Maharage wa TANESCO atimuliwa kwenye kikao cha Waziri Mkuu Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu Biteko. Apewa siku tatu


Naheshimu mawazo yako japo sikubaliani nayo.
Unaposema "TANESCO iendelee kuwa state owned" unakuwa una hofu gani?

Ndio nazungumzia "Transmission" yaani waruhusu pia firms zizalishe na zifanye ugavi kuwepo na "Soko huria" kwenye umeme. Umeme ni bidhaa mzee na hakuna bidhaa itakosa mwekezaji kama inatoka.

Wabadiri sera ya nishati ya 2003 kuruhusu Private sector participation in electricity business na wasiingie katika ununuzi bali waruhusu firms zisambaze (Ugavi) wa umeme.

Ninachokiona kwako ni hufo tuu, watu wa telecoms wanatandika "Deploy" Optic fibre broadband 4000Km kupeleka huduma itakuwa nguzo na transformers!!

Usizunguke Umeme ni chanzo "kikubwa" cha mapato kwa nchi hii kwa hiyo wanaona ni bora tuteseke ila wapate mapato hayo ndio maana wamehodhi sekta hiyo. Hawajaipa kipaumbele huduma bali mapato.
 
Kunavitu havieleweki ambavyo Tanesco hawasemi ukweli..Juzi walisherehekea kwa kupata faida ya billion 100 kwa mara ya Kwanza baada yakuonfoa gharana zote za uebdehsaji.Wakasema SASA hakunashida ya umemee keani wanaziada ya 400MW hivyo hata maji yakikauka bado hizo mega watt 400 zinaondoa shida.Sasa tunajiuliza inekuwaje ndani ya mwezi mmoja hakuna umeme.Ndo maana Naharage lazima araumie SBB hakusema ukweli
 
Bila bwawa la Nyerere kuanza kazi hata aje nani wizara ya nishati lazima mgawo uendelee. 1605 MW kwa nchi kubwa kama hii yenye watu zaidi ya 60m hazitoshi.
 
Hakuna mtu anyeweza kukubali Maharage ahudhurie kikao hicho muhimu kuwaambia eti Tanzania hakuna mgao wa umeme bali kuna upungufu tu wa umeme. Eti mgao wa umeme hufanyika pale ambapo hatuna upungufu wa umeme. Na nonsense zingine. Sijui kwa nini wanasita kumhamishia TBC akasimamie ving'amuzi vya TBC kama alivyokuwa akifanya DSTV kwa ufanisi mkubwa.
 
Naheshimu mawazo yako japo sikubaliani nayo.
Unaposema "TANESCO iendelee kuwa state owned" unakuwa una hofu gani?
Naangalia waliojaribu kufanya na kilichotokea ni Desi ngoja nikupe mfano wa reli tuseme ubinafsishe reli sio zile trains bali na njia za train kupita; sababu tayari njia zipo huwezi kusema ujenge mpya kwahio kitakachotokea ni watu kushindanishwa tender anayeshinda kwa wakati miaka kadhaa anapewa targets asipofikisha anapigwa chini anachukuliwa mwingine na mwingine and the cycle continues sababu hio sekta sio rahisi kama vile ilivyo simu ambapo kila mtu anaweza akawa na vyanzo vyake minara yake n.k. (hata simu unaweza ukakuta wanakuwa forced kulipia miundombinu ya state na wenyewe kutoa huduma; Yaani Tier ISPs wanaununua jumla na kuuza na kuuzia wengine na wengine)

Kuhusu watu kufanya biashara huria ndio nimekuuliza umekatazwa kuja na solar yako, au hata wind farm na kuiuzia Tanesco au kama unaweza ukapaki Biogas efficiently ukaipelekea Tanesco at a cheaper price watakataa...; Issue yangu ni kugawana hizi assets ambazo tayari zipo na UMMA umazigharamikia kwa miaka nenda rudi leo wajanja waje wapewe on a silver platter (kama walivyobinafsisha NHC)
Ndio nazungumzia "Transmission" yaani waruhusu pia firms zizalishe na zifanye ugavi kuwepo na "Soko huria" kwenye umeme. Umeme ni bidhaa mzee na hakuna bidhaa itakosa mwekezaji kama inatoka.
Unajua kilichotokea USA kipindi cha Direct Current na kila mtu kuwa na misitimu yake na nyanya zake ?;

Au unadhani tukisema kila mtu awe na Bwawa lake la HEP is it feasible ?; Au nguzo na transformer kila mtu asimike yake kila kona?.

