Mahakama yaridhia kunyongwa aliyemuua Dereva Bodaboda

Mahakama yaridhia kunyongwa aliyemuua Dereva Bodaboda

Kwahiyo Jamaa amehukumiwa kifo kwa sababu tu alikamwatwa na Pikipiki aliyokuwa anaendesha Marehemu?

Kwamba ameua wamethibitishaje sasa?
Sasa mbona ameshindwa kujitetea, amepataje pikipiki ya marehemu, kama ameikota, alitangaza wapi, kama aliletewa, na akina nani, mshikwa na ngozi.....
 
Yan Leo pikipiki ipotee kesho ukutwe nayo wewe, mnataka kusema nin nyie huko juu mnaotetea, huyu ni muuaji,kama sio basi kahusika na anawajua wauaji awataje wakapumzike wote huko.

Nyumban kwetu sisi ni njian kuna siku usiku tunakula tukawatunasikia watu wanabishana hiv ila tunasikia kwa mbali yan tunakuja kushtuka yule boda anapiga kelele za msaada tunafika pale kashakatwa katwaapanga, kichwan, mabegan na mikononi, wezi wabayaa saaana
Kosa ni aliloshitakiwa nalo ni mauaji ya kukusudia na amepatikana hatia ya mauaji, eti wamfunge miezi sita, wakati yeye amepoteza maisha ya mtu, kwa kitu chenye thamani Tsh. 2,000,000.
 
Usiseme hivyo kwa kua hayajakukuta, watu wanaua na wanakwenda Bank wanachukua Mali za Marehemu bila hata ya uwoga na kujimilikisha!!
Kwenye movie labda, ila kama ulishafiwa utaelewa ilivyo ngumu
 
Tumia akili hakuna muuaji aue kisha abaki na ushahidi, ataua ataiba na kwenda kuiuza pikipiki. Kwa nchi zilizoendelea kwa ushahidi huo tu, huyo jamaa angekutwa na hatia tofauti, sio ya mauwaji.
AMLETE HUYO ALIEMUUZIA PIKIPIKI.
 
Usiseme hivyo kwa kua hayajakukuta, watu wanaua na wanakwenda Bank wanachukua Mali za Marehemu bila hata ya uwoga na kujimilikisha!!
Hiyo ni next level crime , mwizi wa boda boda na kuuwa haezi kuwa na inteligence hiyo
 
Kwa hiyo kutokana na maoni ya mtuhumiwa hiyo pikipiki aliyokutwa nayo haina mmiliki halari ?

Au alishushiwa toka Ahera na Malaika Michaeli?

Tunaomba documents za pikipiki kaka kimya.
Mi milioni mbili hata mwezi mmoja hazinitoshi.

Vijana nchi hii ina fulsa nyingi sana za kujikwa mua kiuchumi.
Uhalifu hauna mwisho mwema.
 
Muuaji hawezi UA, akachukua pikipiki afu kesho aiendeshe maeneo hayo hayo
Anaweza, bila shaka yoyote. Siyo wauaji wote wako smart. Pengine aliibadilisha kimuonekano akidhani hatagundulika. Na pia alikuwa na nafasi ya kuiambia mahakama ameipataje.
 
Sasa mtu ameuawa halafu kesho unapatikana na vifaa vyake kwanini usijibu kesi. Maana kwa vyovyote mrufani anajuwa nini kilifanyika.
 
Mbona umejichanganya?

Unasema wewe siyo mtaalamu wa sheria, lakini hapo hapo unasema “kesi kubwa huwa inameza kesi ndogo”

Lakini hapo hapo unataka kesi ndogo(ushahidi wa kukutwa na pikipiki), ndiyo itumike kutoa hukumu ya kesi kubwa(mauwaji)?

Kama kukutwa na pikipiki ni kesi ndogo, kwanini itumike kutoa hukumu ya mauwaji ambayo ndo kesi kubwa kwa mujibu wa maelezo yako?
Kajichanganya [emoji2]
 
Kuna mapungufu katika hii taarifa. Mleta taarifa Kuna mambo ya msingi hajaandika.
 
Kwenye movie labda, ila kama ulishafiwa utaelewa ilivyo ngumu
Inakua ngumu kwako wwe mfiwa,kwa wahalifu inakua rahisi sana maana mchongo mzima umeshwa chorwa hadi ndani ya system ya Bank!!
 
Inapotea vizuri tu, we jichanganye ndo utajua hujui
Mkuu; Iko hivi, Kama marehemu aliipata pikipiki hiyo kihalali (kwa jasho lake) huyo aliyemdhulumu pikipiki na Uhai (Kumuua)wake HAKIKA damu hiyo iliyomwagika bila hatia na ardhi ikafunua kinywa chake kuipokea, itamlilia muuaji huyo daima.
Ukweli mm sithubutu hata kidogo kujihusisha na mambo ya dhulma kwenye mali za watu. Bora nibaki tu kama nilivyo.
 
