Majibu ya Dr. Masau wa THI kwa maswali mbalimbali

Kitila.

kinachozungumziwa hapa ni kuwa Masau kweli amesoma udaktari Muhimbili na China lakini hajawahi kuwa daktari anayetibu watu Marekani hilo mwenyewe kasema

Sasa sisi ndio hapo tunauliza, kutokutibu America ndio kunamfanya asiwe daktari kamili? Sasa huu mtazamo si ndio wengine hapa wanauita kuwa ni ulimbukeni au siyo?
 
leo mtu mzima (Kuhani) kakamatwa "mbavu"! Kweli akishindwa kuthibitisha kauri zake itakuwa aibu, kwangu mimi nadhani amekwenda kupiga tena simu kwahiyo tumpe muda atarudi tu!

Kwa kifupi Muhimbili kuna Daktari mmoja tu ndiye super specialist wa moyo Dr. W. Wandwi, huyu kamaliza masomo Israel mwaka 2006 na wala hana LICENCE kutoka Israel, Je na huyu atimuliwe/ mbabaishaji??
 
Ukiwa mwanafunzi wa "Residence" hata hapo Muhimbili ulizeni wanafunzi wa Masters. Unatakiwa kushiriki Operation zote zinazofanyika zinazohusu specialization yako. Kushiriki kuna maana mbili, kwanza unakuwa part of the team kama mwanafunzi unayejifunza, lakini pia katika level au baada ya kipindi fulani fulani unakuwa main actor kwenye operation yenyewe chini ya uangalizi wa karibu sana wa Madaktari bingwa wengine.

Kwa hiyo kwa upande wa Dr. Masau, kama alivyosema mwenyewe, kwa vile alikuwa pale mahsusi kujifunza, sio kitu kigeni kushiriki operation za moyo 1800. Na mimi naona mantiki hapo kwa sababu ili uwe mzoefu ni lazima ushiriki kwenye operation za aina nyingi kadri iwezekanavyo.

Cha muhimu ni kwamba Dr. hajasema kwamba operation zote hizo 1800 yeye ndo alikuwa main "actor", na wote tunaelewa kwambaoperation haifanywi na mtu mmoja.

Nadhani, kama kuna madaktari humu JF ambao wamefanye speciliazation (Residence) kokote kule watupe experience zao.
 
Yaani hoja zingine hapa ni vichekesho...Yani watu wameshaona ukisema umekaa marekani miaka mingi basi hiyo ndio hoja tosha!!?? Kwani ukikaa marekani basi wewe ndio unajua kila kitu? hivyi mnajua wamerikani (wazaliwa wenyewe) wengi tu ni so ignorant?
 
Nashangaa ile issue ya yule mgonjwa kupasuka kichwa pale THI kwa sababu aliwekewa gesi nyingi media wanajaribu kuifukia fukia

Kichwa hicho kilikuwa sawa sawa na mpira unaotumika kwenye tairi za gari,pikipiki au baiskeli,sio kichwa cha kawaida cha kiumbe hai
 
Yaani hoja zingine hapa ni vichekesho...Yani watu wameshaona ukisema umekaa marekani miaka mingi basi hiyo ndio hoja tosha!!?? Kwani ukikaa marekani basi wewe ndio unajua kila kitu? hivyi mnajua wamerikani (wazaliwa wenyewe) wengi tu ni so ignorant?

Kwani nani amesema hiyo ndiyo pointi hapa?
Kwani una maanisha kuwa Dk Masau aliposoma Muhimbili basi akija marekani ni IGNORANT?
Muhimbili kuna ma genious na wanahitaji msaada...Jamaa yangu Crispin Severe AKA KOBE kama huko hapo muhimbili bado big ups ndugu yangu...Najuwa mnanyaswa sana na hampewi kipa umbele kabisa na mafisadi wetu.
 
