Magazeti ya Mabeberu yameanza chokochoko El País wamuita John Magufuli, the African Bolsonaro. Nini kipo nyuma ya tuhuma hizi ?

Magazeti ya Mabeberu yameanza chokochoko El País wamuita John Magufuli, the African Bolsonaro. Nini kipo nyuma ya tuhuma hizi ?

Sidhani kama anashida ya kusifiwa na Mabeberu lakini Rais ni alama ya taifa, shutma yoyote inaakisi taifa letu, leo hii hizi chokochoko wanazoanzisha zinafanya Tanzania isionekane salama ama kuwa na visa vingi vya ugonjwa huu wa corona. Kuna mahali wanajaribu kututingisha na kuna sababu, ukisikiliza kauli za Rais kuna kitu zaidi nyuma ya pazia lakini kwa sasa hataki kukisema. Muda utatupa majibu sahihi.
Shida yetu sio sifa bali afya njema na wakishathibitisha kupona kwetu licha ya dua la kuku, basi na watakuja.

Cholochoko nyingi mnazianzisha hapa na kuzituma huko, kisha mna paste na kuturudishia tena sh*ine nyinyi na team kigogo aka zitto kabwe na genge lake.
Tynawaelewa na njaa zenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni Sweden mkuu
Leo nilikuwa nasikiliza KBC asubuhi nikasikia wanaitaja nchi moja kati ya zile za Scandinavia aidha Denmark au Norway siikumbuki inafuata hatua kama za Tanzania. Hawakuwa na lockdown wala nini, ila maisha yaliendelea. Sasa mnakuja na hoja kana kwamba Tanzania pekee ndio imefuata utaratibu huo. Acheni siasa maji taka tunataka nchi iwe na wanasiasa shupavu wenye hoja nzito zenye tija kwa jamii.
Sent from Geneva_ Switzerland

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheka eti rais mkaidi!!😂😂😂😂😂 wazungu msitupande vichwani tafadhari😂😂
 
kwa ufupi.
reli ya sgr ni reli ya kisasa itakayo chochea uchumi na kuongeza ajira.itahudumia mikoa yoote ya central corridor na nchi jirani kama congo,burundi,rwanda na uganda.

mradi wa bwawa la jnhpp utazalisha umeme mwingi na wa gharama ndogo.bidhaa za viwandani zitashuka bei kwa sababu gharama za uzalishaji na usafirishaji(sgr)zitakuwa chini sana.
kumbuka viwanda vinatumia umeme.

tatizo kubwa la nchi za africa ni wizi.ufisadi,rushwa na mikataba mibovu.
rais magufuli kajitahidi sana kwa upande huu kudhibiti ufisadi kiasi mpaka wapinzani kukosa sera.kwa kuwa kila eneo magufuli anashughulika nalo aachi kitu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye pambano la ngumi shabiki hatakiwi kusema iga mbinu za mpinzani wako!!!

Hispania watu waliokufa kwa corona Huwezi linganisha na Tanzania walikuwa wanakufa mabarabarani Kama kuku wa mdondo wapambane na hali yao .Nchi zilizokuwa zikiongoza kwa Vifo vya corona ulaya Hispania imo Baada ya Italia !!!
 
Leo nilikuwa nasikiliza KBC asubuhi nikasikia wanaitaja nchi moja kati ya zile za Scandinavia aidha Denmark au Norway siikumbuki inafuata hatua kama za Tanzania. Hawakuwa na lockdown wala nini, ila maisha yaliendelea. Sasa mnakuja na hoja kana kwamba Tanzania pekee ndio imefuata utaratibu huo. Acheni siasa maji taka tunataka nchi iwe na wanasiasa shupavu wenye hoja nzito zenye tija kwa jamii.
Sent from Geneva_ Switzerland
Umenichekesha mkuu, yani jiwe ndiyo role modal wako?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
El País ndio wamiliki wa Huffington Post au Huffington Post ndio wamiliki wa El País?
 
View attachment 1455981
Gazeti la pili kwa uuzaji nchini Hispania El País limechapisha habari isemayo "John Magufuli the African Bolsonaro" kutokana na njia anayotumia kupambana na janga la virusi vya corona. Gazeti hilo limetaja viongozi kama Donald Trump (Rais wa Marekani) na Jair Bolsonaro (Rais wa Brazil) kama viongozi waliokataa kuchukua hatua madhubuti dhiti ya virusi vya corona. Gazeti hilo limemtaja Rais wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania kama kinara wa Africa kwa ukaidi, limetoa shutma kwa Rais Magufuli kwa kugoma kutoa taarifa kuhusiana na idadi ya visa na vifo vya ugonjwa huu tishio duniani. Wameongezea kwa kuponda mbinu mbali mbali kama maombi, na upimaji wa sampuli za mapapai na mbuzi katika kugundua mapungufu ya maabara ya Taifa.

Hata hivyo gazeti hilo limemsifu Rais Magufuli kwa uwezo wake wa kuchapa kazi na kutokupokea rushwa na ujenzi wa miundo mbinu mingi wakati akilitumikia taifa kama Waziri wa Ujenzi.

Source: John Magufuli, o Bolsonaro africano

Maoni yangu: Taarifa hizi si nzuri kwa sekta ya utalii na hata biashara, japokuwa tuna mapungufu katika vita hii lakini hakuna taifa lisilo na mapungufu kila moja kuna sehemu limeteleza natumaini serikali litafuatilia nini ni chanzo kwa vyombo hivi kutufanya tuonekane wazembe na kudhihakiwa na kupakwa sifa mbaya.
Lazima tujiulize ni nini kipo nyuma ya tuhuma hizi? Hii ni vita na kama alivyosema Mh. Rais leo kuna kitu zaidi lakini hawezi kukisema sasa.
Kwa upande wangu, tunaweza kuchukua tuhuma hizi siyo kama tatizo, bali fursa za kujisahihisha pale ambapo tunaona hatukufanya vizuri na kujiimarisha pale ambapo tumefanya vizuri. Maisha ni mapambano. Binafsi huwa nachukulia 'criticisms' positive. Wakati naanza maisha nilikuwa sina kitanda, meza ya chakula, TV, kabati la nguo na la vyombo, nilikuwa na viatu pair moja na suruari pair mbili. Siku moja nikasikia habari kuhusu mimi mtaani na zilipelekwa na mfanyakazi wa ndani. Niliposikia nilikasirika sana na niliataka kumfukuza maana niliona kwa nini mambo ya nyumbani anayapeleka nje? Lakini nilipojitafakari nilikuta hatabari alizopeleka mtaani ni za kweli. Hivyo, badala ya kumfukuza niliorodhesha na nikapanga mkakati wa kuanza kununua kitu kimoja kimoja kadiri nilivyoweza kupata hela. Mwishowe nikajikuta vyote ambavyo majirani walijua sina nikajikuta ninavyo na baadhi yao kuwazidi na siku'react' kwa chochote. Hali hiyo ilinisaidia sana namna ya ku'deal' na criticisms hadi leo. Hata kama naweza kubisha. lakini deep down naona kilichosemwa na ninakifanyia kazi. Approach hii imenisaidia sana ku'improve' maisha yangu. Watu wengine wanachukia 'criticism'. Ni kama mtu anayekuonyesha kitu cha mbali kwa kidole: anasema (mfano) 'nyote ile...' Yaani anataka ufuatishe kidole chake ili uone nyota ilipo na siyo wewe kuangalia tu kidole anachoonyesha na kudhani hapo ndipo mwezi ulipo. We have to change challenges (including criticisms) into opportunities na kusonga mbele na siyo kubaki tumesimama na kuuhuzunika/kukasirika nk.
 
Umenichekesha mkuu, yani jiwe ndiyo role modal wako?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
Tanzania bado tuna changamoto nyingi maeneo mengi bado hayana huduma ya maji safi, afya, barabara, maslahi ya watumishi wa umma nk. Tulitegemea wapinzani waishupalie hoja moja wapo au zote kwa kuibana serikali ili maeneo yenye shida hizo yapatiwe ufumbuzi na serikali. Lakini cha kushangaza wapinzani wao wanakomalia hoja za kitoto toto sana. Hakuna chama chenye hoja ya kutetea maslahi ya wananchi zaidi ya maslahi ya matumbo yao.
From Geneva_Switzerland
 
Back
Top Bottom