Maelezo ya Wenje yamenyooka zaidi kuliko tuhuma za Lissu! Huenda Mbowe bado ni mtu sahihi zaidi kuongoza CHADEMA

Hakuna ushahidi wowote wa kuonyesha Mbowe kahongwa chochote kutoka CCM, unaweza kuwa hukubaliani na Mbowe anavyoongoza CHADEMA lakini sio sawa kumzushia hayo mambo kwa sababu tu hamkubaliani naye.
 
Sijui umewezaje kupima hadi ukafanikiwa kupata maelezo ya Wenje yaliyonyooka.

Wenje alitumia karibu masaa mawili kuelezea tuhuma iliyotolewa kwa dakika moja.
Nilitaraji ungetamani Lissu ahojiwe ili uweze kupima maelezo yao, lakini imekuwa kinyume chake.
Binafsi maelezo ya Wenje yamezidi kuibua maswali kichwani mwangu, natamani Lissu apatiwe platform kama ile ili abananishwe, baada ya maelezo yake ndiyo naweza nikapima.
Binafsi sikuwahi hata kui buyu ile tuhuma ya Abdul sababu hata namna ilivyoongelewa ni kama imewekwa kwenye mabano, ingawa kuna vitu aliwahi kufungua.

Ila wenzetu mna vipaji vya kupima na mmeshapata majibu...Hongera sana mkuu.
 

Wenje anataka Abdul asaidie nini kwenye kukwamua mambo nchini?
 
Sijaona contradictions katika maelezo aliyotoa Wenje lakini pia ameuliza maswali ya msingi sana ambayo ukiyatafakiri kwa fikra huru unaona anachokisema Lissu kuhusu watu ndani ya chama chake kuhongwa pesa za Abdul hakuna mashiko sana.
 
Umeshindwa hata kuandika muhtasari wa maelezo yake, japo kwa sentensi moja au mbili? Uandishi wako mbona wa mhemko sana?

Tutajadilije hapo sasa?
Maelezo aliyoyasikiliza yeye huko alikosikiliza ambako hatujui ni wapi na lini, na alisikiliza nini anataka tushirikiane nae katika kuyajadili.
 
Wenje anataka Abdul asaidie nini kwenye kukwamua mambo nchini?
Abdul yuko katika nafasi nzuri ya kukwamua mambo ya washikaji, marafiki na ndugu zake pamoja na watu wengine wachache wanaoweza kukatana kama ilivyotokea kwa Wenje ila hayuko katika nafasi nzuri ya kukwamua mambo ya kinchi.
 
Hizi kampeni sidhani kama zitasaidia. Kwa sasa upepo upo kwa Lissu. Machaguo yapo mawili tu, Mbowe agombee tena na apate uenyekiti Chadema ife au Lissu agombee na apate uenyekikiti Chadema iendelee kuwa imara.
 
Tatizo letu ni kuwa tunapenda "conspiracy theories na majibu mepesi mepesi". Mbona maelezo haya yamekaa vizuri kuliko ya Lissu?

Ingawa nahisi Mbowe atatangaza kutogombea lakini anaweza kuamua kugombea baada ya mchezo aliochezewa. Akifanya hivyo atawalazimisha wajumbe wa Kamati Kuu wachague upande. Akishinda, atakijenga upya chama chake kama alivyofanya mara kibao. Akishindwa, atatoa ushirikiano kwa uongozi mpya ili chama kiendelee ku survive.

Nadhani ni muhimu agombee kwa afya ya chama, asionekane amemuogopa Lissu na ampe Lissu uchaguzi huru na ushindani anaosema anataka.

Amandla...
 
Abdul yuko katika nafasi nzuri ya kukwamua mambo ya washikaji, marafiki na ndugu zake pamoja na watu wengine wachache wanaoweza kukatana kama ilivyotokea kwa Wenje ila hayuko katika nafasi nzuri ya kukwamua mambo ya kinchi.

Basi Lissu hahitaji ujanjaujanja ktk mambo ya nchi. Hakuna kitu ambacho Abduli angejua kwa Lissu ambacho mama yake hajui. Lissu alikutana na mama yake Brussels, Lissu akamueleza kila kitu. Pili Mama yake akitaka faili la Lissu ni suala la kuiagiza Idara ya Usalama impe taarifa. Lissu hahitaji "connection" ya mtoto wa rais ili rais atimize wajibu wake kwenye haki zake
 
Nikukumbushe tu mleta mada, Pesa za Abduli za kujaribu kununua watu hazikuanzia kwa Lissu zilianzia kwenye uchaguzi wa chama kwenye kanda ya Nyasa
 
Abdul yuko katika nafasi nzuri ya kukwamua mambo ya washikaji, marafiki na ndugu zake pamoja na watu wengine wachache wanaoweza kukatana kama ilivyotokea kwa Wenje ila hayuko katika nafasi nzuri ya kukwamua mambo ya kinchi.
Hivi kuna mtu yuko karibu na Rais kuliko mtoto wake? Na mwenye access nae kuliko mwanae? Na atakayemuamini kuliko mwanae? Katika nchi ambayo Rais ndio Alpha na Omega, hii inampa nguvu kupita kiasi. Kama vile waziri wa Tamisemi alivyo na nguvu.

Amandla...
 
Unajidanganya. Lissu alihitaji mtu anaeweza kumsukuma Rais ili atimize ahadi yake. Mwanae ana nafasi pekee katika hilo. Kama ilivyokuwa kwa mama Siti. Kama ilivyokuwa kwa Ridhwani n.k. Lissu hakuwa na namna ya kumlazimisha atimize huo unaoita wajibu wake.

Ni kama vile suala la COVID-19. Hamna mtu anaeweza kumlazimisha awanyang'anye ubunge. Si Spika, si Jaji Mkuu. Ni mpaka mwenyewe aamue. Na hamna la kumfanya maana Katiba inampa hayo mamlaka.

Amandla...
 
Wakati wa utawala wa kwanza wa Trump, mkwe wake alikuwa na nguvu kuliko mtu yeyote serikalini. Sasa hivi Elon Musk ana nguvu kuliko Vance. Proximity matters. Watu wanaosema Abdul hana nguvu yeyote wanakuwa disingenious.

Amandla...
 

Sasa mpaka hivi sasa Samia hajasikia hili saga la mwanae na Lissu?. Keshampa Lissu haki yake?
 
Sasa mpaka hivi sasa Samia hajasikia hili saga la mwanae na Lissu?. Keshampa Lissu haki yake?
Inaelekea Lissu hajalipwa bado. Kama ni hivyo mwanae hakufanikiwa. Sasa kuna jamaa anadai kuwa zililipwa ila kuna watu CDM walizipiga. Tutasikia mengi mwaka huu.

Amandla...
 
mbowe ni jiniazi nimecheka sana

kwa ujinga huu wa chadema mama aendelee tu
 
Whether Wenje yupo sahihi au la kiufupi Mbowe keshaoverstay hata kama ni kiongozi mzuri kiasi gani, ni muda wa kuexit, hamna kipya atakacholeta baada ya miaka 20, mbinu zake zote zishatumika na kufikisha hicho chama kilipofika aachie wengine, iwe Lissu au mwingine ni sawa tu! Watanzania wanataka changamoto mpya ili kurudisha imani kwa upinzani, vinginevyo tunaelekea CUF, NCCR na wengine waliobaki skeleton tu sasa hivi, wamebaki kuzikwa tu yaishe!
 
Yamenyooka Kwa wapuuzi kama wewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…