Mahakama Kuu yatengua hukumu ya kuvuliwa Uwakili dhidi ya Fatuma Karume

Mahakama Kuu yatengua hukumu ya kuvuliwa Uwakili dhidi ya Fatuma Karume

Hii ndio taarifa mpya iliyotufikia muda huu kutoka Mahakamani .

Taarifa inaeleza kwamba Mahakama kuu imeona kwamba Fatuma Karume alihukumiwa bila kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya Kamati ya maadili ya Mawakili , hivyo imetengua hukumu yake na kuitaka Kamati hiyo kumaliza jambo hilo kwa haki

Ikumbukwe kwamba Mlalamikaji kwenye hili Sakata la Wakili Msomi Fatuma Karume lililojaa chuki , Wivu na uzandiki alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali , Je unadhani bado anafaa kukalia ofisi hiyo ?

View attachment 1825533
I'll try to put this as simple as i can
Mfumo wa nidhamu kwa mawakili umegawanyika mara tatu
1. Advocate committee (kamati ya maadili ya mawakili)
2. Jaji wa mahakama kuu
3. Jaji mkuu

Sasa kilichotokea jaji wa mahakama kuu Hon. Feleshi JK alimsimamisha wakili karume na kuamuru msajili apeleke shauri lake mbele ya kamati ya maadili ya mawakili kwa hatua zaidi.

Kilichotokea Mwanasheria mkuu akapeleka malalamiko yaleyale pamoja na mengine mbele ya kamati ya maadili ya mawakili.

Sasa mahakama kuu leo imesema haikuwa sawa kwa mwanasheria mkuu kupeleka malalamiko upya wakati kuna amri ya mahakama kuu kumuagiza msajili apeleke malalamiko mbele ya mahakama kuu.

Hivyo basi amri ya Jaji Feleshi kumsimamisha Wakili karume bado inaendelea. Mpaka kamati ya mawakili itakapo kutana tena.

Ms Karume amesema atamuandikia msajili barua kuomba kurenew leseni yake ya uwakili kwani katazo la mda (interim order) la kumsimamisha limeisha (hii ni kwa mtazamo wake)

Disclaimer: huwenda tafsiri yangu ya hukumu imekaa kisheria mno tusaodoane kuelekezana
 
Fatma Karume, hata kama ana matatizo yake yoyote kama mtu, ni mwanamke shupavu, kati ya wachache sana, aliyetusitiri kwa kuongea ukweli bila kuogopa wakubwa.

Watu wa aina hii, nasema wametusitiri, kwa sababu wametuondolea aibu ya watu wote mamilioni kukaa kimya bila kukemea maovu ya wazi kabisa. Sasa hivi, tukiangalia kipindi cha miaka sita iliyopita, ambacho wengi waliogopa kusema ukweli, kuna wachache kama kina Fatma Karume hawakuona uzito kusema ukweli, na kukemea maovu ya utawala, hata kama hilo lilimaanisha kuhatarisha usalama wao binafsi.

Nimefurahishwa na habari hizi kwa sababu haki imetendeka. Kwa sababu wingu la woga linazidi kutoweka, kwa sababu muelekeo wa nchi unarudi relini, kwa sababu watawala wanaonekana kuanza kujirudi, kwa sababu, muelekeo tuliokuwa nao ulikuwa unatupeleka pabaya sana.

Hii ni siku ya ushindi mzuri, hatq kama ni mdogo sana kwa kulinganisha na mapambano yaliyo mbele yetu, kwa wapenda haki wote Tanzania, Afrika na duniani kiujumla.
 
Leo nilikuwa nasikiliza BBC World Service, walikuwa wanaongelea kuhusu protesters wa Thailand, Hong Kong na Myanmar wanaotaka mabadiliko ya kikatiba.

Kuna sehemu mtu akasema, hawa protesters wanakosa support ya watu wengi, kwa sababu wanajikita kudai mambo ya katiba ambayo watu wa kawaida hawaoni umuhimu wake.

Wangeongelea mambo kama ya bei za vitu kupanda, wangeweza kueleweka na kupata support kirahisi na watu wengi zaidi.

Sasa, naona issue ile ile inajirudia hapa JF kuhusu mambo ya Tanzania.
Ni kukosa elimu ya kufahamu katiba ni nini na inachukua nafasi gani kwenye maisha yetu.

Matatizo yote tuliyonayo mpaka mifumo yote, sababu kubwa ni katiba
 
Ipo siku na haipo mbali sana kuna watu watalilia awamu ya Tano japo iwepo tu Kwa siku chache Ila Hilo Jambo halitotokea.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]awamu iliyowafunga watu midomo.?