Ndio, lakini kwanini mtuhumiwa akomalie Kama akijua sio mmiliki?.
Yeah. Yani mtuhumiwa angeliweka wazi jinsi ilivokuwa hadi pikipiki hiyo ikawa iko mikononi mwake. Tatizo hapo linawea kuwa ni UJINGA Uliokubuhu kwamba anawaficha (Anawalinda) wale (kama wapo)waliompatia hiyo pikipiki kwa mtindo wa kumwazimisha au kuijaribu (test) ili ainunue au aendeshe kama bodaboda au waliomwomba aitunze hapo kwake lakini awe anaipasha-pasha hadi watakaporudi wenyewe kuichukua n.k. Hakujua kwamba kwa kufanya hivyo anajipalia mkaa yy mwenyewe. Sasa imekula kwake mazima i.e. hata parole haitamhusu.
 
Yeah. Yani mtuhumiwa angeliweka wazi jinsi ilivokuwa hadi pikipiki hiyo ikawa iko mikononi mwake. Tatizo hapo linawea kuwa ni UJINGA Uliokubuhu kwamba anawaficha (Anawalinda) wale (kama wapo)waliompatia hiyo pikipiki kwa mtindo wa kumwazimisha au kuijaribu (test) ili ainunue au aendeshe kama bodaboda au waliomwomba aitunze hapo kwake lakini awe anaipasha-pasha hadi watakaporudi wenyewe kuichukua n.k. Hakujua kwamba kwa kufanya hivyo anajipalia mkaa yy mwenyewe. Sasa imekula kwake mazima i.e. hata parole haitamhusu.
Angewataja tu kama wangemkatalia polisi wangechunguza na kuwapata wauaji.
Kumbuka kwenye tukio la mauaji lazima kuna alama zinaachwa kama alama za vidole, damu, mawasiliano nk.

Unawezaje kuwalinda wauaji ilhali wapo na ukubali kunyongwe wewe usio na hatia ?

Mimi naona kati ya wauaji mtuhumiwa anahusika, hivyo anaona ni bora aubebe msalaba peke yake kuliko kuwataja na washirika wenzake.

Kwani ashindwe kueleza alikoipata pikipiki ?
Ambayo kashikwa mayo ikiwa chini ya umiliki wake ?

Tena alishindwa hata kuikana kwamba sio yake. Inaonekana walimkuta nayo ana kwa ana mkononi mwake.

Na huenda waliomtambua walimchoma kiasi cha kumkamata ready handled hata kuikana haikuwezekana.
 
Hakuna mtu anaeua afu kesho akaendelea kua hapo hapo, wengi hukimbia mazingira huyu kesi sio yake kilichomponza ni bodaboda aelezee alipoitoa kinachombana kuonekana yeye ndio mhusika ni hio bodaboda, angeeleza vizuri bodaboda imekuaje akawa nayo yeye na sio yake
Ndio; Wengi hukimbia ina maana sio wote hukimbia. Wapo wanaoendelea kuwapo (kubana) hapo hapo eti wanasikizia upepo unaendaje na Huyu ni mmojawapo. Yani atasemaje kwa mfano ameiokota? kama kaokota mbona hakutangaza au kutoa taarifa badala yake anapiga nayo misele? Umauti ulikuwa unamwita huyo.
 
Ndio; Wengi hukimbia ina maana sio wote hukimbia. Wapo wanaoendelea kuwapo (kubana) hapo hapo eti wanasikizia upepo unaendaje na Huyu ni mmojawapo. Yani atasemaje kwa mfano ameiokota? kama kaokota mbona hakutangaza au kutoa taarifa badala yake anapiga nayo misele? Umauti ulikuwa unamwita huyo.
Ndio hivyo na yeye wananchi wenye hasira wangemshtukia angekua kashapigwa petrol zamani,
 
Kwahiyo Jamaa amehukumiwa kifo kwa sababu tu alikamwatwa na Pikipiki aliyokuwa anaendesha Marehemu?

Kwamba ameua wamethibitishaje sasa?
Ingawa hatujui details za hiyo kesi lakini ni hatari sana kukutwa na mali ya mtu ambaye ameuwawa. Yaani ujipange kweli kweli kupangua hoja...
 
Pikipiki aibe leo kwa kumuua mtu halafu kesho atembee nayo mitaani ! Hii nayo imekaa sawa?, ni mwizi gani anaweza kufanya kosa la namna hiyo?
Si kwamba natetea , mimi ni mhanga wa ujambazi wa kikatili ambao umenisababishia ulemavu hadi leo hii, lakini pia namna watuhumiwa wanavyokamatwa inatakiwa iwe safi ili tufurahie hukumu,
Hakika. Yako.
 
Back
Top Bottom