Jamani nahitaji yoyote mwenye gali ndogo kama ist, , Ractis na anaitaji aingize pesa kupitia UBER tuingie mkataba kwa wiki nimletee hesabu ya 200,000 kwa wiki tuandikishane gali iwe kwenye hali inzuri niweze kuingizia pesa
0654960981
 
Habari
Mimi ni mwanafunz kutokana na kushindwa
Kuendelea na chuo nimeona nijitafutie pesa kwa kuganga uku na kule sasa ni hivi
Jamani nahitaji yoyote mwenye gali ndogo kama ist, , Ractis na anaitaji aingize pesa kupitia UBER tuingie mkataba kwa wiki nimletee hesabu ya 200,000 kwa wiki tuandikishane gali iwe kwenye hali inzuri niweze kuingizia pesa0654960981
 
Tumempata rais shujaa! Naamini atatufikisha na atatuachia mrithi mzalendo miaka yake 10 ikifika.
 

Lakini umesahau kuainisha Tsh. Trillion 1.5(bilion 1500) zimetumikaje.
 
Mbona umeshindwa kuainisha matumizi ya zaidi ya Tshs. trilion 1.5 ( zaidi ya Tshs. bilion 1500). Tueleze zimetumikaje.
Milion 50 Tshs. Kwa kila kijiji zimefikia wapi ?
Huduma bora maslai zaidi. Motisha kwa wafanyakazi zipo wapi.
Vyeti feki na malipo yasiyostahili kufuatana na elimu mbona kaogopa kuwatumbua watu wake wa karibu ?
Maendeleo yanaletwa na watu, sio watu wanaletwa na maendeleo chato kuna vivutio gani mpaka kuwe na aiport kubwa, chato kuna population gani mpaka kuwe na trafick light,au hizo trafick light zitaongoza punda ?
Ukiniambia atakuletea kiongozi mzarendo kama msiba sawa utapata msiba.
 
Pato la ndani la taifa limeongezeka, matumizi yake na maendeleo yake yakowapi. Thamani ya shiringi inazidi kuporomoka yupo wapi mwokozi wake ? Je kaudhibiti namna gani mfumuko wa bei ?
au kwa mtoa maoni anapoitwa mchochezi ndio uzalendo halisi?
 
Ninamkubali sana huyu mh Rais ingawa hawezi kufanya kila kitu nilichokuwa natamani kwa mfano sipendi upendeleo awali tuliishi kwenye bwawa la upendeleo na kufanya watoto wa wenyewe kupata kila kitu hapa amepunguza zaidi ya asilimia 75,Kuiibia serikali kwa njia ya semina manunuzi hewa malipo hewa nk kwa sasa asilimia 90 wamedhibiti.Elimu walisoma watoto wao tu hapa mafanikio asilimia 95 tatizo limebakia kwenye elimu ya juu.
Pamoja mazuri mengi lkn mh.angejiweka mbali aache mamlaka zifanye kazi badala ya kuchukua majukumu kama yake binafsi akasimishe kwa mfano vyeti feki angeacha maamuzi yawe ya chombo kingine badala ya kujinadi kwamba yeye amewafukuza au anaposema serikali yangu nk.
 