Ndio maana nikasema kuna njia za kuzalisha umeme efficiently hizo kila mtu aweze kuzalisha na kupelekea grid; na sehemu ambazo Tanesco hajafika na hakuna wateja wawekezaji waweze kwenda (ila economy of scale itakwambia hakuna mtu atataka kwenda huko ambapo profit ni ndogo na atataka achukue creme de la creme) na ukizingatia nishati ni Service mwisho wa siku mteja atakuwa shortchanged.....
Wabadiri sera ya nishati ya 2003 kuruhusu Private sector participation in electricity business na wasiingie katika ununuzi bali waruhusu firms zisambaze (Ugavi) wa umeme.
Nishakujibu hapo juu..... kitakachotea ambacho ni feasible na realistic ni private firms kuwa madalali yaani zitachukua umeme katika wazalishaji walewale na transmission zilezile kitakachofanyika ni wewe Bill yako itasoma amekupa nani Huduma ingawa huduma inatoka kule kule kwa wao kununua kwa jumla na kuuza kwa rejareja; na kila wakikaa na Waangalizi na kulalamika kwamba gharama ya uendeshaji imezidi bei itaongezwa kuwafidia ili wapate profit (Hio sio kwamba ninaitoa kwenye theory bali ndicho kinachotokea katika Prices za Gas kwa Watumiaji wa Europe (Bei zinakuwa inflated ili watu wapate their foreseeable profit)
Ninachokiona kwako ni hufo tuu, watu wa telecoms wanatandika "Deploy" Optic fibre broadband 4000Km kupeleka huduma itakuwa nguzo na transformers!!
Hivi ushaona cable tu za TV zinavyozagaa kama utitiri na watu kutokuzihudumia; just imagine umewekeza wire zako kupeleka nyumba kumi za mtaa wa nane alafu kesho wanahama kwa provider B au wanashindwa kuhama sababu provider B hafiki kwao ?

Ndio maana nikakwambia kitakachotokea ambacho ni feasible hakuna mtu atakayetandanza wire zake kila mahali (hata wakifanya safety haitakuwa guaranteed) kitakachofanyika hizo kampuni zitakuwa madalali au zinakodi njia za main provider ambaye kwa wingi wa pesa na nguvu atakuwa huyo huyo Tanesco..., That's why I have advised kwa yoyote who can generate power cheaply and efficiently private or otherwise aweze kuwauzia Tanesco na katika ushauri wangu sio kampuni tu hata wewe nyumbani kwako ukiwa na solar panels chache uweze kuwauzia Tanesco

Kipindi cha Direct current huko USA kulikuwa kila provider ana wire zake kutoka kwenye generator yake mpaka kwenye nyumba ya mtu (mfano wa cable) kilichotokea mandhari yote ulikuwa ukiangalia juu ni utitiri wa nyaya
Usizunguke Umeme ni chanzo "kikubwa" cha mapato kwa nchi hii kwa hiyo wanaona ni bora tuteseke ila wapate mapato hayo ndio maana wamehodhi sekta hiyo. Hawajaipa kipaumbele huduma bali mapato.
Umeme Nishati ni Nguzo muhimu katika taifa lolote, bila Nishati bora kila kitu kinasimama, hivyo basi Umeme haipaswi iwe chanzo cha mapato ya nchi (unless tunauza nje) umeme inabidi uwe kichocheo cha mapato ya nchi kwa kuhakikisha umeme ni wa uhakika na affordable ili viwanda na uzalishaji uwe wa gharama nafuu; Kuchaji watu pesa nyingi kwenye umeme ili upate mapato makubwa ni kama kujiibia kwenye mfuko wa suruali na kuweka mfuko wa shati
 
Nakubaliana na wewe, ingeruhusiwa hata watu kuwekeza kwenye min grids kwa level hata ya mkoa au wilaya.

