Maji ni huduma ambayo Serikali inafeli vibaya mno, uhaba na mgao karibu kila mkoa japo mabilioni yanatumika. Rais Samia anashindwa wapi?

Maji ni huduma ambayo Serikali inafeli vibaya mno, uhaba na mgao karibu kila mkoa japo mabilioni yanatumika. Rais Samia anashindwa wapi?

Kwa ujumla Serikali inafanya kazi nzuri sana hata hivyo kwa mtazamo wangu wanavyotumia Nguvu kubwa kusambaza maji; Wangetumia pia angalau robo ya hiyo Nguvu Kuhuisha vyanzo vya maji.

!
MKuu, umeongea point nzuri sanam kuhusiana na VYANZO VYA MAJI, lakini sio kuhusu huduma ya maji.

Kwa mfano, Dar kukosa maji tatizo sio vyanzo vya maji, tatizo ni watu kutokuwa makini na uzembe wa kazi. Maji yanayoingia baharini ukanda wa pwani ukilinganisha na yanayotumika kuwahudumia watu ni mengi mno! Kwa mfano, miaka ya 2000 wakati kampuni ya Songo Songo ikiweka mambomba ya gesi toka kule Somanga, iliiambia serikali kwamba nunueni mabomba ya maji ili tuwawekee pembeni ya mabomba ya gesi kutoka mto Rufiji kuja Dar, mbadilishe source ya maji Dar toka Ruvu kuja Rufiji. Unajua serikali ilikataa? Unafikiri kwa nini? Kwa sababu walijua watakosa fedha ya tenda ikiwa mabomba yangeletwa Dar kwa msaada!

Nimetoa mifano ya sehemu kama Iringa, Njombe, Tukuyu, Moshi nk. Maji yapo tele, na wala vyanzo vya maji havijaharibiwa. Na maji yanawezwa kusambazwa kwa garivity tu, lakini wapi. Angalia ramani, Tanzania tunaweza kuwa nchi inaongoza Afrika kwa kuwa na fresh water bodies nyingi na kubwa, na mito Lakini hatujaweza kutumia rasilimali hii, tunazidiwa na nchi ambazo ni jangwa kwenye huduma za maji.

Huko Mbeya, kuna wakati walipewa fungu la fedha la kununua mabomba ya maji kwa ajili ya wilaya ya Rungwe. Sasa katika ununuzi ule, injinia wa maji wa mkoa akaamua kuusimamia yeye, akanununua mabomba very low quality kwa bei poa lakini kwenye documents wakaweka bei ya juu. Walipoyafunga yalipasuka yote! Unajua hata Mkuu wa Mkoa wa Mbeya alimfichia siri? Sasa niambie, tutafika kweli? Uzembe tu umejaa
 
inasikitisha sana kuona mtu anamtazamo wa kizamani kama huo na cha kushangaza utakuta yupo RUWASA,mfano mzuri ni mradi wa maji wa ruwasa kijiji cha lopolun na lemishiri kata ya oloirien wilaya ya ngorongoro mradi umezinduliwa na mwenge lakini yamebaki mapambo tu hakuna usambazaji wa maji kwa wananchi.
Kweli kabisa. Yaani kuna uzembe upande wa huduma za maji nchini sijapata kuona. Sijui hawa watu wana akili za namna gani. Wanajiita viongozi lakini vitu vya msingi na rahisi kama kufikisha maji kwa wananchi vinawashinda. Bibi yangu alipata shida ya maji. Mama yangu pia, mke wangu pia, na sasa binti yangu atapata shinda ya maji. Hadi lini? Utafikiri tunaongelea kila mwananchi kununuliwa gari na serikalim hapanam ni kufikisha huduma ya maji ya uhakika kwa wananchi tu!
 
