Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa. Makala ya leo ni kuhusu fursa ya kuufanya uchaguzi Mkuu ujao wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa utakuwa ni uchaguzi huru na wa haki.
Kwanza tukubaliane katika uendeshaji wa nchi, katiba, sheria, taratibu na kanuni ndio kila kitu.
Tangu tumepata uhuru wetu, nchi yetu Tanzania haijawahi kubahatika kupata rais ambaye ni mwanasheria, hivyo marais wetu wote wanawategemea wanasheria kwenye utengenezaji wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, hivyo kukitokea madudu ya ajabu ya kisheria kama ubatili kwenye katiba yetu, rais ambaye sio mwanasheria, hawezi kujua kwasababu anawategemea washauri wake ambao ni wanasheria.
Mtu ambaye sii mwanasheria, hawezi kuujua ubatili wa sheria, atawategemea washauri wake wamwambie kuhusu issues zozote za kikatiba na kisheria, ikitokea hao washauri nao japo ni wanasheria lakini hawajui sheria kikamilifu, ndio wanampotosha rais wetu, ndio maana bandiko hili ni utetezi kwa rais wa JMT Asilaumiwe kwa yanayotokea kwenye issues zote za katiba na sheria kwasababu yeye sio mwanasheria.
Japo kuna huu msemo wa Kiswahili usemao "Mkubwa ni jalala" na "aliyekutwa na ngozi ndiye aliyekula nyama" maadam rais ndio kipo chetu na macho yetu yote tumeyaelekeza kwake, lakini kuna mengine tutakuwa tunamuonea bure!, ndio maana niliwahi kushauri
Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda
Mfano mzuri na mfano hai ni katiba ya Tanzania ya 1977, imenajisiwa kwa kuchomekewa kifungu fulani batili, waliokichomekea kifungu hicho ni Bunge la JMT, aliyeubaini ubatili huo ni Mahakama Kuu ya Tanzania, aliyeulinda ubatili huo ni Mahakama ya Rufani ya JMT, hivyo mpaka hapa ninapozungumza, usikute Rais wa JMT, she is an innocent victim, hajui kuwa katiba ya JMT imenajisiwa kwa ubatili fulani kwasababu wanasheria washauri wake rasmi ni ama hawaujui ubatili huo ama wanaojua lakini hawamwambii ukweli rais wetu, hivyo ikitokea tukaenda kwenye uchaguzi Mkuu wa 2025 bila kuuondoa ubatili huu, mtu wa kulaumiwa sio Rais Samia, kwasababu yeye sio mwanasheria, and after all, tumekuwa tukiendesha chaguzi zetu zote kwa ubatili huu, hivyo taifa letu kujikuta linalaanika kwa adhabu za karma bila kujijua!.
Kwenye ubatili huu ninao uzungumzia hapa, kiukweli kabisa mhimili wa Serikali, Bunge na Mahakama, umetukosea sana Watanzania!.
Katika mihimili hiyo mitatu, ni mhimili wa serikali tuu ndio pekee unapowakosea Watanzania, unaweza kuushitaki mahakamani lakini mhimili wa Bunge na mhimili wa Mahakama, unapowakosea Watanzania, hakuna mahali popote pa kuwashitaki zaidi ya kutegemea huruma ya rais wa JMT pekee.
Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?
Kama hao wanasheria manguli wabobezi na wabobevu wa sheria ambao rais wa JMT anawategemea wamshauri, ndio hao hao waliotunga sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba, na wakaipeleka Bungeni kutungwa kuwa sheria, sasa kunapotokea madudu ya ajabu ya marekebisho ya sheria kama haya yaliyoletwa jana Bungeni, unategemea nini?. Kumlaumu Rais Samia ambaye sii mwanasheria, ni kumuonea bure!.
