe na vyanzo vya uongo.

Na hata ukitumia uongo, usiutumie sana kiasi kwamba ukashindwa kujitetea.

Share na Wengine Wapate Kujifunza.
Wanawake bila uongo huwezi wapata unless uwe na maisha, au cheo
 
Why not mkuu, mdada akipenda anapenda kweli, maisha yanatafutwa hata hao wenye maisha mazuri walitafuta so ni suala la muda tu

Hiki uliichoongea ni Sawa na Yule dada ambae anaongea biashara ya watermelon ambavyo inalipa haha haha

Ingia kwenye fld sasa ndio utajua ujui
 
Japo mimi si mmoja wao😜 ila naamini na nna rafiki zangu wamependana na kuanzia chini pamoja
You are one of them..😂😂...usijitenge

Kama rafikk zako wapo hivyo na wewe utakuwa miongoni mwao...ndege mnaofanana mnaruka pamoja
 
Back
Top Bottom