Maduka ya Dawa za binadamu yanapogeuka kuwa zahanati kwa kuendesha matibabu

Maduka ya Dawa za binadamu yanapogeuka kuwa zahanati kwa kuendesha matibabu

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Kutokana na mfumo wa maisha ya sasa, ikiwemo hali ngumu ya maisha watu wameamua kuvunja sheria ili kujiingizia kipato kwa namna yoyote ile iwayo.

Maduka haya yamegeuka kuwa zahanati kwa kuendesha shughuli za. Matibabu tofauti na leseni waliyopewa

Mengi sana yamejificha nje ya maduka haya dawa za binadamu yaliyopo mjini na vijijini na baadhi ya watu wanalijiua hili.

Utoaji mimba, baadhi ya maduka ya dawa yamekuwa yakiendesha shughuli hii kwa kificho na baadhi ya wateja wao ni wanafunzi, na wakati mwingine hufanywa na wasiokuwa wataalam na hivyo chanzo za vifo kwa wahanga.

Wasiokuwa na elimu ya ufamasia kuuza duka la dawa, unakuta mtu katoka form four au kaishia form two, anaelekezwa kwa muda wa wiki moja na mwenye duka tayari anaanza kuuza dawa pamoja na kuchoma wagonjwa sindano na kusafisha vodonda wafikapo dukani kwake..

Matibabu kwa wagonjwa, kuna baadhi ya wagonjwa pindi waendapo duka la dawa kueleza dalili za maumivu ya Mwili wanayoyasikia basi muhudumu wa duka humpa dozi ya dawa kwa kukisia aina ya ugonjwa bila vipimo badala ya kumshauri aende hospitali.

Huduma za kujifungua, baadhi ya maduka yaliyopo vijijini hutoa huduma hii kwa wakina mama wajawazito wanaojifungua, na hata baadhi ya maduka ya mjini nayo pia yanafanya huduma hii kitu ambacho ni hatari kwa afya ya binadamu.

Hii ni hatari kwa afya ya binadamu na sio la kufumbia macho, maduka ya dawa kufanya kazi zinazotakiwa kufanywa na Hospital.
 
Wewe unaishi nchi ipi? Kijijini tunakua na nesi moja wa cheti anafanya kazi zote, ndo mfamasia, dakitali bingwa nda anae zalisha, nda anae kuelekeza dawa, na maisha ya naenda tena sio kila siku upo . Kumkuta ni bahati kwa wiki anakuepo siku tatu tu, hi nchi bado sanaaaa
 
Hao watu ukilinganisha idadi ya vifo wanavyo sababisha na vifo wanavyo okoa hakika usinge andika haya na kuwaangashia zigo la lawama.
Utafikiri hajawahi kuharisha akakimbilia dawa kwa hawa hawa anaowaponda. Tatizo letu watanzania tukiharibikiwa tunataka na wengine waharibikiwe.

Ni Mara chache sana unasikia muuza duka LA dawa amembaka mgonjwa au kumuua mgonjwa. Hayo maozo yote tumeyasikia yakifanywa na madaktari tena walioajiriwa.
 
Utafikiri hajawahi kuharisha akakimbilia dawa kwa hawa hawa anaowaponda. Tatizo letu watanzania tukiharibikiwa tunataka na wengine waharibikiwe.

Ni Mara chache sana unasikia muuza duka LA dawa amembaka mgonjwa au kumuua mgonjwa. Hayo maozo yote tumeyasikia yakifanywa na madaktari tena walioajiriwa.
Wengi wanaofanya hizo huduma hawana taaluma yoyote
 
Haya ndiyo maisha katika nchi nyingi za Africa. Hospitali zenye huduma nzuri ni za Private, kutokana na hali ya uchumi unaona ni kheri uruke gharama za kumuona daktari uwende pharmacy upate dawa.
 
Wewe unaishi nchi ipi? Kijijini tunakua na nesi moja wa cheti anafanya kazi zote, ndo mfamasia, dakitali bingwa nda anae zalisha, nda anae kuelekeza dawa, na maisha ya naenda tena sio kila siku upo . Kumkuta ni bahati kwa wiki anakuepo siku tatu tu, hi nchi bado sanaaaa
Huyu nesi ana heshima kubwa sana kijijini, wengi hata chakula wananunua wanachopenda tu. wanakijiji wakivuna mpunga na mahindi anapewa na bado kuna wanaopeleka ndizi na matunda.
 
Utafikiri hajawahi kuharisha akakimbilia dawa kwa hawa hawa anaowaponda. Tatizo letu watanzania tukiharibikiwa tunataka na wengine waharibikiwe.

Ni Mara chache sana unasikia muuza duka LA dawa amembaka mgonjwa au kumuua mgonjwa. Hayo maozo yote tumeyasikia yakifanywa na madaktari tena walioajiriwa.
Hawezi kuelewa
 
Kaa kwa kutulia,, subiri yakukute... Nchi ya mikopo unategemea huduma zitakuwa bora kila mahali...

Kuna siku utaelewa bila kueleweshwa..
 
Mpaka dawa za uzazi mfano sindano siku izi wanachoma serikali iliangalie hili mwingine kasomea sheria anauza duka la dawa
 
Kaa kwa kutulia mkuu..huko mahosptalini kwenyewe kumejaa ufala unaoendeshwa na mafala waliovaa manguo meupe....wananchi wanatafuta sehemu yenye uafadhari wa kimatibabu ya haraka na bei nafuu.....
 
Back
Top Bottom