Mahakama yazuia ubunge wa Halima Mdee na wenzake 18 kuguswa kuanzia leo Juni 27, 2022

Mahakama yazuia ubunge wa Halima Mdee na wenzake 18 kuguswa kuanzia leo Juni 27, 2022

Tuliwaambia mkatutukana hafukuzwi mtu CHADEMA na hafukuziki ovyo!!!!
KUNA MAANA FULAN KUWA PALE BUNGENI NA MKUU WENU ANAJUA FIKA ….

Kama hajui wawafungulie kesi ya kufoji saini ya Mnyika!

Wajinga ndo waliwao , kaeni kushabikia msiyoyajua!!


Nasikia CHADEMA ngazi za chini wamemwangukia KINANA asaidie Bahati nzuri Memo nimeipata! Who is KINANA then ? You are jocking
Cc Evarist Chahali
Britanicca
britanicca mbona unaandika kama kwamba hii ni mara ya kwanza kwa mbunge/wabunge au wanachama influential wa CHADEMA kufukuzwa na chama lakini watawala wakang'ang'ana/wakakumbatia kwa mbinu hizi hizi za kimahakama hadi wakamaliza muda wao wa ubunge..?

Unajaribu kuwataka watu wamlaumu nani? Mwenyekiti Freeman Mbowe? Katibu John Mnyika?

Sikiliza bwana.

Hakuna cha wajinga ndiyo waliwao wala nini. The main issue hapa ni kuelewa tu namna ya kucheza siasa za hawa maCCM..

Kinachowabeba CHADEMA kwa miaka yote kuendelea kuishi na kuwa wapinzani wakuu na tishio la utawala wa CCM ni uongozi dhabiti wa CHADEMA chini ya mwamba Freeman Aikael Mbowe..!!

Huyu mwamba angekuwa ni mtu wa tamaa na njaa kali na kwa siasa za nchi masikini za ki - Afrika na Bongo hii zilizojaa rushwa na hongo, basi ni wazi kuwa CHADEMA ingeshakwenda kibri iliko CUF na NCCR Mageuzi sasa..!

Ukitaka kucheza michezo ya maCCM, wekeza ktk kuijua mikakati yao (know your enemy)..

Ukifanikiwa kwenye hili utakuwa one step ahead of them. CHADEMA kwa hili, wamefanikiwa sana. Ushahidi ni hili linaloendelea sasa..

CCM hawaelewi watoke vipi. Wameishiwa mikakati halali ya kisiasa. Option yao sasa ni kutumia pyuuu pyuuu a.k.a bunduki kuua, kujeruhi, kuteka na kupoteza kama ilivyokuwa kwa TL...

Ndugu, hawa watu wako tayari kumtumia mwanachama yeyote wa CHADEMA na hasa akiwa mbunge na ana maslahi kwao na serikali yao kutumika kama nyundo 🔨🔨🔨 ya kuigongea CHADEMA.....

Hawa kina Halima Mdee na wenzake ni nyundo yao. Wanavizia kukosea kwa CHADEMA kwenye hili ili waitumie. Lakini bahati njema, wenzao CHADEMA ni werevu zaidi ya maCCM...

Ni ubabe na kuvunja sheria na katiba mbele kwa mbele. Ndo kusema, kwa hawa kinamama, hata CHADEMA wafuate sheria na taratibu zote za kinidhamu za kichama, hawataweza kumfanya lolote...

Rejea sakata la Zito Zubeiry Ruyagwa Kabwe na wengine..

Kilichopo na kinachoweza kufanyika kwa sasa, ni CHADEMA kuendelea kucheza kimkakati zaidi kwa kuzielewa mbinu zote za adui yao. Na kwa hili, CHADEMA wako kwenye mstari sahihi wa ushindi..

Mpaka hapo CCM hawana lolote. They are just a group of hooligans and power mongers by all means necessary...

Kwa sasa, you can easily predict the next line of CCM's political strategy..

Na kwa maoni yangu, wameshawaweza na kuwadhibiti na ofcoz wameshawalemea vya kutosha. Wanapumulia machine hawa na ndiyo maana wakati mwingine wana - opt kutumia nguvu za kipolisi na kijeshi kudhibiti wapinzani wao kisiasa hususani CHADEMA..

