Majaribio ya treni ya umeme yafanyika

Hii ndoo ilyofanyiwa majaribio mbona kama itakuja ya hivo tumepigwa pakubwa naona kama imepitwa na wakatiView attachment 2279510
Tuacheni hii tabia ya kupondaponda na kubezabeza kila kitu. Hicho kichwa kinatumia umeme na kinavuta mabehewa mengi kwa kasi ya ajabu. Intercity train (mikoani) Ujerumani na nchi za skendinevia hadi sasa hivi vinatumika. Hapo chini huo mtambo unatoka Oslo hadi Bergen Norway kitu kinavyokata mbuga acha tu.
 
Nchi ngumu hii,tuepuke kufarijiana unaweza ukakuta hicho kichwa kimekuja kujaribiwa na vyenzie vipo njiani kwa sample hiyohiyo.Walivyo na sifa hawa viongozi wetu si wangekuwa wameshatuonesha picha ya hizo treni mapema.
 
Itapendeza kama umeme hautakuwa wa luku....
Nikija Dar, natumai itakuwa tayari niipande mpaka Kigoma nikumbUKE nostalgia ya reli ya kati miaka ileeeee...una safiri na waranti yaa uanafunzi...
Nipite Morogoro, kutoka Moro mpaka Kilosa ni viunga vya misitu ya Uluguru ya ukijani na ukungu wa kutosha, mara tunaingia Kilosa, hatukai sana tunaitafuta Kongwa, mara Dom hii hapa, nishuke niende Wimpy's nikapate msosi, nirudi na kushushia karanga za kuchemsha, tuitafute Manyoni, sijui yale marashi na sabuni za ulaya walikuwa wanatoa wapi wale wauzaji wa Manyoni, mara Honi ya treni ikilia unaliacha liaanze kuondoka ili ulikimbize na kudandia na ujione VanDamme, hapo tunaitafuta Itigi ni Mandhari ya kutosha huku umechungungulia dirisha maeneo ya mlangoni, na nakumbuka ikifika Tabora, unatakiwa uwe macho juu na mizigo yako maana hapo ni wezi wako juu ya treni inaeenda wananing'inia na kuchomoa mabegi,
aaahh naona hivyo vituo nimechanganya madawa....nitarudi nikiwa sober...
 
Kichwa ndiyo nini? Sema*engine"
Mambo mengine mnalazimisha bure
 
Vichwa vya wendawazimu ni vingi Kwa Hawa ukoo wa panya!!
 
Mleta mada lazima atakuwa mfuasi wa Mr #dishlimetilt, maana ndiye huwa ana wafuasi wenye uelewa mdogo kiasi hicho. Yani akili yake ilivyo ndivyo na wafuasi wake walivyo. Timba humfanana mkataji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…