Japkas
JF-Expert Member
- Mar 12, 2014
- 3,011
- 4,617
Unafirisi.Waliooa jasho linawatoka.
Though stori inafundisha sana...
Umalaya sio dili wala nini.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unafirisi.Waliooa jasho linawatoka.
Though stori inafundisha sana...
Umalaya sio dili wala nini.
Dah hongera kwa uandishi mzuri simulizi halikuchosha pia Kuna somo kubwa sn la kujifunzaSehemu ya mwisho...........
........................
Nikatoka pale mti mmoja nikiwa sina hata ninapokwenda,yani sina plani yyt wala sielewi chochote cha kufanya,nikatoka pale kwa kamanyola nikaamua kuchanja kwa miguu hadi bamaga,bamaga nikakata kulia ile njia inayopita mabatini moja kwa moja,nikatembea kwa miguu hadi Biafra, muda huo nafika Biafra ni mchana SAA tisa,nikaingia kwa wakala nikatoa laki 3 crdb,nikapanda boda kurudi sinza tena maana nishachoka kutembea kwa miguu,nikafika mahali nikaona kibao cha massage nikaingia.kufika ndani nakuta mabinti kibao wote nusu uchi,udenda ukanitoka,nikaulizia bei ya massage nikatajiwa,nikalipa 40,000,nikaingia na mdada chumbani,akanipiga massage yake na baada ya kuona nimezidiwa akadai 30,000 ya nyongeza
Hujawahi kutukwanwa jf bwashee. [emoji23][emoji23][emoji23]Kwangu Jamii Forum itabaki kuwa ni lecture room kwa miaka yote!
Noma sanaKwangu Jamii Forum itabaki kuwa ni lecture room kwa miaka yote!
Vipi huyo mchepuko na yeye alikuwa mke wa mtu?tuheshimu sanaaaa wake zetu aiseee hasa kama mke wako ni mtu wa dini sanaaa binafsi mke wangu ni mtu wa maombi sanaaa tumebarikiwa watoto wawili ila zamani kidogo huko tumewahi pitia misukosuko kwenye ndoa ambayo chanzo chake ni mm coz nilikuwa na mchepuko ambao alikuja kufuma mpaka picha zake kwenye simu yangu hii nilisahau kufuta chats siku moja aiseee alilia sanaaa usiku ule na alikuwa mjamzito ilibidi nimbembeleze sanaaa na kuomba msamaha ila alinisamehe yakaisha na amani ikarejea ndani ya nyumba
Hapana huyu hakuwa mke wa mtu ila alikuwa mwanafunz wa chuo alikuwa kapanga mtaa wa pili kutoka mtaa ninaoishi.Vipi huyo mchepuko na yeye alikuwa mke wa mtu?
Alikuwa michepuko wangu na Mimi ndo nililipia Kodi aiseeee... Maisha Ni duara..WANASEMA ulichokiona kwa mchepuko wangu na Mimi nakiona kwa mke wako ngoma droo...wake za watu huwa sitongozi aiseeHapana huyu hakuwa mke wa mtu ila alikuwa mwanafunz wa chuo alikuwa kapanga mtaa wa pili kutoka mtaa ninaoishi.
Sehemu ya mwisho...........
........................
Nikatoka pale mti mmoja nikiwa sina hata ninapokwenda,yani sina plani yyt wala sielewi chochote cha kufanya,nikatoka pale kwa kamanyola nikaamua kuchanja kwa miguu hadi bamaga,bamaga nikakata kulia ile njia inayopita mabatini moja kwa moja,nikatembea kwa miguu hadi Biafra, muda huo nafika Biafra ni mchana SAA tisa,nikaingia kwa wakala nikatoa laki 3 crdb,nikapanda boda kurudi sinza tena maana nishachoka kutembea kwa miguu,nikafika mahali nikaona kibao cha massage nikaingia.kufika ndani nakuta mabinti kibao wote nusu uchi,udenda ukanitoka,nikaulizia bei ya massage nikatajiwa,nikalipa 40,000,nikaingia na mdada chumbani,akanipiga massage yake na baada ya kuona nimezidiwa akadai 30,000 ya nyongeza ili anipe tunda,ckubisha nikatoa,nikapewa goli 1 kwa elfu 30 na massage 40,jumla 70,nimetoka pale nyege zimeisha ndio najilaumu kwamba nimepoteza 70k hv hv,kwa kupata goli 1,muda huo SAA 11 jioni cjala chochote zaidi ya supu nilikunywa muda ule natoka mti mmoja,....nikachukua boda hadi mawasiliano nikapanda gari za tabata,nikashuka bima,nikatafuta lodge nzuri pale nikapata ya elf 30,000.nikatoka nikaenda zangu kwetu pazuri,nikaagiza kuku mzima bila ndizi choma wala ugali,nikamchakata akaisha nikashusha maji kubwa.