Vipi kuhusu shs. Tilion 1.5, huu ni wizi ulio vunja record ya zaidi ya millenium mbili.
Unasema kakomesha upendeleo, vp kuhusu bomoa bomoa ya Dar iwe halali kwasababu hawakumpigia kura halafu mwanza walimpa kura nyingi wasiwabomolewe ?
je vp kuhusu wasifu wa paul makonda ninamaana vyeti vyake, je kwanini alitimua wengine na bashite kaachwa ? Tena namnukuu ' swala la vyeti kwa mtu anayechapa kazi halinihusu, wewe unafanya kazi nzuri, wewe chapa kazi' alisema raisi akimwambia makonda na uma wa watanzania.
Vp kuhusu trafiki light mahali ambako hakuna hata foreni za za magali labda za kuvusha punda na ng'ombe? Je chato ina hadhi gani au fursa gani za kibiashara au maendeleo hadi ikawa na airport kubwa kiasi hicho ?
Unazungumzia swala la elimu je tangu aingie madarakani ni mtoto yupi wa kiongozi ambaye yupo shule ya kata ?
Je unalifahamu swala la Jesca magufuli aliyepata dv 0 form 4 lakini akawa anasoma chuo kikuu cha uma tena kwa kodi za wananchi, na akipata mkopo wa 100% tena kwa course ambayo masomo yake alifeli, huku watoto wa maskini waliofaulu vizuri, wakilia kwa kukosa mkopo hata kuahirisha masomo yao ?
Je niambie serikali ilichukua hatua gani juu shambulio la Tundu lisu ? Wapo wapi waliomshambulia lisu ? Yupo wapi Ben saanane ? Yupo wapi yule azoli gwanda mwandishi habari wa kibiti?
Wanafunzi wanauwawa tena pasipo kosa mfano mwanafunzi wa chuo cha mwalim nyerere ? Nipe tamko la serikali juu ya hilo? Nipe tamko na hatua iliyochukuliwa juu ya kifo cha Aquilina ?
Vp juu ya wakosoaji wa sera au mwenendo wa nchi wanavyoanza kuhojiwa na uhamiaji ?
Vp kuhusu swala la democrasia na utoaji wa maoni, kwanini azuie mikutano ya hadhara ya kidemocrasia ? Vp kuhusu kuonyeshwa mubashara bunge ?
Niambie kosa halisi la manji ? Na kama alikuwa na hatia niambie kwanini yupo huru ?
Hebu niambie kitu gani mzungu akupe bure pasipo manufaa yake ?
Mzungu hawezi kukuachia bombadier bure pasipo sababu, hilo ni changa kwa watanzania.

Kwanini hataki kufanya ziara kwenye nchi zilizoendelea na kukomaa kidemokrasia akajifunze? Anatembelea rwanda atajifunza nini toka kwa kagame ?
 
Sasa anahaha anataka kufungia watsapp na google, je hii ni sehemu ya maendeleo?
Jamaa anataka kuua maebdeleo ya teknolojia.
 
Duuuu!kweli kila baya atatupiwa sijui mlitaka afanyeje ili akipata ushauri wenu aufanyie kazi maana uongozi ni lawama hata ungekuwa wewe kuna mambo ungelaumiwa tu siamini kama anafanya hivi kwa makusudi bali anakuwa na lengo zuri ambalo wasiompenda huvuruga kwa mfano uhasama na vyama vya siasa ulianza siku alipo apishwa walisusa na kutangaza vita aliwafuata bungeni waka msusa wakaanza kumuita majina ya kuudhi huku akipanga kwenda uelekeo fulani wanamvuta shati what do you expect.
Ili tutoke hapa tupate muafaka wa kitaifa mapambano siyo mazuri na serikali ipunguze maadui kwa kusimisha majukumu kwa taasisi maalumu zilizopo mfano vyeti feki siyo kazi ya rais,bandari nk.Maamuzi yawe ni ya taasisi siyo mtu mmoja.
Vyama vya upinzani vijitoe kwenye harakati maana hazina mwisho mfano tulipofanya harakati za uhuru tuliwatukana sana wakoloni lakini leo tunawapigia magoti.
Suala la CAG watu wengi hatuwezi kuelewa malumbao kikubwa wamjibu CAG mwenyewe yeye ndiye mwenye kutujulisha kama wapo sahihi kwa majibu yao au la.
 
Cha muhimu katiba ifuatwe
 
Anaandika Sheikh, Dr Yahya Msangi(PHD).
LOME, TOGO.
SANAA YA MAANDAMANO NA SIKUKUU: NYUMA YA PAZIA KUNA WAKUBWA

Ni vyema wenzangu mkaelewa yanayojiri nchi nyingine ili mtafakari kwa makini.

Kumekuwa na harakati za kuandaa maandamano nchi mbalimbali Afrika toka kipite kimbunga cha ARAB SPRING. Kipunga kiklichoanzia Tunisia kikasambaa kwa kasi Misri. Lakini wengi hamjui mlengwa haswa wa kile kimbunga cha facebook na tweeter alikuwa nani. Hakuwa Tunisia wala hakuwa Misri!

