Maisha na mikasa ya safari yangu nchini DR Congo miaka ya 2000's hadi kutaka kupigwa risasi hadharani

Maisha na mikasa ya safari yangu nchini DR Congo miaka ya 2000's hadi kutaka kupigwa risasi hadharani

Inaendelea sehemu ya sita....

Nawasalimu ndugu bila shaka mnaendelea powa sasa baada ya mechi kuahirishwa hadi saa moja naomba tuendelee sasa .

Tumeshavuka boda tuko upande wa congo huku nipo kwenye gari nafanya mazungumzo na yule jamaa anaetaka lifti mimi sikuwa na chakuongezea tena nikamshukuru jamaa nikamwambia kuna mtu ndo mwenye magari kama atakuja ntamwambia kuna kichwa akikubali tukubebe ntakubeba usijali ila.usikae mbali sanaa na hapa mimi nikapandisha kioo nikaendelea kuwaza huku nawazua aise nikiri kuwa katika maisha yangu yetu siku ile ndo nilipa msongo mkubwa wa mawazo haijapata kutokea imagine nina dolla 130$ mfukoni lakini sio raha hata kidogo kipindi hicho hiyo pesa ilikuwa juu ukiabadilisha kwa madafu unapata hata kodi ya nyumba ya mwaka mzima na chenji inabaki.

Wakati naendelea kuwaza mara ghafla rama akaja akawa ananiongelesha kuhusu hali ilivyo njiani yani linaongea utafikiri lilikuwepo anasema sasa hakuna kitu askali.wa congo walisafisha njia hakuna tena wakutusumbua tusubiri tu maboss waje watupe hela sisi tutoboe halafu anaongea huku anacheka wakati huo mimi mawazo yapo mbali sanaaa.

Kuna kosa kubwa nilifanya pale boda wakati wa kumsikiliza yule jamaa anaetaka lifti nilimwambia kuwa tutaondoka pale mda si mrefu halafi nilivyocheki ila sehemu aliyokuwa aamekaa kwenye kibanda sikumuona yani alipopea ghafla sasa katika kumpa taarifa rama kuhusu yule jamaa ghafla akabadilika akawa ananilaumu nikashangaa kumbe huo ndo mchezo wao majambazi na na watekaji wengine wanakuwa na. informer wa vikundi vya waasi mfano MaiMai yani wanatengeneza mpango kuanzia boda ili kufanikisha utekaji sasa ukiwapa taarifa zako muda wa kutoka wanajipanga vizuri nakutoa taarifa kwa wenzao walipo polini katika ya poli huo ndo unakuwa mwisho wako .wazee wa tank za mafuta wanajua hii michezo , wajinga wanaweza teka tank zima likaingizwa porini wakanyonya disel au petrol yote na wakaichoma gari moto wakikusamehe mnaachiwa gari tupu sasa kimbembe kujieleza kwa majiri lokapu lazima ukae kwanza.

Basi rama akawa ananipa hizo story nikajua kumbe ndo maana jamaa alikuwa ananihoji maswali mengi sanaa kuhusu hata aina ya gari Unajua zile gari zilikuwa mpya tena na makaratasi yake bado hivyo nikawa nimeelewa sasa ghafla tu rama akatoka kidogo akarudi tena baada ya kama nusu saa akaniambia kijana umeshaharibu ratiba sasa ngoma hapa tunaondoka saa kumi jioni hela imeshatumwa na maboss customer kwa jamaa yao tukale tupumzike kidogo ila kuna askali miongoni mwa wale alikuwa anaongea nao pale boda wanataka lift hadi lubumbashi hivyo tutakuwa nao na sasa tumepata ulinzi wa chee

Ebwanaeee nikasema sasa naingia vitani bila kupenda yanii tupo na wale askali kwenye gari na mibumduki yao ile mikubwa mikubwa hivi tukifika katika polini wakatwambia simameni tuzipige kwanza na waasi tutakataa nikawa nawaza najiuliza sasa maisha yangu ndo yamefika mwisho ...