Angalieni waandishi wanavyo DESA ,labda kama huyu dokta aliwatumia hiyo email aliyomtumia mwanakijiji ama mwanakijiji ndiyo huyo mwandishi.

Angalia habari hii ya mwananchi na usome email ya Masau kwa mwanakijiji na ulinganishe


Date::8/9/2008

Mkurugenzi THI azuliwa jambo katika mtandao wa inteneti
Na Jackson Odoyo
 
Yaani hoja zingine hapa ni vichekesho...Yani watu wameshaona ukisema umekaa marekani miaka mingi basi hiyo ndio hoja tosha!!?? Kwani ukikaa marekani basi wewe ndio unajua kila kitu? hivyi mnajua wamerikani (wazaliwa wenyewe) wengi tu ni so ignorant?

Mkuu sizunguki mbuyu, wewe huna hoja hapa ila una kiroja, check this out, nimesema hivi mimi nimewahi kuishi USA miaka 20, kwa kutumia hiyo experience nikasema kuwa Kuhani ni muongo na ukweli umethibitishwa na Dr. Masau mwenyewe kuwa Kuhani ni muongo na mzushi kama nilivyosema kwa kutumia experience yangu ya kuishi USA miaka 20,

Kuhani amesema uzushi kwa kutumia gear ya kuishi USA, nimemwambia kuwa huko USA, alipokwenda alitukuta tayari tupo na tunayajua ya huko kuliko yeye aluyeenda majuzi tu, ukweli umejitokeza wazi kuwa ni mzushi na muongo,

Sasa hapa exactly, anayechekesha hasa ni nani kati yangu, wewe na Kuhani?
 
I'm so done. Swali la msingi limeshabijiwa. Kuhamisha magoli kwa lengo la kukwepa kufungwa haisaidii. Wote tunakosea, wakati mwingine tunaandika vitu kwa jazba au tukiamini ni kweli. Na nina uhakika hata huko mbeleni tutakosea hapa na pale au tutatoa ripoti ambayo si sahihi.

Naamini Kuhani ameona hilo na sidhani kuna haja ya kumlazimisha aombe radhi kama hayuko tayari kufanya hivyo. Akiona ipo haja ya kufuta kauli yake ya kwamba Dr. Masau hajasomea upasuaji wa moyo (kumbuka ilikuwa ni blank statement, akiamini kuwa upasuaji wa moyo ni lazima kuwa angekuwa amesomea Marekani wakati amekuja). Jibu limepatikana.

Kilichonishtua binafsi ni ushauri wake alioutoa kwa mtu na kumwambia amuondoe mgonjwa mikononi mwa daktari halali na mwenye uwezo wote. Hilo lilinitisha na siamini kama Kuhani ana qualification ya kutoa ushauri wa kitabibu based on hearsay.

Mambo ya leseni na mengineyo natumaini yatarudi kwenye mada kuu, lakini suala la elimu ya Dr. Masau natumaini limeekuwa settled once and for all.

Nawashukuru kwa michango yenu mingi ambayo miingine kwa hakika imekuwa too personal and bordered on personality and character attacks. Tuendelee kukumbuka hoja hujibiwa kwa hoja, siyo vioja.

Na ninamshukuru Dr. Masau kwa kutumia muda kujibu hoja zetu kitu ambacho viongozi wetu wengine inakuwa mbinde. Leo hii tukimuuliza Nchimbi au Mkullo kuhusu elimu zao watakuwa tayari kutoa majibu yao kwa kina? I hope so. Vinginevyo, Dr. Masau amekubali kuja kwenye tanuru la moto na ametoka mzima.

Kwa upande mwingine namshukuru Kuhani kwa changamoto yake ambayo sidhani kama alitarajia ingeturn out this way lakini ametusaidia at least to establish ukweli kuwa mjadala wa Dr. Masau ubakie kwenye masuala ya Kodi.

