Madiwani wa Temeke: Mkurugenzi alitumia ubabe kununua gari la milioni zaidi ya 400

Madiwani wa Temeke: Mkurugenzi alitumia ubabe kununua gari la milioni zaidi ya 400

Huyo Diwani aache uzwazwa. Huyo Mkurugenzi alijiandikia mhutasari wa kikao cha maazimio ya baraza la madiwani bila ya ridhaa ya madiwani?

Mbona wanakosa ujasiri wa kusimamia maamuzi yao?
Baraza la Madiwani lilivunjwa mwezi June mpaka Julai zikafiatwa kura za maoni, Kampeni Agosti mpaka Oktoba, Uchaguzi wamekuja kuapishwa Novemba.

kwa hiyo waliobaki ni Mawaziri na wengineo wote.

sasa Diwani ni wapi kkahusika wakati muidhinishaji ni Ofisi ya Waziri Mkuu?
 
Huu ni uwongo uliotukuka,

Mwakabibi kama binadamu ana mapungufu yake mengi tu.... ila kwa haya mnayosema hapana... uwepo wa mahabusu kwa ajili ya watumishi wachelewaji ni uzushi uliotukuka kabisa.

Hiyo mahabusu isemayo ni kwa ajili ya watu wanaokamatwa kwa kutokuwa na leseni za biashara na vibali vinginevyo mpaka pale wanapokamilisha vitu hvyo kwa siku husika inaposhindikana jioni hupelekwa kituo cha polisi chang'ombe.

Kinachoendelea kwa sasa ni smear campaign against Mwakabibi kwa kuwa Madiwani wengi wana tabia ya kuendesha halmashauri kama mali yao binafsi... hivyo na hulka ya Mwakabibi ni mtu ambaye amekuwa akiwakazia kwenye mambo mengi wanayotaka yaende kinyemela tu tangu awamu iliopita (2015-2020) tena kwakuwa madiwani wengi ni wale wale wamerudi.

Hivyo wanajua maisha ya kumuendesha Mkurugenzi hayatafanikiwa ikiwa ataendelea kuwa Mkurugenzi yule yule... wanachokifanya ni kumchafua tu.. ili aondolewe aletwe Mkurugenzi wataoweza kummudu wao.
 
Baraza la Madiwani lilivunjwa mwezi June mpaka Julai zikafiatwa kura za maoni, Kampeni Agosti mpaka Oktoba, Uchaguzi wamekuja kuapishwa Novemba
kwa hiyo waliobaki ni Mawaziri na wengineo wote
sasa Diwani ni wapi kkahusika wakati muidhinishaji ni Ofisi ya Waziri Mkuu?
Gari la mkurugenzi halijanunuliwa baada ya baraza la madiwani kuvunjwa.
 
Kuna tetesi kwamba ili kuzima jambo hili hata yule aliyesimamishwa atarejeshwa , Musukuma atabaki na aibu
Msukuma haogopi aibu, anadai yeye ni la 7 na akamfumua Mkulu na Hotel yake ya Chato ya vitanda 50 je akikosa wateja atajuweje
sema hao Wakurugenzi watawekwa benchi au kubadilishwa
 
Mtoto wa Magufuli. Alisaidia ushindi wa CCM kule kwa Chiza. Baada ya kumtangaza Chiza akahamishwa usiku huo huo. Kuletwa Temeke. Kama akiweza sema hawezi kuongea na mwandishi wa habari, atashindwaje kuwa na mahabusu ofisini kwake. Tanzania ya Magufuli ina furahisha. Kila mmoja ni boss kwa nafasi yake..
Siyo kweli hata kidogo - hajawahi kufanya kazi Kakonko
 
Majaliwa ni jipu.Yeye ndo anaidhinisha manunuzi hayo, baada ya JPM kulalamika kaamua kugeuka. Ningekuwa JPM ningemtumbua PM
Kwa kufikiri kwako unaona waziri mkuu mwenyewe personally ndiye anakaa na kuidhinisha kila gari ya halmashauri inayonunuliwa?
 
Mtoto wa Magufuli. Alisaidia ushindi wa CCM kule kwa Chiza. Baada ya kumtangaza Chiza akahamishwa usiku huo huo. Kuletwa Temeke. Kama akiweza sema hawezi kuongea na mwandishi wa habari, atashindwaje kuwa na mahabusu ofisini kwake. Tanzania ya Magufuli ina furahisha. Kila mmoja ni boss kwa nafasi yake..
Kumbe ndo yeye aliyemtoleaa nje mwandishi wa the super brand
 
Back
Top Bottom