Umeme ni bidhaa waruhusu soko huria kama telecoms industry maana washashindwa kuleta umeme wa uhakika miaka 60 toka uhuru
Kwa sasa hata ukiwa na solar panels unazalisha umeme wa ziada ambao unataka kuuza kwenye grid ya taifa huwezi.

Kwa sababu TANESCO ina monopoly kwenye kuzalisha umeme.

Halafu ukimueleza mtu kwamba monopoly hii ni mbaya haelewi.

Ndiyo maana nchi ina matatizo.

Wananchi wengi hata hawayaoni matatizo kama matatizo.

Wanatafuta mchawi tu, kufukuzana kazi na kukaripiana bila mkakati.

Tunaenda kujenga bwawa kubwa la umeme, la kutegemea mvua, wakati tuna tatizo la mvua na mabadiliko ya tabianchi.
 
Sidhani kama private companies hazipo zimekuwepo na kuna fursa kwa wanaotaka kuzalisha umeme na kuuzia kwenye sehemu ambazo umeme haujafika (kama alivyofanya mobisol) ingawa realistically bila economy of scale hailipi ndio maana mobisol alifeli na kuuza kampuni...., as wawekezaji kuwauzia Tanesco soma hapo chini:-


Kuhusu suala la kila mtu kuweza kuuzia Tanesco nimeliongelea kwenye huu uzi

Ila kuweza kufanikisha hilo itabidi Tanesco ku-invest in smart meters ambazo zinaweza kumpa mtu credit akizalisha zaidi....

In short this is a goldmine kutokana na vyanzo vyetu vingi Tanzania tukiitumia vizuri Tanesco itatutoa kimasomaso ila kikachotokea ni kuendelea kuipa Tanesco a Bad name waiuze alafu kwa mlango wa nyuma wainunue waendelee kulamba asali.... (with no change in efficiency)
 
Hiyo mikataba ilikuwa mikataba ya kazi au MoUs? Waliishia wapi? Sikuijua hiyo.

Ila nafikiri bado kuna ukiritimba kwenye hayo makampuni kuweza kuuza umeme.

Suluhisho lilikuwa hiyo habari ya wananchi kuuza umeme moja kwa moja kwenye grid, kuna siku Maharage Chande alihojiwa hili, inaonekana kuna technical issues kama ulivyosema.

Lakini pia, kimsingi TANESCO wanapata conflict of interest hapo wao wenyewe kusimamia ugavi wa umeme halafu wakawa wanashindana kwenye biashara.Yani ikitokea kitu kinaweza kuja kuchukua market share yao, unafikiri watakiruhusu? Halafu wao wapate wapi biashara?

Hapo inawezekana tukatakiwa kutenganisha anayesimamia ugavi wa umeme na wanaofanya biashara ya umeme ili kuondoa conflict of interest.

TANESCO imeondolewa majukumu ya kusimamia ugavi wa umeme? Hayo yangeachwa EWURA halafu TANESCO ifanye biashara tu.

Sikumbuki vizuri majukumu ya TANESCO kwa sasa yakoje, miaka ya kati hapa muundo umebadilishwa sana.
 
Ofcourse muundo / management inabidi ubadilike sasa hivi tatizo kubwa Tanesco ni Kibubu cha Serikali, wanachota pesa wanavyotaka hawalipi bili na kuanzisha miradi isiyo na tija na kupeana tender ili watu wapige pesa.... (am sure hata hizo Kampuni huenda wana share au 10%, thus selling the power (au kuuza hewa) at inflated prices.....

Ila nadhani perception yangu ambayo ni tofauti na wengi Nishati ambayo ni nguzo ya productivity Kampuni kama Tanesco inabidi ipimwe (at-least ndani ya nchi) kwa kiasi gani watu wanapata nishati ya uhakika kwa affordable prices na sio kiasi gani cha fedha inakusanyia nchi (kuna domino effect inayogusa nyanja zote kama hakuna umeme wa uhakika na wa gharama rafiki); hii ni kama binadamu kujipiga ganji kwenye balanced diet ambayo mwisho wa siku unalipia kwa gharama ya matibabu