Na hata hilo, tutashindwa kujadili sana kwa sababu kuna mchakato wa kisheria unaoendelea. Ingawa kuna watu wanataka alipe "kodi" alimradi mahakama ya chini imeamua bado kuna kesi zinaendelea mahakamani na ni vizuri tunapojadili tuache sheria zifuate tusije kujikuta kama ilivyotukuta kwenye mjadala wa Dr. Mwakyembe pale ambapo baadhi ya wanachama wenzetu walitaka tu "alipe" alichozushiwa kuwa anadaiwa asichafue jina lake.

Hadi mahakama ya mwisho kabisa itakapotoa hukumu, Dr. Masau ana haki zote za kuendelea kufanya shughuli zake na kupinga kitu chochote ambacho anaamini kuwa hatendewi haki yeye na THI.

m.m.
 

Wakuu hebu muangalie haya maneno kwa makini, hivi huwezi kumaliza career ya mtu mwingine na maneno ya uzushi kama haya? Wewe muombe radhi Dr. Masau, kwa sababu maneno kama haya hata adui wako wa aina gani huwezi kumrushia, I mean what a character this guy is! Yaaani nikisoma haya nasikia hata kutapika!

Mkuu MMJ,

Hebu yasome vizuri haya maneno juu, ya uzushi wa Kuhani this is serious! na inaweza ku-turn into a legal problem maana where do you draw the fine line?
 

Inatosha baba! Naona jinsi ulivyomkalia kooni Mzee Kuhani inaonyesha wazi una personal vendetta dhidi yake. Kumbuka kwamba Mzee Kuhani ni binadamu pia na anaweza kukosea kama ulivyo wewe! Utakumbuka jinsi ulivyopotosha wana JF mara kadhaa humu ndani lakini watu hatukuchuulia kama "big deal" au siyo? Mfano mzuri ni jinsi ulivyothibitisha tena kwa "Breaking News" kulingana na "dataz" unazozijua mwenyewe eti Mohamed Mpakanjia kafariki dunia wakati si kweli. Ama kweli Nyani haoni ku....
 
FMES, nimeyaona madai hayo yote ya Kuhani, lakini kama haoni kosa lolote, hatuwezi kwa kweli kumfanya aone. Kama nyani keshakomwa giledi.
 
Mimi Nimesha-conclude Kuwa Kilichomkwamisha Dr Masau Tanzania Ni:

1. Tabia Ya Viongozi Wetu Kuweka Maslahi Yao Mbele.

2. Ukosefu Wa Elimu/ujuzi Wa Biashara Uliojionyesha Wa Dr Masau.

I Am Done, All The Best Dr Masau.
 

Haya ndiyo ninayomaanisha nikizungumzia wapambe! Hakuna upasuaji wa moyo unaofanywa kwa kuangalia TV (nadhani kinachozungumziwa ni monitor). Kinachofanyika ni mpasuaji kuangalia monitor ambayo inamwezesha kuona viungo kwa ubora zaidi. Anayefanya hivi ni lazima awe amebobea na hands on experience. Vinginevyo wamarekani wote wangekuwa surgeons kutokana na kuangalia Grey's Anatomy na ER! Kuwa mgeni wa Surgeon General Marekani hakuna maana yeyote kitaaluma maana huyo kama vile alivyo Attorney General ni mtu aliyepewa wadhfa huo kisiasa. Mtu kuwa AG si lazima kuwa ulikuwa wakili mkali kupita wote. Mfano ni AG aliyejiuzulu kabla ya huyu wa sasa. Wapambe tunamharibia huyu mwenzetu.

Narudia tena, kuhoji credentials ni wajibu wetu. Neno Kihiyo halikutoka hewani. Alikuweko. Sasa kama huyu mkuu ana'load' CV yake ni lazima aulizwe. Hii kukimbilia kila siku kumtetea mtu kwa vile tu ni mzalendo mwenzetu kutatufikisha kubaya.

