Maharage ana uwezo kweli kuendesha shirika la kitaalam kama TANESCO?

Hapo kwenye Magufuli aliwaza mbali umekosea. Kama Magufuli angekuwa na akili angeendeleza phase 3 & 4 za Kinyerezi.

Kwa sasa Kinyerezi 1 & 2 alizoziacha Jakaya Kikwette zina kidhi mahitaji ya umeme kwa 65% maana kila moja inazalisha 400MW.

Magufuli aliwajaza ujinga kwa kwenda kufufua mradi uliofanyiwa feasibility study mwaka 1978 wakati wa Nyerere. Hayo makaratasi yalikuwapo RUBADA ila kwa taarufa yako kati ya 1978 ilipofanywa feasibility study na 2017 Dikteta Magufuli alipolazimisha JNEHP Dam ijengwe maji ya mto Ruaha na Kilombero ambavyo ndivyo vinailisha Rufiji yalikuwa yamepungua kwa 40%. Sababu za upungufu ni mabadiliko ya tabia nchi na shughuli za kibinadamu along the river basin
 
Mkuu acha kupotosha facts.
Unaweza kuwa ni Maharage mwenyewe!
Kinyerezi I inatoa 150MW kama rated capacity na Kinyerezi II natoa 240 MW kama rated capacity.

Juu ya JNHPP, ambayo inategemewa kuzalisha 2115MW, kwa taarifa yako maji yamejaa kwenye Dam hata kabla ya wakati.
Tafuta useful information zikusaidie.
 
Sio kweli. Kinyerezi 1 ina 180MW na kinyerezi 2 ina 240 MW.

Mengine ya kwako sijasoma kwa sababu hayana maana kwa sababu umeanza ma uongo sina sababu ya kusoma uharo wako mwingine.
 
Kinyerezi haina hio capacity mzee
 
Thanks for correction mkuu
 
Inaweza kabisa Kuna theory imetengenezwa pindi umeme unapokatika watu Fulani wanapiga Hela huko tanesco
 
Moja ya mada iliyojadiliwa kwa nondo ni hii. Safi sana wanaJF.. nimesoma mwanzo hadi mwisho ni mwendo wa hoja tu. Naendelea kufuatilia
 
sio Maharage tu, shirika lolote linaloendeshwa na watanzania kwa 100% haliwezi kuwa na ufanisi.

Bado najiuliza ni lini Tanesco iliwahi kuwa na ufanisi? Vipi hapo TRC ufanisi ni % ngapi? Tazara, TPA, ATCL nk huko nako kuna mkurugenzi Maharage?

Watanzania tuna matatizo tu lazima hili tukubali, tunaweza kulaumu mtu mmojammoja lakini kimsingi wote tunashare matatizo yaleyale.

Tumefilisi NBC tukauza kwa kaburu, CRDB vilevile, TTCL imetushinda, tuliachiwa ATC tukaifilisi, Tipper tukaua, viwanda vya nguo mufirisi, mkoloni alituachia reli ikiwa operative nk vyote tumeua.

Nut kwenye vichwa vyetu vyote watanzania zimeregea, na hata ukikaza utazikata tu..
 
Watanzania haohao unaowakandya wakienda nje wanakua na mafanikio makubwa

Nadhani ungeangalia muundo wa taasisi zetu, tabia zetu towards our own people and uvivu uliokubuhu

Atc walikua na mtu anaitwa Dumisani Sangweni… msauzi na ilifia pale

Ungeacha unyani… upeo wako ungeongezeka
 
Usitake kujifananisha na wagonjwa kuhalalisha ugonjwa wako.
Direct question, mbona hali haikuwa hivi wakati wa Maguguli?
 

swali rahisi sana bado hujajibu, nionyeshe shirika moja la umma linaloendeshwa na watanzania 100% lenye ufanisi na la kuchukulia mfano.

Hapo umenipa mfano wa mtanzania mmoja anayekwenda kufanya kazi na WaUSA, WAFIN, WACAN nk.

Hata huyu Maharage kule DSTV alifanya vizuri bila shaka unajua DSTV alikuwa na akina nani, kaja TANESCO kwa manyani wenzake sana.
 
Usitake kujifananisha na wagonjwa kuhalalisha ugonjwa wako.
Direct question, mbona hali haikuwa hivi wakati wa Maguguli?

Kukatika umeme mbona kulikwepo tu kama kawaida? Tanesco kupata hasara mbona ilikuwa kama kawaida tu?.

Ndio maana nimeuliza lini Tanesco ilikuwa na ufanisi.?
 
Kukatika umeme mbona kulikwepo tu kama kawaida? Tanesco kupata hasara mbona ilikuwa kama kawaida tu?.

Ndio maana nimeuliza lini Tanesco ilikuwa na ufanisi.?
Inaelekea wewe ulikuwa nje ya nchi kwa muda mrefu.
Mgso mkali ulianza kupungua baada ya kujengwa Kinyerezi I na Kinyerezi II.
Wakati wa Awamu ya 5, Kinyerezi I ilikamilika 2016 na Kinyerezi II ilikamilika 2018.
Makali ya kukatika umeme yalipungua sana na mgawo ulikiwa si kama sasa.
Ufanisi kwa sisi wateja wa umeme ni kutokatika, na hapo huwa hatuna cha kusema.

Sasa leo Maharage atujibu, kilichobadilika nini?
 
Maharage! Jina lenyewe tu shida.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…