Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Kauli ya Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, kuzitaka Halmashauri zilizonunua mashangingi ya bei mbaya mkoani Mwanza, kujieleza, imeendelea kuungwa mkono.
Baadhi ya madiwani wa Manispaa ya Temeke Jijini Dar es Salaam, wameibua madai mazito wakidai sheria ya manunuzi ya umma haikuzingatiwa wakati wa ununuzi wa gari la Mkurugenzi wao.
Badala yake, madiwani hao wanamlalamikia Mkurugenzi huyo Lusubilo Mwakabibi, wakidai alitumia ubabe kuilazimisha kamati ya zabuni kutekeleza matakwa yake.
Gari lililonunuliwa na manispaa hiyo ni Toyota Landcruser VXR, kwa bei ya milioni 470, huku wadau wa maendeleo wakidai manispaa inakabiliwa na changamoto nyingi za kijamii.
Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa vyumba vya madarasa kwa shule za msingi, Sekondari pamoja nakukosekana ama ukamilishwaji wa vituo vya afya.
Madiwani hao walidai japo matatizo ya kijamii Temeke yasingemalizwa na milioni 470 zilizotumika, lakini zingesaidia kupunguza adha za kijamii katika Manispaa hiyo kongwe.
Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alipotakiwa kutolea ufafanuzi suala hilo, hakutaka kulizungumzia kwa kina, badala yake alikiri kuwa ni kweli wamenunua gari hilo.
Pia soma> Wito: Waziri Jafo tumeona maelekezo ya Geita na Mpanda ni maamuzi mazuri, Temeke je?
“Ni kweli, tumenunua gari hilo, lakini sina majibu kuhusu hilo, mimi ni mtumishi, kuna mamlaka zinazoweza kutoa majibu kwa niaba yangu kuhusu suala hilo, asante.” alisema Mwakabibi.
Mbali na ununuzi wa gari, pia wamedai kuna ubabe unaotekelezwa na Mkurugenzi huyo kwa watumishi wa idara ya mbalimbali ikiwano ile ya zabuni na manunuzi, matumizi ya ovyo ya fedha za Umma kwa ajili ya ukarabati wa ofisi yake na thamani za ofisi hiyo.
Pia walidai fedha zinatumika bila kuidhinishwa na kamati ya Fedha, kwa
ajili ya kazi zikiwemo ukarabati wa nyumba na ununuzi wa thamani za ofisi na nyumbani kwa mkurugenzi zikiwamo TV kubwa.
“Kuna kamati iliyokuja kuchunguza mambo kadhaa Temeke, kamati ile kwa hakika haikufanya kazi, badala yake imeacha majeraha kwa watumishi waliohojiwa.” aliongeza kusema diwani mwingine.
Madiwani hao wamemuomba Waziri Mkuu, kuchukulia hatua kali dhidi ya mambo yaliyotekelezwa na Mkurugenzi huyo na wengine aliosaidiana nao, ili kuwa fundisho.
Wamesema hawataki kumfundisha kazi Waziri Mkuu, lakini wanashauri, Mkurugenzi huyo asimamishwe kazi, ili kupisha uchunguzi wa mambo mbalimbali, likiwamo suala la kudhalilisha watumishi.
Waliongeza kusema kuwa, wapo watumishi waliofikisha madai yao kwa ngazi za Wilaya, kwa maana ya ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo wakati huo, DC Felix Lyaniva, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa.
“Huyu ndio mkurugernzi wa kwanza Tanzania kutengeneza mahabusu maalumu ya watumishi, yaani mtumishi akichelewa kazini anawekwa mahabusu, ameweka kontena Manispaa kwa ajili hiyo, mtumishi anakaa mahabusu masaa kadhaa.” alisema mmoja wa diwani.
Waziri wa TAMISEMI Sulemani Jaffo, ambaye ndiye mamlaka ya nidhamu ya wakurugenzi nchini, hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo, lakini madiwani hao walidai kumfikishia barua ya malalamiko.