Wakati nawaza likaja roli la jeshi la congo pale boda likaanza kuwapakia askali kadhaa kwenye roli wakapanga mle walikuwa wengi takribani kama mia nakitu hivi wakapanda waliokuwa na rama kama 15 wakagoma wakasema wao wana gari za kupanda watangulie tu wao watakuja na sisi .
Yani lile roli limejaa matundu ya risasi ubavuni aise halafu hata vioo halina halafu kilichonifurahisha lile roli alikuwa anaenda mwanamke inaonekana ni shupavu kweli kweli , waozijua zile benz za mitairi mikubwa na mfano wa gari alilokuja nalo yani lile gari kwanza halina vishukio yani nikurukia tu na kushuka unaruka tu sasa yule dereva mdada lakini shupavu kweli kweli yani alivyokata kona kuingia boda nikasema labda mwanaume aise alifungua mlango akaruka kutoka juu hadi chini bila kuteteleka hata kidogo halafu yupo full combati chini na bastora na kisu kiunoni na bomu la granade, juu yule mdada alivaa tu kusinglendi cha jeshi ebwana ee yani niseme tu ukweli yule dada aliniongezea ujasiri yanii mwanamke kwanza mwanajeshi halafu katoboa katika njia chafu kama ile mimi kwanini niogope tena mtoto wa kiume lakini nafsi nyingine inaniambia huyo ndo kazi yake kazoea lakini kwakweli alinifanya mipate faraja ya japo nilimuona tu kwa mbali wala sikupata hata nafasi ya kuongea nae.

Naomba niongee kitu kidogo kabla sijaendelea kuna mdau kwa comment anasema askali.kukupa bunduki ushike shike ni ngumu sanaa nami nakubaliana nae kabisa ila sio askali wa congo kwa kipindi hicho yani wale sio askali ni washenzi yani yule ukashampa beer zile prisner mbili tu unaweza muomba bunduki ukaenda ukafanya yako ukarudi zako hamna askali mle labda sasa sijui nidhamu sifuri halafu kipindi hicho kumuona raia anatembea na bunduki tena zile raifo za masniper mtaani ilikuwa jambo la kawaida kabisa wala hakuna wa kumshangaa mwenzio.
Kama mnafuatilia taarifa kule GOma mashariki mwa DRC haya mambo yalikuwa yanaendelea hadi majuzi mwajeshi mzalendo wa kitanzania GEneral james Mwakibolwa alivyoenda kukomesha huu ujinga kupitia operation ya ondoa waasi wa waADf na wale waliokuwa wanapata ufadhiri kutoka serikali ya Rwanda mwanajeshi muasi kibaraka wa kagame sultan Makanga mpiganaji hodari wa vita ya msituni .siku moja ntaleta story nini alifanya kule mashariki mwa drc hadi wacongo wakiona siraha wanaikimbia kwa kifupi hii ni mbinu yakuchanganya jeshi la serikali yani waasi hugawa silaha kwa raia na kuwaambia wajilinde wenyewe hivyo huvichanganya vikosi vya usalama kujua muasi ni nani ?

Itaendelee....wazee sasa tumefika patamuuu urojo.iftar inakaribia karibuni.
Saa nne tena tupia nyingine mkuu

Sent from my SM-G935F using JamiiForums mobile app
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ndugu zangu bila shaka mwenyezimungu anaendelea kutupigania hadi sasa.

Ndugu leo naona nilete story kidogo kuhusu safari yangu moja hivi nchini DRC mikasa na visa mbali mbali kwa kipindi chote cha safari wakati napambana na maisha kwenye udereva ili niweze kuishi kama mnavyojua maisha ni popote na kujaribu ni muhimu kuangalia kila sehemu ili uweze kutoka ukinzingatia kuwa wengine shule yetu ni kidogo hivyo ni muhimu kijipambania kwa kila hali ili uweze kujikimu kimaisha tukawa tunashike hili na lile ili mrasi tuweze kuishi.

Story yangu ni ndefu kigodo ila ntajitahidi niimalize kwa wakati ili kuepuka zile maneno za kakimbia sijui nini ila naomba tuwe na uvumilivu tu kwani swala la kuandika nalo ni mtihani ukizingalia device tunazo tumia sio rafiki .kwa wale wasio wavumilivu naomba tupite tu hakuna haja ya kulalamika.

Story inaanzia hapa...