Nilikua napita maeneo fulani ni genge la mboga la wamama. Walikua wanalngea kwa kujiachia issue za siasa huku wakisema saizi tupo huru hatuogopi kusema
 
Kwani wewe unajua kafa kwa nini?
Tumetangaziwa chanzo cha kifo chake japo inawezekana isiwe kweli ila pia kudai kuwa kafa kwa corona bila ushahidi au sababu yeyote ya msingi hiyo haikubaliki.

Mtu anakwambia kafa kwa corona kwa sababu aliidharau corona ni sababu ya kipumbavu.
 
Ni kukosa elimu ya kufahamu katiba ni nini na inachukua nafasi gani kwenye maisha yetu.

Matatizo yote tuliyonayo mpaka mifumo yote, sababu kubwa ni katiba
Inawezekana ni kweli. Ingawa binafsi, nafikiri matatizo yetu ndiyo yametuletea katiba mbovu, si katiba yetu mbovu ndiyo imetuletea matatizo yetu.

Ndiyo maana hata mazuri ya katiba yetu mbovu hatuyatumii kikamilifu.

But for the sake of argument, suppose you are right.

Lakini, ukiwa na ramani ya vita nzuri sana, bila ya uwezo wa kuwashawishi wanajeshi, unaweza kupigwa ukaangukia pua na ramani yako ya vita isikusaidie kitu.

Inabidi ku balance the theoretical and the practical, the abstract and the actual.

Donald Rumsfeld anakuambia "You go to war with the army you have, not the army you want".

Tunapenda ndugu zetu waelewe umuhimu wa katiba, lakini, inawezekana hayo ni mambo ya kueleza mbeleni, kwanza tuwavute ndani ya hema kwa lugha wanayoielewa vizuri zaidi ya "bei za vitu inapanda, watu wanashindwa kula vizuri na kujenga".

Hii ndiyo point aliyokuwa anaisema huyo jamaa aliyekuwa anajadili Thailand,Myanmar na Hong Kong BBC. Naona hata Bongo ina apply.
 
Piga kazi mama Samia tumecheleweshwa mno kama taifa
 
Inawezekana ni kweli. Ingawa binafsi, nafikiri matatizo yetu ndiyo yametuletea katiba mbovu, si katiba yetu ndiyo imetuletea matatizo yetu.

But for the sake of argument, suppose you are right.

Lakini, ukiwa na ramani ya vita nzuri sana, bila ya uwezo wa kuwashawishi wanajeshi, unaweza kupigwa ukaangukia pua na ramani yako ya vita isikusaidie kitu.

Inabidi ku balance the theoretical and the practical, the abstract and the actual.

Donald Rumsfeld anakuambia "You go to war with the army you have, not the army you want".

Tunapenda ndugu zetu waelewe umuhimu wa katiba, lakini, inawezekana hayo ni mambo ya kueleza mbeleni, kwanza tuwavute ndani ya hema kwa lugha wanayoielewa vizuri zaidi ya "bei za vitu inapanda, watu wanashindwa kula vizuri na kujenga".

Hii ndiyo point aliyokuwa anaisema huyo jamaa aliyekuwa anajadili Thailand,Myanmar na Hong Kong BBC. Naona hata Bongo ina apply.
Uzuri ni kwamba dunia inaenda kwa kasi sana. Katiba zitabadilishwa huko mbele ambako idadi kubwa ya jamii utakua na uelewa wa kutosha na kama kweli hitaji lao la muhimu litakua ni hilo
 
Tumetangaziwa chanzo cha kifo chake japo inawezekana isiwe kweli ila pia kudai kuwa kafa kwa corona bila ushahidi au sababu yeyote ya msingi hiyo haikubaliki.

Mtu anakwambia kafa kwa corona kwa sababu aliidharau corona ni sababu ya kipumbavu.
Basi usipanic mkuu si unajua hapa kilaa mtu anaongea la kwake ilimradi siku iende?

Jamaa haijalishi kafa kwa nini, issue ni kwamba hatunaye tena. Maisha yaendelee na tuendelee kuijenga nchi yetu ikiwa ni pamoja na kumpa support aliye madarakani.

Pia tunapaswa kumwambia asisahau kuweka mfumo. Asitumie ile style ya one man show
 
Basi usipanic mkuu si unajua hapa kilaa mtu anaongea la kwake ilimradi siku iende?

Jamaa haijalishi kafa kwa nini, issue ni kwamba hatunaye tena. Maisha yaendelee na tuendelee kuijenga nchi yetu ikiwa ni pamoja na kumpa support aliye madarakani.