Muda huo SAA 12 jioni,
Nikaagiza Serengeti lite bariidi nikaanza kuzishusha,nikanogewa,nilizishusha sijui ngapi hata sikumbuki idadi,...ila zaidi ya kumi na kuendelea,...... Sasa nimelewa,nikatamani kutafuta demu nikaogopa ataniibia maana nishalewa.SAA tano ucku nikatafuta bajaji ikanirudisha kulala Lodge,
Cku inayofuata nikaona hapa dar kwa stress nilizonazo nitakula hii hela hadi iishe bila kufanya chochote,....nikampigia jamaa mmoja tulifanyaga nae kazi kipindi cha nyuma,nikamuuliza alipo akanambia yuko kwao Dodoma wilaya ya chemba anapambana na kilimo,...huyu jamaa yy alitumbuliwa na Magu kwa kufoji cheti 2017,na Mimi nikatimuliwa kwa makosa ya kizembe na kusababisha eti wao wanasema hasara kwa serikali kwa kuingia mkataba mbovu,mkataba wenyewe ulikuwa unahusu jamaa mmoja aliekuwa ana supply vifaa vya ofisi,na kweli kwenye ile ishu nilipiga hela kidogo kama milioni 2 ila wao wakanambia nimesababisha hasara ya 18 milioni,nikaishia jela miezi kadhaa na kazi nikakosa,.
Bac huyu jamaa aliitwa sele,sele nikamwambia bwana nimejiingiza mwenye biashara ya mazao imenipiga hasara kubwa,....sele akanambia niachane na biashara,akanishawishi niende chemba nikakodi mashamba tulime,na yy akaahidi kunisaidia ushauri maana yy ni mzoefu kiasi..cku inayofuata nikapanda basi zinazoenda hadi babati kutoka dar,...nikashuka chemba pale SAA tisa mchana,jamaa akanipokea vzr tu.jioni tukakaa mahali na kupanga mipango yetu,akanambia kuwa sasa tuwahi mashamba kabla hayajapanda bei za kukodi,kwa wakati huo tulipata sh 20,000 kwa kila heka,nikachukua heka 40 kwa sh laki 8,tukaanza kuandaa shamba kwa kusafisha.baadae tukatulia kusubiri msimu wa mvua uanze tulime na kupanda,...wakati tukisubiri msimu wa mvua nikaondoka kwanza kurudi home arusha kusalimia familia,....
Dah jamani ukimtegemea Mungu kwa kweli unafanikiwa sana,nimefika Arusha nikakuta wife biashara imekubali kweli kweli,duka limependeza na ile 2m nilomuongezea ameongeza vitu vingi ambavyo hakuwa navyo mwanzo,na biashara ilikua inatoka kweli kweli,wife akanambia napoteza muda tu kuzunguka mwenye mabiashara yanayonipa hasara wakati pesa IPO pale pale mjini,akanishauri sana nifungue duka lingine tofauti na like lake na kujaza Mali kisha kila mmoja asimame na duka lake,nikamwambia kuwa nishaingiza pesa nyingi kwenye kukodi shamba na kulisafisha,tukashauriana na wife kuwa baada ya kuvuna na kuuza bac nirudi mjini nikawekeze zaidi,ukweli nilitamani kuanza biashara kama ya wife maana kwa Siku nilozokaa nae pale dukani kwake nilishuhudia mauzo yake yalivyo mazuri.
Cku zilienda hatimae msimu wa kilimo ukawadia,nikafunga safari kurudi chemba kwenye kilimo,tulipanga kupanda alizeti na mahindi.nikaingiza trekta shambani kulima,on kanunua mbegu na kupanda,nikaendelea na matunzo ya shamba hadi kupalilia na kuvuna,mavuno hayakuwa mazuri sana kiasi cha kupata faida nzuri,baada ya kuvuna ckutaka kupoteza muda nikauza mazao,kwa msoto wote niliopata shambani nikaambulia faida ya sh laki 8 pekee,nilikua naandika kila shilingi niliyotumia hadi nauli za basi,chakula na malazi,mwisho wa cku naambulia faida ya laki 8 kwa miezi zaidi ya 6,nikashukuru Mungu kwa hicho kidogo maana angalau hela ilirudi,
Nikaondoka kurudi mjini,nikakuta wife kwa biashara yake ile ndogo ametengeneza faida ya milioni na laki 4 kwa kipindi mm nipo nahangaika na shamba lililonipa faida ya laki 8 pekee,hio milioni na laki 4 ya wife ni faida alotengeneza tofauti na mtaji matumizi ya nyumbani.
