Elections 2015 Magufuli aliongea na Mh. Waziri Kigoda akiwa ICU!

Elections 2015 Magufuli aliongea na Mh. Waziri Kigoda akiwa ICU!

Maana ya ICU ni nini? Kwanini mgonjwa atolewe ward ya kawaida apelekwe ICU? Mazingira ya chumba cha ICU liko be vipi?

Kuna chumba kinaitwa HDC=High Dependency Care(Chumba cha Wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu/huduma tegemezi)
Mgonjwa anaekua kwenye hiki chumba anakua hajiwezi kufanya chochote bila msaada toka kwa muuguzi na ni lazima awe na mpira wa kukojolea na wengi wao wanalishwa kwa kutumia mpira unaopitishwa puani.Kila Wodi katika Hospitali ya Bugando ina hiki chumba tena kinatazamana na Ofisi ya wauguzi.

ICU=Intensive Care Unit (Kitengo cha Huduma Kubwa) Hiki chumba katika Hospitali ya Bugando kiko wodi na2 na ni karibu kabisa na Chumba cha upasuaji na Idara ya Dharula.

Jina lingine maarufu la hicho chumba alichopelekwa Kigoda(R. I. P) kinaitwa Chumba cha Bahati Nasibu kiukweli ni Wagonjwa wachache sana wanaopelekwa kwenye hicho chumba wanatoka salama wengi wao hufariki. Wagonjwa wote waliolazwa humo wanapumulia Mashine ambazo zikileta hitilafu tu kwa muda mfupi Uhai wao unakua mashakani.

Sasa huyu Magufuli anapolidanganya Taifa kua aliwasiliana na Marehemu kabla na akiwa ICU ana maana gani?

Sasa fikiria mgonjwa anaeihitaji uangalizi maalumu hawezi kufanya chochote kile bila kusaidiwa ingawa anakua ajitambua kwa kiasi flani je huyo aliyeko ICU ambae kwa asilimia kubwa anaendelea kuishi kwa msaada wa mashine atawezaje kutumia Simu au Laptop tena simu yenyewe Smartphone?

Jamani mambo mengine tusipende kufanya Siasa tu?
 
Mimi sijamuelewa Mhe. Magufuli leo akiwa uwanja wa ndege kupokea mwili wa aliyekuwa waziri wa Viwanda na biashara amesema:

- Kabla waziri Kigoda hajapelekwa ICU nje ya nchi niliongea nae akanishauri juu ya kuwasaidia wafanyabiashara nchini.
- Alipokuwa nje ya nchi akiwa ICU alinitumia email na kunishauri.

Maswali yangu:
-Hivi mpaka mtu anapelekwa ICU anakuwa na uwezo wa kuchati?
-Je, Magufuli anasema ICU tunayoijua au?

Huyu ndo anataka urais?


Magufuli amechanganyikiwa kabisa.
Kuna suku atasema ameongea nae baada ya kufariki.
 
Tuache Familia,jamaa na Watu wa Karibu na Dr.Abdallah Kigoda waomboleze na kumzika Ndugu yao kwa amani na salama, tuache kuhusisha Jina la Kigoda na Siasa Chafu.Dr.Kigoda kafanyiwa rafu nyingi sana 2005 lakin hakuwa mtu wa Visasi wala Mbwembwe na Madaha mengi kama walivyo wanasiasa lakini alikuwa ni Mtu mwenye bundle nyingi sana za Kichwani.Pole Mh.Mkapa, Pole Familia
Familia ilitakiwa kutokubali siasa kwenye msiba wao, lkn kwa kukubali mwanasiasa akatafute "huruma ya waombolezaji" kwenye msiba wao basi ikubali dhihaka!

Tumechoka wanasiasa wasiopambana na "hoja" na kukimbilia misibani kutafuta huruma.
 
Kama aliweza kumtembelea rais Gadafi wa Kuwait alipomaliza mazungumzo naye akamtembelea rais Saadam Hussein wa Libya kabla hajaondolewa madarakani. Ni nini cha kumshinda kuongea na marehemu akiwa ICU? Si ulimwona alivyokuwa amehuzunika??
Alionesha alivyompenda mchapa kazi mwenzake jamani. Tz yetu na siasa zake. Ni kupiga dili tu kila mahali hata msibani. Anatamani kura zote za Handeni zimwendee. Oktoba 25 si mbaali kama anavyofikiri. Kuwabadilisha watu maamuzi yao sasa si rahisi
 
Tuache Familia,jamaa na Watu wa Karibu na Dr.Abdallah Kigoda waomboleze na kumzika Ndugu yao kwa amani na salama, tuache kuhusisha Jina la Kigoda na Siasa Chafu.Dr.Kigoda kafanyiwa rafu nyingi sana 2005 lakin hakuwa mtu wa Visasi wala Mbwembwe na Madaha mengi kama walivyo wanasiasa lakini alikuwa ni Mtu mwenye bundle nyingi sana za Kichwani.Pole Mh.Mkapa, Pole Familia
Sidhani kama mleta thread kaingilia msiba, anamuongelea mtu wa nje kabisa. Lakini mkuu, msiba ni majonzi ila hausimamishi dunia. Poleni nyote mlioguswa na msiba huu.
 
Tutakuja kujuta zaidi ya uongozi wa sasa...! Makomeo ameonyesha hayupo makini na ni mtu wa kukurupuka....rejea Gadafi rais Libya, kasema pia rest in peace kikwete na sasa mambo ya mgonjwa wa ICU kutuma email...
 
Tuache Familia,jamaa na Watu wa Karibu na Dr.Abdallah Kigoda waomboleze na kumzika Ndugu yao kwa amani na salama, tuache kuhusisha Jina la Kigoda na Siasa Chafu.Dr.Kigoda kafanyiwa rafu nyingi sana 2005 lakin hakuwa mtu wa Visasi wala Mbwembwe na Madaha mengi kama walivyo wanasiasa lakini alikuwa ni Mtu mwenye bundle nyingi sana za Kichwani.Pole Mh.Mkapa, Pole Familia
Mbona Magufuli yeye hakuiacha familia ipokee mwili wa Mpndwa wao, kaanza kufanya siasa hapo hapo, hivi tangu lini mtu akaruhususiwa kuingia na simu ICU ?
 
Mimi sijamuelewa Mhe. Magufuli leo akiwa uwanja wa ndege kupokea mwili wa aliyekuwa waziri wa Viwanda na biashara amesema:

- Kabla waziri Kigoda hajapelekwa ICU nje ya nchi niliongea nae akanishauri juu ya kuwasaidia wafanyabiashara nchini.
- Alipokuwa nje ya nchi akiwa ICU alinitumia email na kunishauri.

Maswali yangu:
-Hivi mpaka mtu anapelekwa ICU anakuwa na uwezo wa kuchati?
-Je, Magufuli anasema ICU tunayoijua au?

Huyu ndo anataka urais?
Acha kunukulu watu vibaya, Magufulu hajasema utumbo wako huo. Alisema aliongea naye akiwa nje kwa ajili ya matibabu. Hii inamaanisha kabla hali yake haijawa mbaya sana. Acheni kuongelea mambo ya kuchanganya watu. Acha watu waomboleze. Kama huna hoja njoo nikupe hoja uweke kwenye jamvi.
 
Shemeji yangu alipata ajali ya gari Abu Dhabi na alioawafanyia ICU kwa siku zaidi ya 5, tulip example kuzungumza nae, japo kuwa alikuwa na maumivu makali sana. Mara nyingi inawezekana ku fanya mawasiliano mgonjwa akiwa ICU.
 
Back
Top Bottom