Baada ya kumuua Sadam wababe wa kimagharibi walilenga mitutu na makombora yao kwa Algeria, Libya na Syria. Wengi mnajua kuhusu kilichofanywa Libya na sasa Syria. Lakini wengi hamjui kuhusu Algeria.

Algeria ni nchi ya 10 kwa ukubwa duniani (geographically). Nchi kubwa kama hiyo haikosi kuwa na mali asili zinazowatoa mate mafisi makubwa! Lakini pia Algeria imepakana na kina Morocco, Mali, Tunisia, Libya, Niger, Mauritania na Sahara ya Magharibi. Kutokana na hili Algeria inapakazwa kuwa ni mfadhili mkubwa wa vikundi vya kigaidi! Hakuna ushahidi wowote ila hila hii inafanywa ili kupata sababu ya kuivamia na kuivuruga Algeria.

Mfaransa bado hajamsamehe Algeria kwa kiichowakuta enzi ya vita ya ukombozi! Mfaransa bado anayataka mafuta ya Algeria. Mfaransa anaona Algeria ndio inaofadhili wa TOURAG wanaompiga vita kutokana na wizi wa Uranium kaskazini mwa Chad na Mali! Wapiganaji wa kitourag walikuwa wakihifadhiwa na Gadaffi. Watourag wanatetea mali zao na nchi yao iliyotwaliwa kwa mabavu na kampuni ya kifaransa inayochimba uranium! Kuna taarifa zisizo na shaka kuwa umeme woote unaowaka ufaransa unatokana na Uranium inayoibwa Chad na Mali. Mazingira, wanyama na watu wamelemaa kwa athari za uranium mfaransa hajali! Wakubwa wamefumba macho! Mijizi combined! Baada ya Libya kuvamiwa sasa ni Algeria inatafutwa! Ukumbuke Algeria ina utajiri mkubwa wa mafuta! Algiers na Cairo ndio miji pekee Africa in aundergroung transport system ya hadhi ya kimataifa!

Arab spring ililenga Algeria ikaja bahati mbaya akabondwa Tunisia na kipenzi chao Misri! Ndio maana pamoja na arab spring kupamba moto Misri na Tunisia zimekufa kifo cha mende! Waliokuwa nyuma ya Arab Spring walipoona mlengwa kakwepa wakatuliza ngoma! Vijana wa facebook na tweeter wakaumia buree!

Sasa kuna nchi 2 maandamano yanatumika kutaka kuzivuruga. Ni Tanzania na Togo. Kila moja na sababu zake tofauti.

Tuanze na Togo.
Togo ni kanchi kadogo kabisa barani Afrika. Nadhani ni Sao Tome na Principe pekee ndio ndogo kuliko Togo. Wakazi wa Togo ni kama milioni 8 hivi na mji mkuu wa Lome una wakazi takriban milioni moja. Ni mji ambao kwa tuliozoea Dar hauna mikikimikiki kabisa. Togo haina madini isipokuwa ina bandari maarufu toka enzi za ukoloni. Ikitumika kama bandari maalum kwa makoloni ya Ufaransa. Kwa kipindi cha kuanzia mwaka jana Togo imekabiliwa na maandamano mawili au matatu kila wiki! Mjumuiko wa vyama vya upinzani hapa (unaweza kuwaita UKAWA TOGO BRANCH) vimekuwa vikiandaa maandamano haya. Yamesababisha watu kufa na mali kuharibiwa kila yanapoitishwa. Ilishangaza watu ni wapi watu hawa ambao vyama vyao ni dhaifu mno walipotoa fedha za kuendesha maandamano kila wiki? Pia ikashangaza wengi ni kwa nini maandamano haya yamechukua sura ya udini? Baadhi ya mashehe na misikiti imetumika sana. Inashangaza kwa kuwa asilimia 54 ya watogo wanaamini vodoo!

Lakini wengine tunajua chanzo!