Kwahio kwa muktadha huo ningekuwa mimi Tanesco nisingeiangalia kama mshindani wa wadau wengine bali facilitator na mshirika ambaye anafanya nao kazi; Kwahio yoyote anayeweza ku-generate umeme cheaply kuliko vyanzo vyake Tanesco wachukue;(hapa washindani ni individuals whom can generate to supply to the GRID - bei yao lazima iwe cheaper or atleast the same as what Tanesco can generate) Biashara ifanyike kwa kuuza surplus nje ya nchi ili kujipatia pesa ya kusaidia kampuni na nchi na kuwahudumia watu wa ndani; from that perception utaona kwamba kutakuwa hakuna conflict of interest na wadau wazalishaji (ambao kila mtu mwenye paa la nyumba na yeye atakuwa mzalishaji) bali itakuwa ni symbiotic relationship..., kila mtu ananufaika kwa productivity ya mwingine na sio competing....

Lakini realistically that is a Pipe Dream, Tanesco ni Kibubu cha Serikali na wanufaika wachache wanaotumia technicalities kuwahadaa watu; and now they are giving the Dog a bad name, and soon they will hang it......
 
Hili jambo ulilolisema kama nimekuelewa vizuri- nalielewa na nishawahi kuliongelea.

Kwa nchi zinazoendelea kuna umuhimu wa kufanya mambo kama umeme, maji, internet kuwa "public good", kama barabara, ili kuchochea uchumi ukue kwa kasi na vizuri zaidi, halafu kadiri uchumi unavyokua zaidi, kuongeza bei iwe realistic zaidi.

Tuingize watu wengi kwenye gridi ya taifa, tupate econonies of scale vizuri, tywanyanyue wengi kutoka abject poverty, halafu wakinyanyuka kutatokea kuongezeka kipato na consumption patterns fulani tutawaongezea kulipa tu.

Nafikiri huu ndiyo ulikuwa mpango mzima wa serikali, kwenye makaratasi zaidi, lakini, ukiingia kwenye utekelezaji ndipo unakutana na changamoto zetu za kila siku.

Tunaandika mipango vizuri sana, ila kwenye utekelezaji kila mtu anapenyeza 10% zake na kufanya mambo kwa amri kutoka juu, inakuwa matatizo mengi kuliko ufanisi.

Nilikuwa namsikiliza Maharage Chande anasema gharama za uendeshaji ni kubwa sana halafu watu hawalipii umeme inavyotakiwa, wanalipa below market price, hivyo uzalishaji wa umeme unakuwa na changamoto nyingi.

Ila hilo la watu kuuza umeme kwenye grid wangewekeza hapo, wakaweka bei nzuri, nafikiri watu wengi wangechangamkia tenda hiyo kuweka solar panels, kuuza umeme etc.

Mimi mwenyewe sina tatizo la umeme kukatika, ila nafikiria sana habari za mazingira zaidi. Kuna jamaa yangu namtafuta, akiweza kunipa plan ya $30,000 au pungufu nataka nipige solar panels nyumbani, uzuri hapo naweza kupata subsidy kutoka state government, halafu nikifunga panels nauzia umeme kwenye grid, huku US wanaweza kufanya hivyo.
 
Tatizo ni Samia kukumbatia mafisadi ndio chanzo Cha mambo yote haya, Yani huyu mama ni janga, Hana hata uwezo wa kukemea.
 
Nani anaemteua? Halafu kwani Maharage Chande ndio kaleta ukame? Maharage ndio mtoa pesa za kuanzisha vyanzo vipya? Upuuzi.

Ila Sasa Kwa Afrika Jamaa wanaodhalilisha hivi na kuongea ndio huonekana Viongozi Sasa [emoji16][emoji16]
Hao wamefungulia maji kule mtera makusudi, hakuna ukame bwana wewe, huu ni mwendelezo wa mambo ya kishenzi ya serikali hii iliyojaa wezi
 
Hao wamefungulia maji kule mtera makusudi, hakuna ukame bwana wewe, huu ni mwendelezo wa mambo ya kishenzi ya serikali hii iliyojaa wezi
Hivi kumbe Kuna watu mna akili za kipumbavu hivi? Wanaojiita baba Wana hasara ikiwa mwanaume unaweza amini Kila unachoambiwa kama mwanamke.Pole
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…