Mbinu hii huwa ni ishara ya mwisho ya uhai wa uwepo wa chama chochote cha siasa..

Ndiyo maana nayo ni kama njia inayo prove failures every day...

Mimi nawatia moyo CHADEMA. Songeni mbele. Your time to reign is just ahead of you...!
 
Hili suala la hawa wanawake 19 mpaka sasa limeshaonesha CCM hawako serious kwenye main issues za nchi yetu.

Chadema wanapoteza muda, na rasilimali fedha, kuendelea kufuatilia kesi ambayo kimsingi dalili zote zimeshaonesha kuna mchezo mchafu unaochezwa na CCM na idara zake.

Watanzania wameshaona nia ovu ya CCM kwenye hili, Chadema wajitoe huko wawaache CCM waendelee na watu wao, na Mbowe aondoke kwenye yale maigizo ya maridhiano, vinginevyo kubaki kwenye maridhiano katikati ya hali hii ni kujiaibisha.
CCM inahusikaje?
 
..Nashauri Cdm wasusie hii kesi.

..Kuendelea nayo kunaipa uhalali.

..Ni kuendekeza upuuzi tu.
LOoo, hapana mkuu. Kupuuzia ni kususia, kuzira.

Hakuna chochote cha maana kitokanacho na kufanya hivyo.

Acha iendelee hata kama ni maigizo watu watayaona wenyewe.

Hii ni sehemu muhimu ya ushahidi wa utawala usiofuata sheria.

CHADEMA ni lazima wakomae na huu upuuzi hivyohivyo.
 
Kilichopo na kinachoweza kufanyika kwa sasa, ni CHADEMA kuendelea kucheza kimkakati zaidi kwa kuzielewa mbinu zote za adui yao...

Na kwa maoni yangu, wameweza na wameshawalemea vya kutosha na ndiyo maana wakati mwingine wana - opt kutumia nguvu kujaribu kuwadhibiti hawa CHADEMA ambayo nayo ni kama njia iliyokwisha shindwa spectacularly...
Umeeleza vizuri sana, nami naungana nawe katika ufafanuzi wako uliouweka hapa.

Ila naomba tu CHADEMA waelewe kwamba mbinu huko CCM sasa zimebadilika.

Badala ya kuwapa shurubu mbalimbali, sasa wanapewa mipozo ya kila aina huku wakiendelea kulegezwa. Mbinu hizi ni 'lethal' zaidi ya zile zilizotumika huko nyuma.

Mwisho wasipojitambua watajikuta wamekwisha.
 
Tuliwaambia mkatutukana hafukuzwi mtu CHADEMA na hafukuziki ovyo!!!!
KUNA MAANA FULAN KUWA PALE BUNGENI NA MKUU WENU ANAJUA FIKA ….

Kama hajui wawafungulie kesi ya kufoji saini ya Mnyika!

Wajinga ndo waliwao , kaeni kushabikia msiyoyajua!!


Nasikia CHADEMA ngazi za chini wamemwangukia KINANA asaidie Bahati nzuri Memo nimeipata! Who is KINANA then ? You are jocking
Cc Evarist Chahali
Britanicca
We naye umezidi kiherehere, si heri sasa ubebe mimba uzae?
 
Hili suala la hawa wanawake 19 mpaka sasa limeshaonesha CCM hawako serious kwenye main issues za nchi yetu.

Chadema wanapoteza muda, na rasilimali fedha, kuendelea kufuatilia kesi ambayo kimsingi dalili zote zimeshaonesha kuna mchezo mchafu unaochezwa na CCM na idara zake.

Watanzania wameshaona nia ovu ya CCM kwenye hili, Chadema wajitoe huko wawaache CCM waendelee na watu wao, na Mbowe aondoke kwenye yale maigizo ya maridhiano, vinginevyo kubaki kwenye maridhiano katikati ya hali hii ni kujiaibisha.
Mkuu 'denooJ', hii ndiyo nafasi/fursa nzuri kabisa kwa CHADEMA, hasa wale wasioamini uigizaji unaoendelea chini ya Samia huku akiimba nyimbo za maridhiano/maafikiano.