Miaka 2000's kulitokea wimbi kubwa la usafirishaji wa magari kutoka bandarini Dar kwenda DRC kipindi kicho ikitwa congo (kama sijakosea) kipindi hicho nilikuwa najishughulisha na udereva taxi pale Mapambano kijitonyama nikipindi ambacho biashara ya taxi ilikuwa na hela kiasi kwani biashara ya Bajaji na bodaboda ilikuwa bado na watu walikuwa hawajazoea kupanda vyombo hivyo, basii maisha yakawa yanasonga mbele kama sijasahau mwishoni mwa miaka ya 2001 ndo vita congo ilikuwa imepowa japo nilikuwa siwahi kufika huko hata mara moja.

Kijiweni kulikuwa kuna mshikaji alikuwa anaitwa Rama kwanza nikili kuwa huyu jamaa alikuwa mjanja kupitiliza na alikuwa anasafiri sanaa inasemekana hata nganda alikuwa anabeba japo tulikuwa wote pale pale kijiweni nae ana kigari chake mwenyewe anabeba abiria ndipo akanipa mchongo wa kusafiirisha magari ya wa kongo kwenda Congo kipindi hali haikuwa nzuri kwakweli hivyo madereva wengi walikuwa hawapendi kwenda huko japo wacongo walikuwa wanapanda offer ya mpaka dolla 250 kuifikisha gari KASUBALESA boda ya Congo na zambia then unamwachia anamilizia kipande chake.

Hapo ndipo jamaa yangu Rama alipopata hiyo fursa kwa jamaa yake alieoko pale bandarini ambae alikuwa na kampuni yake ya clearing na fowarding pale bandarini na kumwambia kuwa kuna wacongo wanahitaji magari yao yafike lumbumbashi then wao watayasafirishi kwa ndege kwenda kinshasa ila wao hawapandi hizo gari wao tutakutana lumbumbashi sehemymu moja sehemu moja kunaitwa KOTA naona nikaribu na soko kubwa la Lubumbashi mjini katikati.

Cha ajabu jamaa walitoa pesa yote kwa jamaa yao wa pale bandarini na kampuni ndo ilitakiwa isimamie kila kitu hapo ndipo mwanangu Rama akanitustua nakumbuka ilikuwa ni kati ya mwezi wa tano kwenda wa sita. Mvua zinanyesha Dar hakuna mfano abiria hakuna nikaona bora nitoe gari kwa jamaa nikimbize IT kwanza nami nipate uzoefu.

Baada ya jamaa yangu kuweka mambo sawa ikiwemo kupata passport ya karatasi na chanjo ya homa ya manjano mzes mzima siku ikawadia jamaa yule akatupa dolla 100 advance, 50 maillage na 50 ya barabarani nikiongea bararani mnilewe hiyo ya wazee .Gari mpya kutoka kiwandani yani bado zina makaratasi mitusubishi dabo cibin mpya kabisa wazee tukawekewa full tank. Zikabandikwa number za IT .siku ya j2 ndo safiri ikawa imeanza rasmi mara ya kwanza kusafiri na magari ya IT ila mwenzangi rama yeye alikuwa mzoefu hata kwa njia hio pia alikuwa anaijua vizuri na alikuwa anajua hata kizambia kidogo na kikongo kisawahili chao kile cha kuya Papa uko na makuta ngapi? Hhhhaaaa...

Safari imeanza.

ITAENDELEA JIONI...
Mh
 
Kumbe😁 Sasa ndo nmekuelewa
Huko comments za juu naona watu wanamtaja huyo konda msafi, nikawa nashangaa ndo Nan huyo na alifanya nn?🤔,
😅😅😅😅 konda msafi jamaa wa nyuzi za south Africa

ukileta tu uzi kuhusu south africa anauvamia anaanza kusahihisha kama na yeye ulikuwepo naye yani 😅😅
 
Rama katili[emoji23][emoji23]

Ila ile njia konki sana aisee ukiwa na roho nyepesi kule hakufai

Kule unakua na roho ya Pakashume aisee. Nishaenda Kolwezi kama mara mbili na Lubumbashi banyamulenge kama kawaida walitutaitisha wakatupukutisha dizeli nyoko wale
Kolwezi nakubali mkuu ni balaa ile mahali asee nakumbuka mm nilienda kupeleka generators nikiwa kama kushoto kwa watubwa malori wanaelewa kushoto ni nani
 
Back
Top Bottom