Majasusi wabobezi 8 wa Kitanzania wakamatwa nchini Malawi

Mkuu mwenye uelewa amekuelewa hakuna state security aliye mzembe hivyo they are full of techniques
Tunawasubiri tu hao. Malawi wafanye ujinga wao. Ngerengere mazoez tuendelea kufanya
 
Kweli kabisa JF imepoteza credibility. Imegeuka kijiwe cha wahuni

Na Wewe pia ukiwa miongoni mwa hao Wahuni, hivyo sisi Wana JF tunafurahi kuwa na Muhuni Wewe uliyetukuka kabisa.
 

Mapovu yote haya ya nini Mkuu? Haya kaunganishe sasa nguvu zako na Waziri husika muende mkawatoe hao Ndugu zetu huko Malawi ili pengine na Wao wasijewekwa katika Viroba na Mawe Shingoni kisha wakatupwa Ziwani au Mtoni. Maneno mengi halafu Pumba tupu. Kuna mahala labda umeona nimeikashifu TISS? Nilichokisema na bado nasisitiza tena kukisema tena huku nikijiamini kabisa ni kwamba Idara hiyo inahitaji kujitathmini mno hasa Kiutendaji na jinsi ya kuwakufunzi na kuwaajiri Watumishi wake kwani kuna mapungufu mengi ya hatari yanajitokeza kwao kila mara na si jambo jema kwa ustawi mzima wa Kiusalama kwa nchi yetu iwe ndani au nje. Jifunze kujenga Hoja na epuka kuwa Mpuuzi tafadhali!
 
Hii ni habari mbaya kwa nchi yetu kama ni kweli,

Nchi ndogo kama Malawi kukamata wapelelezi wetu inatuweka sis ktk kiwango cha chini zaidi yao.
 
Nyie nn tena mnaongea wenyewe tu

Usisumbuke nao Mkuu unaweza ukadhani hao ni Watu tofauti tofauti wanatiririka na hicho Kifaransa chao ila nikuhakikishie tu kuwa huyo ni Mtu mmoja. JF ni zaidi ya uijuavyo Mkuu!
 
Je kweli ni majasusi wabobezi kama mleta mada alivyosisitiza?
 
Majasusi 8 wakamatwe kwa pamoja, sidhani na sitarajii kitu kama hicho kwa jasusi anayeijua kazi yake vyema. Hamuwezi mkapelekwa lundo kwa pamoja kama polisi wanakwenda kutuliza ghasia.
 
Usisumbuke nao Mkuu unaweza ukadhani hao ni Watu tofauti tofauti wanatiririka na hicho Kifaransa chao ila nikuhakikishie tu kuwa huyo ni Mtu mmoja. JF ni zaidi ya uijuavyo Mkuu!
Mkuu lakini kwa uzoefu wako inakuwaje majasusi 8 washikwe kwa pamoja hapa ndipo nimekuwa na mashaka na uwezo wao utakuwa ni Mdogo sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…