Utamjuaje mtu unayetafuta maridhiano naye kama siyo kwa mambo kama haya?

Acha Mbowe na wenzake wajionee ukweli wenyewe, halafu wajiridhishe kwamba watu wanaofanya nao maridhiano ni watu wa kuwaamini au hapana.

Acha CHADEMA wajiridhishe, halafu tuone watakavyoendelea na mchezo huu.
 
Mkuu 'denooJ', hii ndiyo nafasi/fursa nzuri kabisa kwa CHADEMA, hasa wale wasioamini uigizaji unaoendelea chini ya Samia huku akiimba nyimbo za maridhiano/maafikiano.

Utamjuaje mtu unayetafuta maridhiano naye kama siyo kwa mambo kama haya?

Acha Mbowe na wenzake wajionee ukweli wenyewe, halafu wajiridhishe kwamba watu wanaofanya nao maridhiano ni watu wa kuwaamini au hapana.

Acha CHADEMA wajiridhishe, halafu tuone watakavyoendelea na mchezo huu.
Saccos kutafuta maridhiano na walamba asali ni usanii tupu. Ni vile tu Iq za kina faru John ni ndogo, walipaswa kuwa na maono ya mbali kujua wanauzwa hata kabla ya mdana wenyewe.
 
Nawapongeza kina mama shupavu 19 kupambania haki yao. Naipongeza mahakama kusimama kwenye haki. Spika kijana Tulia nae pia siwezi acha kumpongeza.
 
Ilifikia hatua hii naonna kabisa mambo ya katiba mpya ni kupoteza fedha za wananchi (sorry to say this). Ikiwa katiba hii tuliyonayo inaeleza wazi kuwa mbunge lazima awe na chama lakini haifuatwi. Hakina Mdee hawana chama na bado ni wabunge and nothing we can bado wanaendelea kufuja kodi zetu pasipo halali. Sasa hiyo katiba mpya ikija nani ataisimamia? Hawahawa wanaoikanyaga ya sasa au tutakodi Mabeberu waje waisimamie?
 

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo Jumatatu Juni 27, 2022 imetoa zuio la muda la kutofanyika chochote kwenye Ubunge wa Halima Mdee na wenzake 18 mpaka pale itakaposikiliza maombi ya rufaa yao.

Chanzo: MwanaHalisi


===========


Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo Jumatatu Juni 27, 2022 imetoa zuio la muda kuhusu kutofanyika chochote kwenye Ubunge wa Halima Mdee na wenzake 18 mpaka pale Mahakama hiyo itakaposikiliza maombi ya Rufaa yao.

Hatua hiyo imekuja baada ya CHADEMA kupitia kwa mawakili wake akiwemo Peter Kibatala, kuwasilisha pingamizi la awali wakipinga maombi mapya ya akina Mdee dhidi yao ambapo wanaiomba mahakama hiyo iwape kibali cha kufungua kesi ya kupinga kuvuliwa uanachama wa chama hicho.


Mdee na wenzake wamefungua maombi Mahakama Kuu dhidi ya Bodi ya Wadhamini wa Chadema (iliyosajiliwa) wakiomba ridhaa ya kufungua shauri la kupinga kuvuliwa uanachama wa Chadema.

Sambamba na maombi hayo ya ridhaa namba 27 ya mwaka 2022, pia wamefungua maombi ya amri ya zuio dhidi ya NEC na Spika, kutochukua hatua dhidi ya uamuzi wa Chadema kuwavua uanachama.

Maombi hayo yaliyopangwa kusikilizwa na Jaji Mustapha Ismail yametajwa leo Jumatatu Juni 27,2022, ndipo mawakili wa Chadema wakaibua pingamizi, dhidi ya maombi hayo ya zuio.