Tukubali tukatae, Tanzania tuna tatizo kubwa la wanasheria wa ajabu!. Sakata la IGA ya DPW na Bandari ndio limetufungua macho!. Kwa mujibu wa katiba yetu Ile IGA ya DPW na Bandari zetu ni batili!, lakini IGA hiyo, pamoja na ubatili wake wote, bado ilipitishwa na Bunge letu Tukufu hivyo hivyo ilivyo without any reservations!,
Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! tukauliza
"IGA ya DPW imetusaidia sana kujitambua. Tuna wanasheria wa Aina Gani!, Bunge na Serikali yetu, Ilipitishaje IGA Hii? mwisho wa siku hii IGA, iliwekwa pembeni HGA safi ikasainiwa. Sasa unapowategemea wanasheria wa type hii ndio washauri wa sheria na wasaidizi wa Rais Samia, unategemea nini?!. Tusimlaumu kabisa Rais Samia.
Unaweza kufuatilia baadhi ya madudu ya ajabu ya kisheria yaliyofanywa na wanasheria wetu!
Mpaka leo ninapoandika hapa, ubatili huo bado uko ndani ya katiba yetu!. Kwa vile Rais wa JMT sio mwanasheria, tulichofanya akina sisi, ni kumweleza Rais Samia kuwa baadhi ya wanasheria anaowategemea hawamsaidii, hivyo akina sisi tukajitolea kuwa bypass and reach out kumfikia Samia mwenyewe na kumweleza kupitia mitandao ya kijamii na makala magazetini kuwa katiba yetu ni batili!.
Kuhusu huu ubatili kwenye katiba yetu, kama ni kumweleza Rais Samia, tumemweleza sana!.
Kikosi kazi kilipomaliza kazi tumampongeza tukamkumbusha.
Pongezi Rais Samia, Serikali, Kukubali Kubadili Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi!. Tuanze na Katiba Kwanza Ndipo Sheria Au?.
Wakati hayo yote yakiendelea, watu tukajitolea kufanya uelimishaji umma kuhusu katiba kupitia vipindi vya TV, Redio, makala magazetini na kwenye mitandao ya kijamii.
View: https://youtu.be/Ku8I626xl_k?si=obas7_hk4kMwpfcY
Nikazungumza na wanasisa mbalimbali wana mategemeo gani kuhusu hali ya siasa, nikatengeneza Vox Populi, kwenye Vox Populi, ukikusanya sauti za wengi, ukaziweka sauti hizo pamoja, sauti hizo haziwi tena ni Vox Populi, zinageuka ni Vox Dei!.
Baada ya Serikali yetu sikivu kukubali italeta mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na mabadiliko ya tume ya uchaguzi, tukashauri tena na tena!.
Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?
Hatimaye jana Ijumaa, hiki ndio tukaletewa!. Sisi wa kupongeza tukapongeza
Lile fupa lililowashinda marais wanaume 4, rais mwanamke 1 aligegeda kama mlenda!. Miswada 3 ya ukombozi mpya wa taifa letu yatua bungeni asubuhi hii
Kuna watu watamlaumu Rais Samia kwa kuamini ni yeye!, kumbe masikini ya Mungu, sio Rais Samia, yeye sio mwanasheria, hiki kilicholetwa Bungeni jana yaani ile Miswada ni kazi ya washauri wake ambao ni wanasheria.
Tujifunze kuwa na Shukrani kwa Madogo ili Tupatiwe Makubwa!. Japo Tulitaka Kikubwa, Tumepewa Kiduchu!, Tukipokee Tushukuru, au Tususe Kudai Kikubwa?.
Sasa kwa vile tunayo miezi 3, ya kujadili na kutoa mapendekezo yetu, nashauri na kuwasisitiza tusimlaumu Rais Samia, wala tusiwalaumu wasaidizi wake, bali tutoe mapendekezo yetu kama tulivyofanya kwenye ile IGA, tukapata HGA nzuri.
Tupendekeze sheria nzuri ya uchaguzi na Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi, naamini kabisa Rais Samia ni Rais msikivu na tutasikilizwa na mwisho wa siku tutabadili kwanza katiba kuondoa ubatili, kisha tutaunda Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, Tutabadili sheria yetu ya uchaguzi kuleta sheria mzuri ya haki ya uchaguzi ambayo itasawazisha uwanja wa siasa, a level playing field, tutafanya uchaguzi wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa, hivyo utafanyika kwa siku moja na utasimamiwa na Tume moja Huru ya Uchaguzi na uchaguzi Mkuu wa 2025 utakuwa ni uchaguzi huru na wa haki!.
Mungu Ibariki Tanzania
Paskali