Baadhi ya madiwani wa Manispaa ya Temeke Jijini Dar es Salaam, wameibua madai mazito wakidai sheria ya manunuzi ya umma haikuzingatiwa wakati wa ununuzi wa gari la Mkurugenzi wao.
Badala yake, madiwani hao wanamlalamikia Mkurugenzi huyo Lusubilo Mwakabibi, wakidai alitumia ubabe kuilazimisha kamati ya zabuni kutekeleza matakwa yake.
Gari lililonunuliwa na manispaa hiyo ni Toyota Landcruser VXR, kwa bei ya milioni 470, huku wadau wa maendeleo wakidai manispaa inakabiliwa na changamoto nyingi za kijamii.
Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa vyumba vya madarasa kwa shule za msingi, Sekondari pamoja nakukosekana ama ukamilishwaji wa vituo vya afya.
Madiwani hao walidai japo matatizo ya kijamii Temeke yasingemalizwa na milioni 470 zilizotumika, lakini zingesaidia kupunguza adha za kijamii katika Manispaa hiyo kongwe.
Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alipotakiwa kutolea ufafanuzi suala hilo, hakutaka kulizungumzia kwa kina, badala yake alikiri kuwa ni kweli wamenunua gari hilo.
Pia soma> Wito: Waziri Jafo tumeona maelekezo ya Geita na Mpanda ni maamuzi mazuri, Temeke je?
“Ni kweli, tumenunua gari hilo, lakini sina majibu kuhusu hilo, mimi ni mtumishi, kuna mamlaka zinazoweza kutoa majibu kwa niaba yangu kuhusu suala hilo, asante.” alisema Mwakabibi.
Mbali na ununuzi wa gari, pia wamedai kuna ubabe unaotekelezwa na Mkurugenzi huyo kwa watumishi wa idara ya mbalimbali ikiwano ile ya zabuni na manunuzi, matumizi ya ovyo ya fedha za Umma kwa ajili ya ukarabati wa ofisi yake na thamani za ofisi hiyo.
Pia walidai fedha zinatumika bila kuidhinishwa na kamati ya Fedha, kwa
ajili ya kazi zikiwemo ukarabati wa nyumba na ununuzi wa thamani za ofisi na nyumbani kwa mkurugenzi zikiwamo TV kubwa.
“Kuna kamati iliyokuja kuchunguza mambo kadhaa Temeke, kamati ile kwa hakika haikufanya kazi, badala yake imeacha majeraha kwa watumishi waliohojiwa.” aliongeza kusema diwani mwingine.
Madiwani hao wamemuomba Waziri Mkuu, kuchukulia hatua kali dhidi ya mambo yaliyotekelezwa na Mkurugenzi huyo na wengine aliosaidiana nao, ili kuwa fundisho.
Wamesema hawataki kumfundisha kazi Waziri Mkuu, lakini wanashauri, Mkurugenzi huyo asimamishwe kazi, ili kupisha uchunguzi wa mambo mbalimbali, likiwamo suala la kudhalilisha watumishi.
Waliongeza kusema kuwa, wapo watumishi waliofikisha madai yao kwa ngazi za Wilaya, kwa maana ya ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo wakati huo, DC Felix Lyaniva, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa.
“Huyu ndio mkurugernzi wa kwanza Tanzania kutengeneza mahabusu maalumu ya watumishi, yaani mtumishi akichelewa kazini anawekwa mahabusu, ameweka kontena Manispaa kwa ajili hiyo, mtumishi anakaa mahabusu masaa kadhaa.” alisema mmoja wa diwani.
Waziri wa TAMISEMI Sulemani Jaffo, ambaye ndiye mamlaka ya nidhamu ya wakurugenzi nchini, hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo, lakini madiwani hao walidai kumfikishia barua ya malalamiko.