Mahakama ya Mafisadi imekufa kifo cha kawaida?

Mahakama ya Mafisadi imekufa kifo cha kawaida?

Fisadi mzalendo kachemsha na mahakama yake ya mafisadi imebaki hadithi tu atampeleka nani amwache nani ?
Mafisadi woooote wapo CCM na NI wamoja si rostam so luwasa so mzee meko[emoji15][emoji15]

Screenshot_20190313-073128.jpeg
Screenshot_20190313-073140.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii Mahakama jina lake rasmi ni Mahakama Kuu, Kitengo cha Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, yaani Corruption and Organized Crime Division. Ni moja ya division za Mahakama Kuu. Division nyingine za Mahakama Kuu ni High Court Land Division, Labour, na Commercial.

Mwenye mamlaka ya kuamua ni kesi ipi inafaa kwenda division ipi ni DPP. Na anaamua kwa kuzingatia sheria na vigezo vya kikanuni.

Usiniulize kwani Kisutu ni Mahakama Kuu.

Ni kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Dar es Salaam, Kisutu, huwa ina exercise extended jurisdiction yaani, Hakimu Mkazi anapewa mamlaka ya kuwa Jaji na Mahakama ya Hakimu Mkazi inakuwa na hadhi ya Mahakama Kuu, na hivyo kuamua kesi za Mahakama Kuu. Na hata mtu akikata rufaa kutokana na hukumu hiyo, rufaa inaenda Mahakama ya Rufaa.

Mwanasheria ndiye atanielewa zaidi
Wacha kelele wewe Sasa huyu anayesema anapambana na ufisadi akaweka mahakama ambayo haina kazi alimaanisha Nini basi kwa maana fupi tz HAKUNA mafisadi Wala mapambano yoyote no uonevu tu inaoendelea...... Kwanza mafisadi kina pengo tibsijuka change wapo kitaa[emoji48][emoji48][emoji48][emoji48] HAKUNA mapambano na mahakama haina kazi [emoji15][emoji15][emoji15] PERIOD

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wacha kelele wewe Sasa huyu anayesema anapambana na ufisadi akaweka mahakama ambayo haina kazi alimaanisha Nini basi kwa maana fupi tz HAKUNA mafisadi Wala mapambano yoyote no uonevu tu inaoendelea...... Kwanza mafisadi kina pengo tibsijuka change wapo kitaa[emoji48][emoji48][emoji48][emoji48] HAKUNA mapambano na mahakama haina kazi [emoji15][emoji15][emoji15] PERIOD

Sent using Jamii Forums mobile app


Mahakama haifanyi kazi kwa mashinikizo na mambo ya kusikia. Makosa ya ufisadi ni makosa ya jinai. Makosa ya jinai yanahitaji ushahidi usiyoacha chembe ya shaka ila kumtia hatiani mtuhumiwa. Kujenga Mahakama kunaweza kukawa na msukumo wa kisiasa ila kuendesha kesi ni lazima kuzingatiwe sheria na siyo mihemko na hisia.

Mtu kuwa na tuhuma za ufisadi siyo lazima atangazwe na Media. Kama mnabisha kuwa Mahakama ya Mafisadi haifanyi kazi nendeni pale nyuma ya Mawasiliano Towers mkaone.

Sheria ni taaluma kama ilivyo daktari, ni lazima kujiridhisha na tatizo kabla ya kutoa tiba. Kesi lazima zifanyiwe upembuzi kujiridhisha na ushahidi kabla ya kupeleka mahakamani.

Na siyo kila kesi inafaa kupelekwa mahakamani.

Kesi za jinai zinahitaji udhibitisho dhahiri kwa hiyo lazima DPP ajiridhishe na ushahidi.

Kazi ya Mahakama ni kusimamia haki na siyo kukomoa mtu kwa kuwa tu jamii inamuhisi kuwa ni mhalifu
 
Mahakama ya Mafisadi ipo, na jengo lake lipo nyuma ya ofisi za TCRA, na ndani ya geti la Law School. Kila siku watuhumiwa wanaletwa hapa na majaji wanakuja. Acheni kusambaza uongo eti hii mahakama haifanyi kazi
Tudagaa tu
 
Kwahiyo huko mahakama ya mafisadi waandishi wa habari hakuna ,mana kwengine kesi zote tunaona kwenye tv,acha fiksi aikambe
Mahakama ya Mafisadi ipo, na jengo lake lipo nyuma ya ofisi za TCRA, na ndani ya geti la Law School. Kila siku watuhumiwa wanaletwa hapa na majaji wanakuja. Acheni kusambaza uongo eti hii mahakama haifanyi kazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo huko mahakama ya mafisadi waandishi wa habari hakuna ,mana kwengine kesi zote tunaona kwenye tv,acha fiksi aikambe

Sent using Jamii Forums mobile app

Hata kama wangekuwepo, siyo kila kesi inaripotiwa.

