Jela ni kubaya mnoo, mi nimewahi kukaa rumande kwa miezi 2, kwa kosa alilolifanya mtu mwengine kabisa, lakini ningeshauri viongozi wa CHADEMA ni aheri kuenda jela tu kuliko kulipa mamimilioni hayo, wakienda jela wata gain huruma ya Watanzania na watajitangaza zaidi kuliko kampeni yenyewe,
kwa mtazamo wangu ni fursa kubwa sana kwa CHADEMA, miezi mitano kitu gani banaaa katika kipindi hiki ambacho kufanya siasa kwa vyama pinzani ni marufuku? Wapite tu njia ile ile ya wakina Mandela, Walter sisulu, maalim seif and the like.
Democrasia ni gharama, unalipa mamilioni mwenzako anayatumia kwa kukukandamiza zaidi, sasa unafanya siasa gani? Mi nasema hakuna kuwachangia Hawa watu. Dhahabu sharti ipitie kwenye moto ipigwe pigwe na nyundo kubwa ile iitwe dhahabu, tusiwalee Hawa viongozi enendeni tu jela muwe imara zaidi