Nikaanza kutafuta fremu nzuri iliopo site nzuri ya kazi.nikapata maeneo ya Shamsi,fremu nzuri tu nikalipa kodi ya mwaka,nikafungua duka LA nafaka,.....nauza mchele wa magugu,wa kahama,na wa mbeya,nauza maharage ya sina mbalimbali,nauza choroko,kunde,ufuta,ulezi,karanga,mahindi,na unga wa mahindi,nauza pia njugu,unga wa ngano,mafuta ya alizeti,dagaa,na vingine vingine.nilipata shida kidogo kukusanya mahitaji ila baadae nikajaza kila kitu,hio ilikua 2019 mwezi wa 7,kazi nikawa napiga mwenyewe,na kazi ikaenda vizuri sana,nikatafuta kijana wa kunisaidia ambae alikua shemeji yangu mdogo ake wife.Nikarudi kufanya ibada zilizonyooka,kifupi nikamrudia Mungu baada ya kuona nimetulia na hela inaingia....
Akiba Benki nikabakisha milioni 2 tu,zingine zote nikaingia dukani,jamani asikwambie MTU Mungu ukimtegemea anakuokoa,nilishakata tamaa kabisa ya maisha baada ya kwenda jela...,Sasa hivi mtaji umekuwa mkubwa hadi nafata Mali mwenyewe,kama mchele napiga simu kahama natumiwa hadi tani 10.hela kiukweli imeongezeka sana na usafiri nimenunua mwaka huu mwez wa 3,japo nimenunua gar ya kawaida tu raum lakini inanisaidia sana,...Mambo yakienda hivi natarajia mwisho wa mwaka nifungur duka lingine LA nafaka mtaa mwingine maana nataka zinalipa,MTU hawezi kushinda na njaa,lazima atakuja kununua tu chakula,tofauti na maduka ya vitu kama nguo,nguo MTU akiwa hana pesa atavaa nguo za zamani ila chakula atakopa hata pesa anunue chakula cku ziende,nawashauri wadau mjaribu hii biashara,ukiangalia faida yake ni ndogo ila inauzika sana,unajikuta jioni mauzo yako ni laki 4 hadi 4.5,ukitoa mtaji hapo faida inachezea 50-70 kwa cku,ni pesa nzuri sana,wife nae hakosi faida ya 30 kwa cku,maisha yanasonga kwa Uwezo wake Allah.Nilikuja kumuomba wife msamaha kwa yote machafu nikimfanyia nae akanisamehe na kusema nizidishe kuomba msamaha kwa Mungu maana ndio nimemkosea zaidi.
Eti cku moja mwaka huu mwanzoni yule Sauda akanitafuta tena,cjui anatoaga wapi namba zangu huyu Dada,akadai yupo arusha na amenimisi,akaomba tuonane,nikajua hapa narudishwa tena kule kule kwenye mabalaa na manuksi ya wake za watu,nilimfokea sana kwenye cm,nikamwambia we mwanamke koma kabisa kunitafuta,kwa tulia na ndoa yako na umuheshimu mumeo,mm sio yule wa miaka ya nyuma tena km ulivyozoea,mm nimerudi kutenda mema na nikaomba asipige namba zangu maana zitaanza kuleta vishawishi,wanawake wengine cjui wakoje jamani,akawa hasikii na kuzidi kunisumbua hadi nikamtukana matusi ndio akakoma(Mungu nisamehe kwa kumtukana),...ilikua sina jinsi ya kufanya maana alitaka kunizoea,...
Namshukuru Mungu hadi hapa nilipo na ninatamani Mungu anisamehe kwa maovu niliyofanya.
Nawashauri vijana wenzangu na wakubwa zangu na wadogo zangu waume kwa wanawake,tujifunze kuheshimu ndoa zetu na ndoa za watu wengine,tuzihifadhi tupu zetu pia.
Majanga mengine ktk maisha huwa yanakuja kwa mikosi na lawama za watu wengine tunaowadhulumu,kudhulumu sio lazima udhulumu Mali tu,Bali hata kuzini na mke wake au muwe wake pia umemdhulumu,..
Nimependa kuwashirikisha ili atakaejifunza na wajifunze,asije kupita nikipopita mimi na kupata madhara kama yangu au makubwa zaidi yangu,Mimi Mungu aliniepusha kuuwawa,kufanyiwa unyama wa kudhalilishwa na pia aliniepusha na maradhi japo alichapa fimbo ya kuniadhibu kimaisha lakini nimetubu kwa dhati na sasa naona nafuu ya maisha.
Asanteni sana kuwa kushiriki pamoja,na ninawaomba mjifunze kutokana na matukio hayo,msisome tu kama burudani na kisha mkaja kupita nilipopita ndugnizangu.Leo nimeutua mzigo mzito
Naweka kalamu chini...
Amani ya Mungu iwe nanyi.