Huku Morogoro kuanzia kihonda kelekea mkundi, tungi ni balaa tuu!! Na akina side hata uwezo wa kuchimba kisima hatunaa!! Tunasubiriii maboza yalete ndoo moja shilingi mia Tano[emoji20][emoji20][emoji20] na familia ni shiidaa!!! Tunasubiriii mvua zikinyesha ndio nafuu yetuu!! Na mvua nazo ndio hazijii[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Maji na umeme ni huduma zisizo na kikomo yaani kuna wamasai na wahadzabe ukiwapelekea maji na umeme wanahama wanaenda mbali kuanzisha makazi mapya huko sasa tatizo haliwezi kuisha kwa style hyo
Fikirisha ubongo huo..

Hapo juu wametajwa hao watu?mimi nipo Dar hapo Mbezi kwenye stand kuu na maji hamna mimi ni mhadzabe useme nimeyakimbia hayo maji?
 
Dodoma mjini Nako nilishanga kukutwa mgao wa maji eti,huku nkuhungu yanatoka kwa wiki Mara 2 kaahh
Hivi hii nchi kuna mkoa ambao maji huwa yanatoka mfululizo mwezi mzima kweli?
 
Mimi mpaka nimeamua kuita wachimbaji wa Borehole drilling na nimepata maji matamu bila chumvi.

Sasa hivi natengeneza swimming pool ili niwe najipoza huku nikiburudika na Bia bardiii.

Maisha mafupi sana haya.

Na huenda nikafungua kiwanda cha maji siku za usoni nataka kuvuta mkopo wa Kiisilamu wenye riba nafuu iliyofichwa fichwa.
Wasambazie watanzania wenzako wanunue walau ndoo sh 100 mkuu Mungu atakuongezea..
 
Wasambazie watanzania wenzako wanunue walau ndoo sh 100 mkuu Mungu atakuongezea..
Hata bure ningewapa Watanzania wenzangu tatizo mtaji wa mabomba ila kama mtu akitia timu hata aje na mapipa.
 
1.8 mills hiyo gharama kina ni mita hamsini (inategemea bed rock ya eneo uliloko)
Imewachukua siku mbili kupima ili kupata maji yasiyo na chumvi.

Nimeweka tenki la 1000 ltrs na linajaaa mpaka yanamwagika.

Tanzania tuna rasilimali nyingi sana ila know how to ndio inahitajika.
Mkuu GT kuna kodi unalipa ukichimba kisima?
 
Mkuu GT kuna kodi unalipa ukichimba kisima?
Sijui, na kwasababu siyafanyii Biashara ni kwa ajili ya,domestic use.

Ila sitoshangaa wakija maafsaa na vitambi vyao na kuanza kudai serivce charge wakati hawajaingiza senti.

Wakidai nakifukia chap chap😁 just kiddin
 
Sijui nianze kufuga organic Sato ambao ni clean wasiokuwa na kemikali za kuhifadhia maiti?
 
Nilitegemea kwamba serikali inayosema inapigana na kupambana sana kuhudumia watu wake ingefanikiwa sana katika suala la kutoa maji kwa watu wake. Lakini inasikitisha sana kwamba hadi leo Tanzania inafeli sana katika kutoa huduma hii kwa wananchi. Na kinachosikitisha hata zaidi ni kwamba hii ni huduma muhimu sana hasa kwa wananwake na watoto, na ina athari katika mambo mengi.

Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
  • Wanawake wanapoteze muda mwingi katika kufuata maji
  • Matatizo ya kijamii kama kubaka watoto na wanawake wanapokuwa wakifuata maji
  • Hatari za afya za wananchi kutokana na kutokunywa maji safi na kutokuwa na usafi wa mwili
  • Ugomvi katika familia na jamii kutokana na uhaba wa maji
Matarajio yangu yalikuwa kwamba kuwa na raisi mwanamke kungekuwa ni chachu ya tatizo hili kukomeshwa nchini, lakini hali bado ni mbaya leo kama ilivyokuwa jana. Tunachoona ni matumizi makubwa ya fedha kwenye miradi ya maji bila kuona matukio ya miradi huo. Ufisadi umezidi mno kwenye miradi ya maji na hatusikii watu kuchukuliwa hatua.

Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?

Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.

Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.

Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.

Reference: Mgawo wa maji watikisa mijini, vijijini
Umenikumbusha Rungwe, sisi pale shuleni maji yalikuwa gravity..ikitokea yamekatika bas ni chamber zimeziba huko mliman, tunaenda kuzibua basi.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi mpaka nimeamua kuita wachimbaji wa Borehole drilling na nimepata maji matamu bila chumvi.

Sasa hivi natengeneza swimming pool ili niwe najipoza huku nikiburudika na Bia bardiii.

Maisha mafupi sana haya.

Na huenda nikafungua kiwanda cha maji siku za usoni nataka kuvuta mkopo wa Kiisilamu wenye riba nafuu iliyofichwa fichwa.
Underground water bila chumvi. Lol! Kama mzaha vile.
 
Umenikumbusha Rungwe, sisi pale shuleni maji yalikuwa gravity..ikitokea yamekatika bas ni chamber zimeziba huko mliman, tunaenda kuzibua basi.



Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa watu wa Rngwe wameshindwa kufanya hilo kwa ajili ya wilaya yote? Hao ndipo utapoona labda Chadema wako right wanaposema wanataka utawala wa majimbo. Mnaletewa Mkuu na Mkurugenzi wa wilaya ambao hawajali maendeleo ya eneo kwa kuwa sio watu wa hapo. Wapo hapo kwa ajili ya kazi na mshahara, sio maslahi na upendo wa eneo kwa sababu ni wazaliwa wa hapo
 
Sijui, na kwasababu siyafanyii Biashara ni kwa ajili ya,domestic use.

Ila sitoshangaa wakija maafsaa na vitambi vyao na kuanza kudai serivce charge wakati hawajaingiza senti.

Wakidai nakifukia chap chap😁 just kiddin
MKuu kama bado hawajaja nashangaa, tena wanaweza kukufungulia mashitaka. Wanasema maji ni rasilimali ya taifa huwezi kuyatumia lazima uwe na kibali, hata kama ni borehole
 
MKuu kama bado hawajaja nashangaa, tena wanaweza kukufungulia mashitaka. Wanasema maji ni rasilimali ya taifa huwezi kuyatumia lazima uwe na kibali, hata kama ni borehole
Huwa naenda kuogelea Baharini mara kwa mara tena bure sasa kama Maji ni rasilimali ya Taifa mbona huwa siwaoni wakinisubiri na taulo langu?

Najua nchi hii inavisheria kandamizi vingivingi sana ambavyo huwa havifutwi ambavyo vingine tumetoka navyo kwa Mkoloni.

Au tulipewa Uhuru wa Bendera?

Mfumo wangu wa kuvuna Maji ya Mvua pia wataniuliza Kibali.

Au yule Mpenzi wangu kutoka Kagera mwenye "Maji" mengi pia watauliza Permit?

Wakija maswali watayakimbia.
 
Huwa naenda kuogelea Baharini mara kwa mara tena bure sasa kama Maji ni rasilimali ya Taifa mbona huwa siwaoni wakinisubiri na taulo langu?

Najua nchi hii inavisheria kandamizi vingivingi sana ambavyo huwa havifutwi ambavyo vingine tumetoka navyo kwa Mkoloni.

Au tulipewa Uhuru wa Bendera?

Mfumo wangu wa kuvuna Maji ya Mvua pia wataniuliza Kibali.

Au yule Mpenzi wangu kutoka Kagera mwenye "Maji" mengi pia watauliza Permit?

Wakija maswali watayakimbia.
Nadhani kuna tozo pia ikiwa unavuna maji ya mvua utafikiri yametoka serikalini 🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom