Amepotosha lipi, give specific examplesLissu kila siku anasema mapya...
Amesema mengi ya kupotosha na ya uongo.....
Endelea tu kumfanya SOURCE ya kila jambo[emoji1787]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Amepotosha lipi, give specific examplesLissu kila siku anasema mapya...
Amesema mengi ya kupotosha na ya uongo.....
Endelea tu kumfanya SOURCE ya kila jambo[emoji1787]
Watu hapa magomeni kota wamesimama kumkumbuka Magufuli timu, gaidi hawatapenda
Wenye chuki na magu,mtaweweseka sana,Kwa hiyo Tanzania yote ipo Magomeni? shame on you
SIO KWA WATANZANIA BALI KWA WALIOPANGISHWA NYUMBA WEWE UKAE UNAKUMBUKA HUKU UMEPANGA UTAKUWA MWEHUNilikuwa nafuatilia runingani namna Rais Samia anavyowakabidhi majengo wale wananchi walioahidiwa kujengewa na hayati JPM. Alipoanza kuongea yule Bibi aliyekuwa ameongozana na Babu kama ndio wawakilishi wa wakazi 644 akawa mzalendo katika kutoa shukrani zake.
Kasimama mbele ya Rais SSH lakini akaanza kwanza kumshukuru JPM kwa maamuzi ya kizalendo ya kuamua kutumia kodi za wananchi kwa faida yao wenyewe ya kuwajengea majengo yatakayowasitiri wao na familia zao na yatakayokuwa ni sehemu ya mapambo ya kisasa ya jiji la Dar.
Kwamba Mungu amemchukua, ni maamuzi ya Mungu mwenyewe hakuna mwenye jeuri ya kuyapinga siku yake ikifika. Lakini kushukuru aliyekuwa na ujasiri wa kuyafanya ni deni ambalo bibi ameweza kulilipa vyema mbele ya Rais wa sasa.
JPM angeweza kutumia pesa iliyotumika katika kuhudumia anasa za tabaka la wenye vyeo, akaona hapana, ni lazima awajengee wakazi wa Magomeni makazi ya maana yatakayodumu kwa miaka mingi ijayo.
Angeweza kabisa kutumia pesa zilizotumika pale Magomeni katika kulipia safari za anasa za kwenda Dubai na kurudi kila mwisho wa wiki, angeweza kabisa kuzitumia zile pesa katika kuendeleza matanuzi yasiyodumu ya kibinadamu yanayofanywa kila siku na viongozi wengi wa kiafrika wa mataifa ya bara hili na hakuna mtu ambaye angeweza kumfanya lolote.
Kivitendo ilikuwa ni vigumu sana kwake kumtimizia kila aliyekuwa akimlilia njiani ili aweze kumtatulia shida zake mbalimbali, asingeweza kuwa na uwezo wa kufanya yote ya wasaidizi wake kwa wakati wote akiwa pale ikulu. Lakini hili la nyumba za kisasa kwa kaya 644 ni kielelezo au ni ishara ya utayari wake wa kuwasaidia wote wenye shida mbalimbali aliokuwa akikutana nao kila mara safarini.
Jukumu la kijasiri la kuyajenga makazi lilifanywa na JPM lakini jukumu la kuyatunza makazi hayo yasigeuke kuwa ni uchafu ulio karibu kabisa na katikati ya jiji, ni la wakazi wenyewe wa Magomeni wakiongozwa na yule Bibi aliyemshukuru hayati JPM mbele ya SSH.
Kimwili JPM alitutoka mwaka mmoja uliopita na siku chache. Lakini kila tutakapokuwa tukikatiza tukiwa ndani ya vyombo vya usafiri maeneo yale ya Magomeni tutakuwa tukimkumbuka hayati. Ataendelea kuishi kupitia ujasiri wa maamuzi ya kujenga makazi ambaye kila mtazamaji atakuwa akimkumbuka.
Alichokifanya JPM ni sawa na kile alichokifanya Hayati Karume kule Michenzani Unguja. Kwamba alikwisha kuondoka duniani tangu april 1972 lakini ushahidi wa upendo aliokuwa nao bado upo hai mpaka leo hii.
JPM alikuwa ni populist leader, na alitamka wazi bungeni siku ya kwanza kabisa alipohutubia. Kwamba anajivunia wingi wa wapiga kura waliompigia kura na atakuwa nao bega kwa bega. Ni maamuzi magumu sana kujenga majengo ya kisasa, kwani ni kama amekubali kuziba riziki nyingi za wasomi wenye kumsaidia kazi mbalimbali.
Ni kama alijua kuwa hana muda mrefu juu ya uso wa dunia, hivyo akaamua kuacha amejenga makazi kwa wakazi wa Magomeni. Ni maamuzi ya kizalendo ambayo siku zote hayawezi kukosa wa kuyapinga.
Ulale pema peponi JPM.
Story za kwenye kahawa zimeathiri fikra zako sana. Kama hujanielewa basi nakishauri usome comment #94 ya mdau hapo.Wananchi wanahitaji maendeleo, kwa nyerere hii kitu haikuwepo....labda ungesema mwinyi hapo sawa.
Unalalamika masuala haya Tanzania, ukienda huko Somalia au Sudan nadhani utalalamika mpaka sauti itafika kwenye mawingu.Issue sio wadhifa wa mtu, issue Ni uhai wa mtu
Mambo aliyoyafanya Nyerere ndio aliyoyafanya Magufuli. Yet unakuja kumponda Nyerere na kumsifia Magufuli kwa mambo yale yale.Tunahitaji maendeleo....
Weweseke nini kwani tuna lala nje?Wenye chuki na magu,mtaweweseka sana,
Nipo na maza akoMuulize mama yako
Nipo na maza akoMuulize mama yako
Alikuwa anapiga pesa kupitia manunuzi snPesa za kununulia ndege moja ya kisasa ya ATCL huenda ingetosha kujenga majengo kama yale ya magomeni katika mikoa kumi.
Magufuli alikuwa ni mtu wa ovyo ovyo kabisa.
Wewe ni mbumbu na mzungu wa reli kabsa,unasema kipindi cha mwinyi kulikuwa na pesa mfukoni?,sina hakika kama ulikuwepo,hakuna kipindi kilikuwa kigumu na maisha magumu kama kipindi cha mwinyi,Mambo aliyoyafanya Nyerere ndio aliyoyafanya Magufuli. Yet unakuja kumponda Nyerere na kumsifia Magufuli kwa mambo yale yale.
Ukieleweshwa unaibuka na kauli "Tunahitaji maendeleo.."
Sasa tuambie unaungumzia maendeleo gani? ya vitu au watu?
Kama ni MAENDELEO YA VITU basi Nyerere na Magufuli wapongezwe. Kama ni MAENDELEO YA WATU (hasa pesa mfukoni) pongezi zimfikie Mwinyi..
Ila kutuambia Magufuli anamzidi Nyerere unadhihirisha usivyojua lolote kuhusu wawili wale.
Mkuu manunuzi ya ndege ni muhimu sana kwa mustakabali mzima wa uchumi wa taifa. Watu tatizo letu tunaangalia leo tu na tunamhukumu JPM kwa upeo wetu unaoishi leo tu.Pesa za kununulia ndege moja ya kisasa ya ATCL huenda ingetosha kujenga majengo kama yale ya magomeni katika mikoa kumi.
Magufuli alikuwa ni mtu wa ovyo ovyo kabisa.
Hakuna kipindi chepesi tangu awamu ya kwanza ya Nyerere, kuwa na pesa mfukoni au kutokuwa nazo ni ujanja wako na wepesi wa akili yako.Wewe ni mbumbu na mzungu wa reli kabsa,unasema kipindi cha mwinyi kulikuwa na pesa mfukoni?,sina hakika kama ulikuwepo,hakuna kipindi kilikuwa kigumu na maisha magumu kama kipindi cha mwinyi,
Vijana hawaelewiKumbe humu jf vijana ni wengi sana !! Nyerere wakati anang'atuka aliacha viwanda zaidi ya 400 na tukisema viwanda wajue vilikuwa viwanda kweli kweli ! Hayati Mkapa aliwahi kukiri kwamba katika uongozi wake kitu anachojutia sana kukifanya ni kubinafsisha vile viwanda !! Mzee Mwinyi alichofanya ni kuachia watu waingize bidhaa kutoka nje kiholela na ndipo maadili yote yalianza kuporomoka yakaanza madili !!!
Si hoja, ni indicator hiyo! Pokea jamaa alikuwa hafai.Kunenepa kwa mke wake ni hoja ya kitoto sana, siitegemei kutoka kwa mtu wa umri wako.