Mahakama ya Temeke wanasumbua kulipa pesa za Mirathi bila hoja za msingi

Mahakama ya Temeke wanasumbua kulipa pesa za Mirathi bila hoja za msingi

Hilo linajulikana.

Ndio maana nimeleta humu ili na wengine wajue mahakama zilivyo sehemu za ovyo
Kesi yako iko mahakama ya Wilaya au ilianzia mahakama ya Mwanzo? Unaweza kufika kwa hakimu Mfawidhi hapo mahakama ya Wilaya na ukamweleza malalamiko yako. Pia unaweza kufika mahakam ya Rufaa kitengo cha mirathi unawambia concern yako. Wao wanaweza kukuelekeza namna ya kufikisha malalamiko yako
 
Very sad, wengi wao wanaotoa ushauri hapa wanashauri utoe rushwa!
 
Umetisha mkuu.mganga mwenyewe tapeli nae anataka malipo
We endelea kusikiliza hao waganga wa instagram ila usiniulize mganga mzur utampata wapi maana sifanyi promo za waganga mimi

Njia za kupata hela ni 2
~Karoge
~Toa rushwa

Kazi kwako
 
Mkuu, Naomba kukuuliza kama nakala ya hukumu ya mirathi mlishapewa?

Kama malipo yote ya marehemu yalishaingizwa kwenye account ya mahakama, Na kama ni kweli wategemezi mlifata taratibu zote ikiwemo kujaza vendor form, Basi tatizo lipo kwa Muhasibu wa mahakama.

Kinachokosekana ni uwazi wa kupewa taarifa, Mimi ni Muhasibu wa mahakama pia Kuna taratibu za kiofisi ambazo lazima ziwe kwa maandishi,mfano pesa zikishaingizwa Judiciary Mirathi Account lazima ziwe approved kutoka makao makuu then mh hakimu aidhinishe malipo ndo mlipwe sio kitu Cha siku moja ni process kidogo.

Ninachokiona ni ww kuwa na jazba au kutokupewa taarifa kamili na hao wahusika. Kwa situation uliyofikia haikupaswa uwe mtu wa hasira jitahidi kumfanya uyo Muhasibu kuwa rafiki ili akupe taarifa sahihi kwa wakati. Jishushe ongea nao kirafiki uone kama hawatokuhudumia vizuri.

Kama imeshindikana unaweza pia kuwasilisha malalamiko yako kwa msajili wa mahakama au hakimu husika kwa hatua zaidi. Kumbuka malalamiko yawe kwa njia ya maandishi sio mdomo.

Mahakama ya Tanzania kwa sasa imejitahidi kufanya maboresho hasa wakati huu ambao huduma zote zitahamia kwenye mfumo wa tehama.

Ni vyema ukawepo hapo mahakamani siku ya kilele Cha wiki ya sheria jumanne ya tar 2 February ili utoe kero yako hapo hapo na utasikilizwa.
 
Kutoa rushwa ni kuondoa tatizo ama kuongeza tatizo.

Kiukweli wafanyakazi wa mahakama wanaifanya mahakama ionekane ni sehemu ya ovyo sana. Usumbufu mwingi sana
Hapo ndio utajua hujui kwa Tanzania eneo la mahakama rushwa imehalalishwa. Mfano karani anakuambia eti mheshimiwa hajanywa chai!! Hakuna msaada popote Nakushauri wape hela ya chai na maandazi tu wamalize shauri lako
 
Mkuu, Naomba kukuuliza kama nakala ya hukumu ya mirathi mlishapewa?

Kama malipo yote ya marehemu yalishaingizwa kwenye account ya mahakama, Na kama ni kweli wategemezi mlifata taratibu zote ikiwemo kujaza vendor form, Basi tatizo lipo kwa Muhasibu wa mahakama.

Kinachokosekana ni uwazi wa kupewa taarifa, Mimi ni Muhasibu wa mahakama pia Kuna taratibu za kiofisi ambazo lazima ziwe kwa maandishi,mfano pesa zikishaingizwa Judiciary Mirathi Account lazima ziwe approved kutoka makao makuu then mh hakimu aidhinishe malipo ndo mlipwe sio kitu Cha siku moja ni process kidogo.

Ninachokiona ni ww kuwa na jazba au kutokupewa taarifa kamili na hao wahusika. Kwa situation uliyofikia haikupaswa uwe mtu wa hasira jitahidi kumfanya uyo Muhasibu kuwa rafiki ili akupe taarifa sahihi kwa wakati. Jishushe ongea nao kirafiki uone kama hawatokuhudumia vizuri.

Kama imeshindikana unaweza pia kuwasilisha malalamiko yako kwa msajili wa mahakama au hakimu husika kwa hatua zaidi. Kumbuka malalamiko yawe kwa njia ya maandishi sio mdomo.

Mahakama ya Tanzania kwa sasa imejitahidi kufanya maboresho hasa wakati huu ambao huduma zote zitahamia kwenye mfumo wa tehama.

Ni vyema ukawepo hapo mahakamani siku ya kilele Cha wiki ya sheria jumanne ya tar 2 February ili utoe kero yako hapo hapo na utasikilizwa.

Nimekuelewa sana. Ukisoma vizuri uzi wangu nimeilalamikia idara ya uhasibu kwa majibu yao mepesi kama ya kusema mtu amepata msiba .

