Mahari sio lazima, ni mila potofu ya kupingwa

Mtibeli nakuunga mkono asilimia zoooteeeee!
 
Muache na kuwahonga basi kama hamtaki kutoa mahari. Kutoa mahari hamtaki lakini kila s iku mpo bize kuwhonga pesa ili mkalale nao.. Hii mada naitafsiri kama shambulio jingine dhidi ya jinsia ya kiume..

Mahari ina maama kubwa sana katika maisha ya wanandoa zaidi ya unavyofikiria..
 

Embu tupo mantiki ya mahari kwèñye Ndoa ili tuone hoja yako inanguvu kiasi gani
 
Nashukuru.
Uje úkiwa na hoja kuntu na ZENYE mashiko. Kizazi Hiki kinahitaji hoja zaidi kuliko zile hadithi zetu za Zamani za sungura na Fisi
Zamani mahari ilikuwa ni shukrani kwa mzazi wa mtoto wa kike.. Mahari ilikuwa ni kuunganisha koo mbili tofauti.. Ilikuwa heshima kwa mzazi wa mtoto kike..

Leo hii mahari haijabadilika maana yake katika jadi zetu bali imeongezeka.. Mahari ni ishara ya utayari wa mtoto wa kiume kuingia katika ndoa.. Mahari kwa asilimia kubwa ni usalama wa mtofo wa kike katika mahusiano.. Mahari ni kutimiza mapenzi ya Mungu.. Kumbuka Yakobo alifanya kazi miaka 14 kama mahari ya wake zake wawili..

Mahari kwa kiasi kikubwa inamfanya mtoto wa kike awe na amani na utulivu katika mahusiano akitambua fika kuwa mtu aliyenaye ni wa uhakika.. Mahari inaonyesha umakini wa kijana wa kiume katika ndoa..
Naomba niishie hapo.. I stand to be corrected..
 
Katika Qur'an haina mapokeo ya watu usizue! Lete ushahidi.

Qur'an ni true revelation from Almighty Allah.

Biblia ndio kuna maneno mengi ya watu yenyewe inajitambulisha hivyo.

Wakorintho wa vitabu vinginevyo.
 
Mahari ni swala lililoegemea katika misingi ya Kidini/imani na tamaduni za kimakabila/mila.

Ndoa nyingi zimefungwa katika misingi ya aina hiyo (kidini/kimila) misingi ambayo mahari ni sehem ya jambo la wajibu katika kukamilika kwa tukio lenyewe (ndoa)

Tunaweza kutoa maoni juu ya kinacho tolewa as mahari ikiwa itatumika kama fursa ya mtu/watu kumkomoa mtu au kuona hiyo ndio njia ya kutoka kimaisha... na maoni yetu yakapokelewa.

Ila maoni juu ya kutokuwepo kwa mahari katika ndoa hayana nafasi katika misingi ya ndoa kidini hasa uislam.
Kwa sababu mahari ktk uislma ni jambo la wajibu, japo sheria haikuweka bayana juu ya nini kitolewe na kwakiwango gani. Ila makusudio ni kuwepo kwake...


Nje na misingi ya Kidini au kimila mahari si jambo lililotiliwa mkazo, linaweza kuwepo na hata lisipo kuwepo haliathiri wala kuzuia ndoa isifungwe, muhimu ni makubaliano ya wanao oana, uwepo wa mashahidi na mfungisha ndoa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…