Mahakama yazuia Vijiji vya Ngorongoro Kufutwa
Jaji Wewe Hii Bhaghoha Sana
MMashughuli Gete Gete
 
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imesimamisha utekelezaji wa amri iliyokuwa imetolewa na Serikali kupitia tangazo la Serikali namba 673 ya 2024 la kufuta vijiji, kata na vitongoji pamoja na kusitisha tangazo la kuwataka Wananchi kuhama katika Wilaya la Ngorongoro.

Umuamuzi huo umetolewa leo August 22,2024 mbele ya Jaji Mwenda wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha katika kesi namba 59630 ya mwaka 2024 kufuatia maombi yaliyopelekwa Mahakamani na Mpeleka maombi Isaya Ole Posi ya kuiomba ipime na kutazama kama amri ile ilikuwa halali au la hasha au kama ilitolewa na Mtu mwenye Mamlaka ya kisheria kufanya hivyo.

Wakili wa kujitegemea Peter Njau akimuwakilisha Mteja wake Isaya Ole posi amesema Mteja wake alikuwa Mwathirika wa kuondolewa katika eneo hilo jambo ambalo aliamua kwenda Mahakamani kupinga kitendo hicho.

MBWA WAMEANZA KUBWEKA

View attachment 3076651
Tatizo wengi bado hamjui siasa za manipulation nchi za Africa, sasa muwe tayari kupokea hukumu ya rufaa ya serkali kwenye kesi hiyo hiyo,.......hapo serikali inatafuta official recognition ya mahakama zoezi liko pale pale.
 
Kwa mahakama za Tanzania kesi zote zinazoihusu serekali,serekali haijawahi kushindwa hata siku moja,hukumu ya kwanza inaweza ikashindwa,kwenye rufaa inashinda kwa kutumia wale majaji ambao kwenye uchaguzi utasikia wanagombea nafasi mbalimbali kupitia chama cha CCM.
 
26 September 2024 tunaona ujeuri wa Serikali kufika mahakamani kutetea tangazo lake haramu la tarehe 02 Agosti 2024 katika gazeti la serikali lililotolewa na waziri wa TAMISEMI kufukuza wakaazi wa Ngorongoro ingawa waziri hana mamlaka na siyo sahihi kutoa amri kuwahamisha


TOKA MAKTABA :

Serikali yafuta vijiji na vitongoji vyote vya wamasai wa Ngorongoro kupitia Amri ya tangazo la Serikali namba 673​


AMRI YA MAREKEBISHO YA AMRI YA MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA KATIKA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA WILAYA) YA MWAKA 2024

1. Amri hii itajulikana kama Amri ya Marekebisho ya Amri ya Mgawanyo wa Maeneo ya Utawala katika Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) ya Mwaka 2024 na itasomwa pamoja na Amri ya Mgawanyo wa Maeneo ya Utawala katika Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) ya Mwaka 2019 ambayo hapa imerejewa kama "Amri kuu".

2. Amri kuu inarekebishwa katika Jedwali kwa kufuta kata, vijiji na vitongoji katika Halmashauri za Wilaya ya Ngorongoro, Bahi, Chemba, Kasulu, Kakonko, Hai na Rombo kama ilivyoainishwa katika Jedwali.

Hili ni Tangazo la Serikali namba 673 la Agosti 2, 2024.

Kwa mujibu wa tangazo hili, vitongoji 96 na vijiji 25 vya Ngorongoro vimefutwa.
 
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imesimamisha utekelezaji wa amri iliyokuwa imetolewa na Serikali kupitia tangazo la Serikali namba 673 ya 2024 la kufuta vijiji, kata na vitongoji pamoja na kusitisha tangazo la kuwataka Wananchi kuhama katika Wilaya la Ngorongoro.

Umuamuzi huo umetolewa leo August 22,2024 mbele ya Jaji Mwenda wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha katika kesi namba 59630 ya mwaka 2024 kufuatia maombi yaliyopelekwa Mahakamani na Mpeleka maombi Isaya Ole Posi ya kuiomba ipime na kutazama kama amri ile ilikuwa halali au la hasha au kama ilitolewa na Mtu mwenye Mamlaka ya kisheria kufanya hivyo.

Wakili wa kujitegemea Peter Njau akimuwakilisha Mteja wake Isaya Ole posi amesema Mteja wake alikuwa Mwathirika wa kuondolewa katika eneo hilo jambo ambalo aliamua kwenda Mahakamani kupinga kitendo hicho.

MBWA WAMEANZA KUBWEKA

View attachment 3076651
Samia akimuweka mkwewe tamisemi ili aweze kufanikisha malengo yake batili
 
Back
Top Bottom