Nakala ya hukumu ipo, kila kitu kipo.

Hakuna sehemu nilipomlalamikia hakimu.

Nimelalamikia idara ya kulipa pesa tu.

Na hata ukisoma wachangiaji wengine na wao wamelalamika kwamba ni tabia ya wahasibu kutolipa mpaka wapewe pesa za rushwa.. wanaita push money.

Yaani mtu hapewi haki yake mpaka push money.

Why utumie zaidi ya miezi mitatu ama sita kumlipa mtu aliyekamilisha kila kitu kwa wakati. Mbona mahakimu hawana shida siku hizi
 
Nimekuelewa sana. Ukisoma vizuri uzi wangu nimeilalamikia idara ya uhasibu kwa majibu yao mepesi kama ya kusema mtu amepata msiba .

Nakala ya hukumu ipo, kila kitu kipo.

Hakuna sehemu nilipomlalamikia hakimu.

Nimelalamikia idara ya kulipa pesa tu.

Na hata ukisoma wachangiaji wengine na wao wamelalamika kwamba ni tabia ya wahasibu kutolipa mpaka wapewe pesa za rushwa.. wanaita push money.

Yaani mtu hapewi haki yake mpaka push money.

Why utumie zaidi ya miezi mitatu ama sita kumlipa mtu aliyekamilisha kila kitu kwa wakati. Mbona mahakimu hawana shida siku hizi
Ndo Mana nasema usiwe na jazba, Muhasibu hawezi kulipa kama anatoa pesa mfukoni mwake, Kuna taratibu za malipo.

Unachotakiwa ni kujenga ukaribu nae ili awe anakupa taarifa sahihi za hatua alizofikia.

Sio kwamba anahitaji rushwa, Hapana isipokuwa mazingira na taratibu za kazi wakati mwingine inaonekana kama muhusika anahitaji rushwa wakati si kweli.
 
Ndo Mana nasema usiwe na jazba, Muhasibu hawezi kulipa kama anatoa pesa mfukoni mwake, Kuna taratibu za malipo.

Unachotakiwa ni kujenga ukaribu nae ili awe anakupa taarifa sahihi za hatua alizofikia.

Sio kwamba anahitaji rushwa, Hapana isipokuwa mazingira na taratibu za kazi wakati mwingine inaonekana kama muhusika anahitaji rushwa wakati si kweli.

Ukaribu gani out of proffessionalism. Mbona mahakimu na wengineo waliohusika huko nyuma hawakutaka ukaribu.

Kwenye kazi ama proffessionalism mahusiano yanatakiwa yawe ya kikazi tu. Sio nje ya kazi

Nakuja ofisini kwako unaniambia taratibu zako na vinavyohitajika.

Mimi mteja nakupa vinavyohitajika na wewe unagonga unanigongea proof of delivery na date yake uliyo receive. Nakuuliza kinachofata nini. Unanijibu kasubiri baada ya wiki 6 hela itaingizwa kwenye account uliyoijaza pamoja na vendor form.

Wiki 6 zinapita hela haijaingia. Narudi ofisini kwako nakuuliza kwa nini hela haijaingia na umeniambia wiki 6. Unanijibu vumilia nakubali. Navumilia tena miezi 3 mbele bado hulipi

Nikija nakuuliza why unasema staff ana msiba ama yupo likizo, je mtu akipata msiba ndio kazi zinasimama miezi mitatu mbele. Hapo nikuelewe vipi hata ungekuwa wewe
 
Mahakama ya wilaya ya temeke ina wafanyakazi wa ajabu sana.

Tumekamilisha taratibu zote za mirathi za mzee wetu.

Bank alizokuwa anatumia marehemu, mifuko ya hifadhi ya jamii psssf na mobile money zote zimetuma pesa kwenda kwenye account ya mahakama toka october 2021

Barua ya mchanganuo wa mgao wa mirathi imepelekwa toka November mwanzoni. Na taratibu zote za zikafanyika kama kujaza vendor form na nyaraka za kibenk za warithi wa marehemu.

Ila mpaka leo mahakama haijawalipa hao warithi.

Msimamizi wa mirathi akienda kufatilia anaambiwa subiri. Kuna wafanyakazi wa idara ya uhasibu wamepatwa na msiba wa wazazi wao. Ukaguzi bado hawajaumaliza.

Siku nyingine wakienda wanaambiwa December kuna sikukuu nyingi sasa walipaji hawakuwa kazini.

Akienda kuulizia tena anaambiwa mlipaji ameenda likizo fupi.

Miezi zaidi ya miwili ni longo longo tu

Kweli mfanyakazi akipata msiba na ofisi yake mahakamani inasimama kufanya kazi zake mpaka arudi ?
Kama vipi tengenezeni mazingira ya kuwalipua,maana hapo wanachotaka ni rushwa tu hakuna jipya.
 
Kama vipi tengenezeni mazingira ya kuwalipua,maana hapo wanachotaka ni rushwa tu hakuna jipya.

Msimamiz wa mirathi ametoa 2 weeks za ziada Wasipolipa tunampanga jamaa yetu wa takukuru yeye atatulekeza cha kufanya ili liwe fundisho
 
Back
Top Bottom