Mahakama ya Kisutu imewatia hatiani Viongozi wa CHADEMA na kuwahukumu kulipa faini ya Tsh. Milioni 350 au kwenda jela, Wapelekwa Segerea

Hahahaaaaa....... Usiitafsiri sheria kama madaraja ya ulanzi yaani mtogwa, mkangafu na mdindifu.

Ukilipa faini historia ya kesi inaishia hapo unarudi bungeni kuendelea kula bata!

Napenda Mndindifu lakini hukumu ikitolewa swali la aina ya utekelezaji halitatengua hukumu Kwa njia yoyote. Nimesomea sheria Gerezani lakini nikawa mbobevu
 
Umewaza deep sana Dr. Kweli hii inawezekana.
 
Jumla ya faini sh. 350 ml ni makusanyo makubwa kwa serikali kuliko kuwafunga miezi mitano. Lakini kwa CHADEMA na amani ya nchi ni ushindi.
 
Wanafilisiwa ili wakose jinsi ya kuendesha kampeni za uchaguzi. Makosa gani hayo yanayogharimu kiasi chote hiki? Na pesa zinakwenda kwa nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Nchi imeishaingiliwa Ndugu yang, hicho kiasi atakuwa Hakimu kaletewa tu orodha na kiasi kila mmoja akaambiwa kuwa yeye Kazi yake nikuandika Maelezo ya Hakumu tu na kusoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Kwenye hizo pesa tutakazowachangia faini viongozi wa Chama ondoa "Chenchi" ya D Mashinji, huyu hatutamchangia"

Alisikika mlevi mmoja karibu na bar iliyopo mkabala na mamlaka ya mapato kisutu, nchini danganyika.
 
HAKIMU SIMBA: "Mahakama imeepusha adhabu ya vifungo kwa Washitakiwa"

Aseme tu 'wameogopa' nguvu ya umma na kuamua kutuliza hali ya kisiasa nchini ambayo imetikisika kufuatia sakata hili linalozua maswali mengi juu ya nia ya serikali kuweka mazingira huru na ya haki katika kufanya siasa za vyama vingi chini ya mwamvuli wa demokrasia na chaguzi huru nchini Tanzania.
 
Hata hivyo nimiezi mitano kwakila kosa yaani kama umekutwa namakosa 12 inamaana utakaa jela miezi 60 sawasawa na miaka 5

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo technically wanaachiwa Kwa kuwa halikuwa shtaka la msingi...anyway Mimi ni layman kwenye Sheria
Hata mimi maamuma wa sheria maana tuliambiwa hukumu leo mbona tena wanaishia wametiwa hatiani kwa makosa 12/13 hivyo wapewe adhabu kali, siku ya kusoma adhabu ni nyingine
 
Wakati mwengine Serikali inajidhihilisha hadharani kwamba ndiye mvunjifu wa haki na katiba hapa inchini

Kifupi serikali inajidhalilisha mchana kweupee
Sasa tunawadhalilisha zaidi kwankuwalipia ndani ya 24hours watu 10m wakitoa kila mmoja 350
 
That means, hawawezitena kugombea Urais, ubunge au udiwani kisa wamekutwa na makosa ya jinai.

Kuna vacant position already ndani ya Chadema ya wagombea wapya kwani hawa hata wakikata rufaa hawawezi pata miezi 7 hii ilobaki.
 
Tuendelee na siasa, haya mengine tutapandishana pressure bure.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…