Kama wewe ni Mtanzania halafu una unga mkono huu ujinga wa kugushi barua na serikali kulipa hawa wabunge na wewe ni tatizo la nchi hii. Sio kila kitu ni siasa inabidi ufike wakati sheria ziheshimiwe! Usije tena ukaanza kulalamika kuhusu maandamano kwamba hayafuati sheria wakati kuna wabunge kama hawa!

Mahakama wawe makini spika anajaribu kuwa twisha hili zigo ili tatizo liwe kwao na sio bungeni sasa wanapigiana mpira tu.

Kama mnafiki hii inawaharibia Chadema ni makosa makubwa sana hii inawapa mifano halisi Chadema na wananchi wanalijua hili. Support ya hawa covid 19 ni kwa CCM na sio wananchi
 
Saccos kutafuta maridhiano na walamba asali ni usanii tupu. Ni vile tu Iq za kina faru John ni ndogo, walipaswa kuwa na maono ya mbali kujua wanauzwa hata kabla ya mdana wenyewe.
Lakini ni hawa hawa waliihimiri mikikimikiki na dhoruba zilizowakumba huko nyuma hadi wakaifikisha 'saccos' yao hapa leo!

Usibeze, wape muda.
 
Tuliwaambia mkatutukana hafukuzwi mtu CHADEMA na hafukuziki ovyo!!!!
KUNA MAANA FULAN KUWA PALE BUNGENI NA MKUU WENU ANAJUA FIKA ….

Kama hajui wawafungulie kesi ya kufoji saini ya Mnyika!

Wajinga ndo waliwao , kaeni kushabikia msiyoyajua!!


Nasikia CHADEMA ngazi za chini wamemwangukia KINANA asaidie Bahati nzuri Memo nimeipata! Who is KINANA then ? You are jocking
Cc Evarist Chahali
Britanicca
Wewe acha porojo kila kitu leo kinajulikana nani mratibu na nani msimamizi lakini mwisho wa yote kila jambo lina mwisho wake kama mmewafadhili ili mkopesheke shauri yenu,upumbavu huu kwa kweli mtaujutia ninyi ccm pamoja na hao covid 19.
 
TUMECHOKA KUSIKILIZA UZEMBE HUU KILA WAKATI .WAKAE NAO BUNGENI DAIMA.MAISHA YATUFIKIRISHE NA UZEMBE!.BOWE NA VIONGOZI WENZAKE HAWATOKI HADHARANI KUFAFANUWA LOLOTE WAMEZIDIWA JANJA.
Hawajazidiwa ujanja ila mratibu wa mipango hii ndiye mwenye ingekuwa wewe ungefanyaje?
 
Tuliwaambia mkatutukana hafukuzwi mtu CHADEMA na hafukuziki ovyo!!!!
KUNA MAANA FULAN KUWA PALE BUNGENI NA MKUU WENU ANAJUA FIKA ….

Kama hajui wawafungulie kesi ya kufoji saini ya Mnyika!

Wajinga ndo waliwao , kaeni kushabikia msiyoyajua!!


Nasikia CHADEMA ngazi za chini wamemwangukia KINANA asaidie Bahati nzuri Memo nimeipata! Who is KINANA then ? You are jocking
Cc Evarist Chahali
Britanicca
Hawa watu wakiambiwaga fact wanatukana matusi tu ndio eanachojua.
Wanaambiwa kilasiku humu DJ anajua mchoro A to Z hawaelewi wana kaza mafuvu tu.
Muda ni msemakweli namba moja.
 
Tuliwaambia mkatutukana hafukuzwi mtu CHADEMA na hafukuziki ovyo!!!!
KUNA MAANA FULAN KUWA PALE BUNGENI NA MKUU WENU ANAJUA FIKA ….

Kama hajui wawafungulie kesi ya kufoji saini ya Mnyika!

Wajinga ndo waliwao , kaeni kushabikia msiyoyajua!!


Nasikia CHADEMA ngazi za chini wamemwangukia KINANA asaidie Bahati nzuri Memo nimeipata! Who is KINANA then ? You are jocking
Cc Evarist Chahali
Britanicca
We Ni mwongo mara nyingi habari zako Ni za kutunga. Weka hapa hiyo memo kuthibitisha uongo wako.
 
Back
Top Bottom