Mwaka jana Netanyahu alijitahidi kupitapita nchi mbalimbali za kiafrika na hata kuhudhuria kikao cha wakuu wa nchi za Afrika mjini Addis na kuhudhuria sherehe za kumuapisha Uhuru mjini Nairobi japo hakwenda kiwanjani! Netanyahu huyo huyo aliitisha kikao cha wakuu wa nchi za kiafrika wakati wa kikao cha UN General Assembly mjini New York kikao ambacho Kagame aligoma kuhudhuria! Agenda kuu ya Netanyahu ilikuwa kuomba nchi mojawapo ikubali kuandaa IZRAEL AFRICAN SUMMIT ili tu aonyeshe Izrael inakubalika Afrika na ili kuwadhibiti Wapalestina baada ya Taifa lao kutambulika. Izrael inamezea mate kiti Baraza la Usalama na inadhani Afrika itaunga mkono siku wakiwasilisha ombi. Katika harakati zake hizi alifanikiwa kuishawishi Togo iandae hiyo Summit.

Kabla hata Togo haijaanza maandalizi maandamano yakaanza! Nia ni kuizuia isiandae hiyo Summit na wahusika wanaungwa mkono na mataifa yoote ya kiarabu na baadhi ya mataifa mema ya Ulaya. Wanapinga Afrika kumpa Netanyahu karata ya kuendelea kuikandamiza Palestine na watu wake!

Kweli summit imeshindikana kuandaliwa kutokana na hizi vurugu lakini pia kutokana na mataifa mengi ya Afrika kuiambia Togo utahudhuria wewe na Netanyahu hiyo Summit! Hii ndio hali tete iliyopo Togo hivi sasa. Kuna maandamano ambayo nguvu inatoka nje! kelele za uchaguzi, tume huru, uvunjifu wa haki ni geresha tupu!

Turudi Tanzania
Toka JPM adhibiti uporaji wa kimataifa kwa kiwango cha kutishia maslahi ya nje pameibuka watu ambao kutwa kucha wanawaza maandamano! Huhitaji akili ya ziada kujua ni wao au wanaowalipa! Kwa ilivyo Tanzania wamekwama ila msiwadharau kamwe! Tayari wameanza kuingiza udini kwenye harakati zao! Tumeanza kuona baadhi ya viongozi wa kiroho wakigeuka kuwa wanasiasa! Hawakemei mambo ya kiroho wanakemea mambo ya kisiasa! Utashangaa kiongozi wa kiroho hakemei watu kusoma misa ya wafu mbwa! Hawakemei kiongozi wa kiroho kutoka hadharani na kumtukana kiongozi mwenzao wa kiroho eti ni mjinga na kala maharage! Wao kwao haya ni sawa! tatizo kwao ni katiba ya nchi!

Hapa Togo maandamano yamefikia ukomo! Serikali iliwakusanya viongozi woote wa UKAWA na kuwafungia ndani toka alfajiri hadi usiku wa manane wiki mbili zilizopita baada ya wao kutangaza maandamano tena! Wiki imepita sasa bila maandamano! Waandamanaji waliokuwa wakilipwa wamerejea makwao!

Najua Tanzania leo haikuwezekana ila serikali isidhani yameisha! Kuna watu na mataifa yanatamani amani itoweke wapenye kama walivypenya DRC, Libya, Syria, Iraq, Afghanistan, Somalia, Sudan na kwingineko! Tanzania ni nchi yenye utajiri mkubwa sana uliokuwa ukinufaisha wengi! Sasa unanufaisha Tanzania imekuwa nongwa.

Serikali itafute dawa ya kukomesha maandamano! Haiwezekani maandamano yakafanywa ni mchezo wa kitoto! Maandamano yanayoshinikizwa na watu wa nje ni uhaini! Wahusika watendewe kama wahaini!

Najua makala ni ndefu lakini soma!
 
Inasikitisha sana na kwa kweli kwa hali hii "YAJAYO HAYAFURAHISHI"
 
Jiwe litampata mtu gizani ngoja mtoa mada na jeshi lake waje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…