Kwani hizo za Kisutu na kwingine zimeripotiwa zote?


Mimi ni mwanasheria na ninachokuambia nina uhakika nacho
 
Ss mkuu ndo kusema umekosa hoja mpk unataka nianze na kutaja majengo ya mahakama?daah kwel tuna safar ndefu sana kutoka hapa tulipo


Sasa kama hujui jengo la mahakama husika, inakuwaje unabisha kwamba haifanyi kazi? Umeenda hapo ukakuta pamefungwa?

Jana tu akina Kitilya na Sioi pamoja na Shose walipelekwa pale.

Lengo la kukuuliza jengo ni kutaka kujua ufahamu wako.

Kama hujui ndiyo ninakufahamisha sasa kwamba mahakama inatenda kazi na uache kubisha usiyoyajua
 
Mahakama ya Ufisadi ilianza rasmi ikiwa ni jitihada za serikali ya awamu ya 5 kupambana na ufisadi nchini. Uazishwaji wa mahakama husika, uliambatana na uwepo wa kesi nyingi za uhujumu uchumi ikiwa ni uwepo wa wateja wa mahakama hiyo.

Wingi wa kesi hizo zikiwa bado katika hatua za mwanzo mahakamani Kisutu, jana limekuja wazo la kushauri uwezekano wa kusamehe watuhumiwa iwapo wataungama makosa na kuwepo uwezekano wa kulipa fedha kulingana na kiwango cha ufisadi.

Magwiji wa sheria naombeni mtujuze juu ya uwepo wa mahakama ya ufisadi iwapo kila mtuhumiwa ataamua kuungama na kuahidi kulipa kiasi cha fedha aliyofisadi.
 


Toka mwanzoni kabisa tulionya kuwa mahakama ya ufisadi ni upumbavu na ujinga ,watu wakatuona wakorofi. Haya sasa ina kazi gani kuwepo kama watu wanalipa hela na kusamehewa ili kesi ziishe. Meko una roho ya usumbufu na uharibifu sana katika maisha ya watu! Tulijua utafeli tu yaani




Mr yamoto.
IMG_20190925_100046.jpeg
 
Tunazihitaji sana hizo hela za mafisadi ili tuendelezee ujenzi wa standard gauge na stiglers gorge! Hela tulizositisha, za kuwapandisha madaraja na kuwaongezea mishahara wafanyakazi, hazitoshi!
 
Tunazihitaji sana hizo hela za mafisadi ili tuendelezee ujenzi wa standard gauge na stiglers gorge! Hela tulizositisha, za kuwapandisha madaraja na kuwaongezea mishahara wafanyakazi, hazitoshi!
Yaani mtu mmeshindwa kuthibitisha mahakamaani kosa lake la kuhujumu uchumi kwa zaidi ya miaka 3,
Halafu unamwambia akiri kosa na alipe fedha.ili aachiwe.
huu ni uonevu uliopitiliza na hakuna mahabusu atakayekubaliana na huu upumbavu
 
Wapinzani ni watu makatili Sana. Mahakama ya ufisadi sii sehemu isiyo na uhuruma. NI sehemu ya kutoa haki
 
Zamunda, The Banana republic with kangaroo courts!
 
Mahakama ya Ufisadi ilianza rasmi ikiwa ni jitihada za serikali ya awamu ya 5 kupambana na ufisadi nchini. Uazishwaji wa mahakama husika, uliambatana na uwepo wa kesi nyingi za uhujumu uchumi ikiwa ni uwepo wa wateja wa mahakama hiyo.

Wingi wa kesi hizo zikiwa bado katika hatua za mwanzo mahakamani Kisutu, jana limekuja wazo la kushauri uwezekano wa kusamehe watuhumiwa iwapo wataungama makosa na kuwepo uwezekano wa kulipa fedha kulingana na kiwango cha ufisadi.

Magwiji wa sheria naombeni mtujuze juu ya uwepo wa mahakama ya ufisadi iwapo kila mtuhumiwa ataamua kuungama na kuahidi kulipa kiasi cha fedha aliyofisadi.

Hakujawahi kuwa na vita vya ufisadi nchi hii hasa awamu hii ya tano zaidi ya kupambana na matumizi ya neno fisadi. Na vita vya ufisadi hupiganwa kwa sheria na sio mahubiri ya kusaka kiki kwenye majukwaa ya kisiasa.
 
Back
Top Bottom