Pia tunapaswa kumwambia asisahau kuweka mfumo. Asitumie ile style ya one man show
Si mimi niliyopanic wenye hasira na kushughulishwa na maiti ndio waliyopanic, mimi binafsi Mwendazake ameshafariki basi ila sasa kuna watu kama hawaridhika kwamba Jiwe kafa tu halafu imeishia hakupigwa hata kofi kama rais wa france.
 
Uzuri ni kwamba dunia inaenda kwa kasi sana. Katiba zitabadilishwa huko mbele ambako idadi kubwa ya jamii utakua na uelewa wa kutosha na kama kweli hitaji lao la muhimu litakua ni hilo
Kusema ukweli hata 1992 tulivyobadili mfumo kukubali vyama vingi ilikuwa kama sijaamini jinsi zoezi lile lilivyotokea kwa haraka sana, bila kulazimishwa sana na watu.

Yani ilikuwa watu wenyewe wamesema mfumo wa chama kimoja poa tu, Nyerere akasema twende na vyama vingi, sababu za kuzuia vyama vingi zilizokuwapo miaka ya 1960s hazipo tena, tukabadili.

Baadaye nikaja kusoma Nyerere alivyokataza vyama vingi miaka ya 1960s, nikaelewa vizuri zaidi kwa nini alisema vile.

Alikuwa kashaona Romania huko walivyomuondoa Nikolai Causescu, akaona bora CCM ikubali mabadiliko na kuya control, yakija kwa nguvu za wananchi, nchi inaweza kuwa haitawaliki by then.
 
Si mimi niliyopanic wenye hasira na kushughulishwa na maiti ndio waliyopanic, mimi binafsi Mwendazake ameshafariki basi ila sasa kuna watu kama hawaridhika kwamba Jiwe kafa tu halafu imeishia hakupigwa hata kofi kama rais wa france.
Nadhani hawaamini kama kweli amekwenda. Au kwa dhati wanajua wakizungumzia issue za mwendazake, kuna watu hasa wale waliokua wanafurahia utawala wake, wanakereka kwakua alikwenda ghafla sana. Huwezi kuamini, nilipopata taarifa za kifo chake, nilitoa chozi japo sikupenda style yake ya uongozi. Utafika wakati watasahau wenyewe na maisha yataendelea
 
Kusema ukweli hata 1992 tulivyobadili mfumo kukubali vyama vingi ilikuwa kama sijaamini jinsi zoezi lile lilivyotokea kwa haraka sana, bila kulazimishwa sana na watu.

Yani ilikuwa watu wenyewe wamesema mfumo wa chama kimoja poa tu, Nyerere akasema twende na vyama vingi, sababu za kuzuia vyama vingi zilizokuwapo miaka ya 1960s hazipo tena, tukabadili.

Baadaye nikaja kusoma Nyerere alivyokataza vyama vingi miaka ya 1960s, nikaelewa vizuri zaidi kwa nini alisema vile.

Alikuwa kashaona Romania huko walivyomuondoa Nikolai Causescu, akaona bora CCM ikubali mabadiliko na kuya control, yakija kwa nguvu za wananchi, nchi inaweza kuwa haitawaliki by then.
Ni miaka michache sana imepita tangu mfumo wa vyama vingi uanze kutumika. Waliozaliwa mwaka huo, ndio kwanza walianza kupiga kura mwaka jana.

Hivyo bado kuna masalia vizazi vya mfumo wa chama kimoja ambao naamini wakishaondoka, basi mambo mengi sana ya kimfumo yatabadilishwa
 
Hii ndio taarifa mpya iliyotufikia muda huu kutoka Mahakamani .

Taarifa inaeleza kwamba Mahakama kuu imeona kwamba Fatuma Karume alihukumiwa bila kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya Kamati ya maadili ya Mawakili , hivyo imetengua hukumu yake na kuitaka Kamati hiyo kumaliza jambo hilo kwa haki

Ikumbukwe kwamba Mlalamikaji kwenye hili Sakata la Wakili Msomi Fatuma Karume lililojaa chuki , Wivu na uzandiki alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali , Je unadhani bado anafaa kukalia ofisi hiyo ?

View attachment 1825533


Fatma Karume I love you....wewe ni mpambanaji wa HAKI.

Against all odds you are still shining.

Keep it up Darling
 
Huyu jamaa inawezekana hata yeye mwenyewe alikuwa hajui kama JPM alikuwa hoi ,pia inaonekana JPM alifanya ugonjwa kuwa siri hata kwa wasaidizi wakw
Kweli kabisa. Ndio maana Chalamila akaamua ajiropokee tu kuwa "nimeongea naye leo asubuhi...." Dah nchi ngumu hii!
 
Back
Top Bottom