MAGARI YA UMEME: Fahamu Faida Zake, Aina na Namna Yanavyofanya Kazi

Hahah vile vi tesla vinatembea kishenzi mzee baba,ziko zinazoenda mpk 0-60 kwa 2.3sec ,yaani kuliko hata supercars.

Ila hazina mzuka ule wa Petrol car,ogopa sana gari inakimbia kichizi afu haina muungurumo wa kibabe hata hainogi aisee.
Si wanaweka simulator tu mzee. Unaswitch mlio tu ukitaka hata wa lamborghini upo tu wa benz v12 nao ni mzuka tu.
 
Wadau kwani inashindikana kutengenezwa gari ya umeme lkn ikawa na mfumo wa kupiga kelele kama alteza yenye muffle kubwa?,wengine maisha yetu yatakuwa magumu na kukosa raha ya kuishi sasa mambo ya kutembea kimyakimya kama nyoka.
 
Wadau kwani inashindikana kutengenezwa gari ya umeme lkn ikawa na mfumo wa kupiga kelele kama alteza yenye muffle kubwa?,wengine maisha yetu yatakuwa magumu na kukosa raha ya kuishi sasa mambo ya kutembea kimyakimya kama nyoka.
Inawezekana mkuu, inafungwa sound adapter tu. Inaplay kupitia speakers ambazo ziko attached ndani ya gari na sehem flan kwa nje kwa ajili ya kuliza huo mlio.
 
Inawezekana mkuu, inafungwa sound adapter tu. Inaplay kupitia speakers ambazo ziko attached ndani ya gari na sehem flan kwa nje kwa ajili ya kuliza huo mlio.
kama ni hivyo tutaenda sawa maana ilikuwa sehemu ya msiba maishani.
 
Masa
hihisho kwenye slow charging hapo. Ni kuanzia masaa 5 na kuendelea, 8 mpaka kumi. Rejelea charging systems za tesla, nisaan leaf, Y peng za china ambazo ubora wake bado ni mzuri tu.
 
Nasikitika huu uzi umekuwa dormant, nikajua utakuwa hot hasa ukizingatia umeme ndio mapinduzi ya ki tenkolojia yalikofika
 
Haya magari watu itabidi wawe wanatembea na spare battery, just in case inatokea battery ikapata hitilafu na ku-discharge uko njiani ambako hakuna kituo cha kuchaji battery, au kukawa na hitilafu kwenye charging sytem ya gari, battery ika-drain. Ikitokea hivi uko njiani katikati porini lazima uchoke tu!
 
Hii ni vita ya Mzungu kumchinja Mwarabu kiuchumi... Mazingira visingizio tu. #iran #saudia #russia #china
 
hutaki kukaa kwa saa moja (dakika 60) kuchaji betri ya gari... Kwa madai ni upotevu wa your precious time.

Lakini at the same time unaweza kukaa saa moja (dakika 60) kupiga stori mitandaoni.. Je huo nao siyo upotevu wa your precious time?

Vipi simu yako nayo huwa unaichaji kwa muda gani? Vipi na hiyo siyo upotevu wa your precious time.


Uzuri ni kwamba, tukubali au tusikubali, lakini Electric Vehicles are here to stay.
Cha muhimu ni kukubaliana na hili na kujiandaa.

Kama binadamu wote wangetaka kuishi kwa mazoea kwa kile walichokizoea basi hata hii Internet, Electronic Devices au Umeme navyo visingekuwepo pia.

Anyway, wakati mwingine inabidi tuache kuishi kwa mazoea, na tujiandae na hizi electric vehicles.
 
Hata hizi electric vehicles kama ukitaka zitoe sauti kubwa hilo linawezekana sana tu mbona.

Na sauti zitakuwa ni halisi na wala siyo mimic sound, sababu ni ukweli kwamba motor ya gari za umeme nazo pia huzalisha sauti kama ambavyo motor zingine zozote vile zinavyozalisha sauti wakati zikizunguka.

Tukumbuke hata Mashine ya Kusaga Nafaka nayo ni motor ya umeme na huwa inazalisha sauti kubwa tu, ndiyo ni motor kama motor ya kwenye gari za umeme.

Rejea umeme ni nishati (energy), na nishati ya umeme inaweza kubalishwa kuwa sauti (sound energy).

Hata speakers za simu yako ndiyo kitu zinachofanya, zinabadilisha electric signal into sound waves, kisha sauti inasikika.

Vivyo hivyo kwa Combustion Engine za gari za petrol na diesel, ile sauti inakuja kutokana na Nishati ya Kikemikali iliyomo kwenye Mafuta kuunguzwa na kuzalisha nishati nyingine ikiwemo nishati ya sauti (sound energy) inayotoka katika injini.

Energy can neither be created nor destroyed, but it can be transformed from one form into another.


Namalizia kwa kuandika hivi, katika electric vehicle kinachofanyika ni kwamba kwenye gari kuna Motor ambayo hufanya kazi ya kubadilisha Nishati ya Umeme (Electrical Energy) ili iwe Nishati ya Kimakenika (Mechanical Energy).

Injini za Petrol au Diesel hizi hubadilisha Chemical Energy ya Petrol au Diesel ili iwe Mechanical Energy.

Mechanical Energy ndiyo inayozungusha gari, na kufanya gari lijongee.

Pia motor za electric vehicles inapozunguka huwa inazalisha sauti pia. Sema tu ile sauti ni ndogo sana.

Lakini ukitaka electric vehicles nazo zizalishe sauti kubwa, Kitaalamu hiyo inawezekana kabisa.

Ni kama Motor na mfumo mzima wa Machine ya Kusaga Nafaka zinavyotoa sauti.. Ndiyo motor ya machine ya kusaga Nafaka inafanya kazi kama vile Motor ya Gari za Umeme tu.

Motor zote hubadilisha umeme (electrical power) ili kuwa Mechanical Energy, ambapo mechanical energy ndiyo huzungusha kitu na kufanya kijongee.

Hata Mwili wa Binadamu nao hubadilisha Chemical Energy iliyopo katika Chakula na kuwa Mechanical Energy inayotuwezesha kujongea (kutambaa, kuogelea, kuruka, kukimbia, kutembea etc.)
 
Magari yanatengenezwa kwa teknolojia kubwa sana, battery zake ziko standard, mara chache sana hilo kutokea ungesema changamoto ya gharama hapo sawa.... Gari za umeme ni GHARI MNO
 
Magari yanatengenezwa kwa teknolojia kubwa sana, battery zake ziko standard, mara chache sana hilo kutokea ungesema changamoto ya gharama hapo sawa.... Gari za umeme ni GHARI MNO
Gharama inatoka wapi tena? Ni kitu gani kinasababisha kuwa ghali, umeme?
 
Gharama inatoka wapi tena? Ni kitu gani kinasababisha kuwa ghali, umeme?
Yes kwetu lazima iwe ghali sababu magari mengi ni brand new.... Tz ukinunua gari brand new unasomeka una hela sana hata kodi utakayo pangiwa utashangaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…