Tusichelee kuwaangalia kwa undani wataalamu wote wanaokuja nyumbani. Tabia ya kuogopa kuhoji kwa kisingizio kuwa tutawakimbiza wenye moyo does not hold water. Wengi wa hao wataalamu wetu wasingeweza kufikia kirahisi hapo walipo kama wangebakia ughaibuni. Wangepata pesa nyingi zaidi bila shaka lakini si wadhfa na heshima ambayo wanaipata kwetu. Leo tunaona watu kurudi nyumbani kuwa magavana wa benki kuu, mawaziri n.k. ni kutufanyia fadhila!!!!! Hapana. Ni lazima tuwe humble na kushukuru kupata nafasi hizo. Tusiwabeze kwa kutishia kuwa tusipolambwa miguu tutarudi tulikotoka. Pale tunapoonewa tulalamike lakini si kwa kuhojiwa credentials zetu.

Amandla!
 

Leo mtahangaika sana, hiyo Breaking newss aliyeitoa sio mimi, ilitolewa na mtu mwingine, na unaweza kuitafuta uiweke hapa, maana hapa hakuna mate bro tuna wino tu, huwezi kuchukulia big deal habari ambayo sikuianzisha, sina vendetta na mtu yoyote hapa ila kama kawaida ninasimamia ukweli tena kiroho mbaya, kukosea ni one thing na kuzusha ni another thing, huyu amezusha kwa sababu alikuwa na nafasi nyingi sana za kubadili habari yake lakini akaendelea kutoa uzushi zaidi,

Kwenye ukweli nimesema siku zote simuogopi mtu, mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kumwambia kuwa huwezi kupiga simu Texas Medical Board ukapewa habari za mwanafunzi, lakini akajifanya much know sana, hebu tizama maneno yake hapa chini, haya sio ya kukosea haya ni uzushi wa makusudi, hivi umeshawahi kuifikiria familia ya Dr. Masau ambayo inaishi kwa kutegemea kazi ya huyu mzee aliyezushiwa, hebu soma hapa chini halafu uniambie kuwa ni kukosea:-


 
Where was I wakati haya maelezo yalipoletwamezani?? Kwa kweli nashukuru MwanaJJ kwa kuleta taarifa hizi bayana, Dr. Masau keep up the good work, Kuhani where are you?
Nadhani majibu umepata ya uhakika............from the horses mouth
 
Narudia tena, kuhoji credentials ni wajibu wetu. Neno Kihiyo halikutoka hewani. Alikuweko. Sasa kama huyu mkuu ana'load' CV yake ni lazima aulizwe. Hii kukimbilia kila siku kumtetea mtu kwa vile tu ni mzalendo mwenzetu kutatufikisha kubaya.

Kuhoji na kuzusha ni vitu viwili tofauti, huhoji kwa ku-conclude na uzushi, tunajua tofauti yake mkuu, hakuna mwenye tatizo na kuhoji tatizo lililopo mbele yetu ni kuzusha, na credibility ya JF, you know better than that!
 


kama umeamua kuhamisha goal posts then fine.Sasa imerge hii thread na ile ya Masau kutolipa rent NSSF kisha katika kuonyesha nia yako na uzalendo wako waombee MAGAGAGIGIKOKO na MASATU msamaha ili wawe un Banned mana inasemekana walikuwa banned kwa sababu walikuwa wamepishana na wewe na wamekutukana, japo ushahidi ulioletwa hatujaona tusi lolote lile
 

Sawa, binafsi nimeshafikia uamuzi kwamba tuhuma zote nzito alokuja nazo Kuhani dhidi ya Dr. Masau si sahihi tokea pale Kyomo alivyotoa hoja pamoja na ushahidi mzito kuonyesha kwamba Dr. Masau kweli alisomea na kuhitimu vilivyo fani ya Upasua Moyo Texas Heart Institute; achilia mbali kauli binafsi toka Dr. Masau mwenyewe. Lakini swali linakuja: jee wewe hujatoa hoja tena zenye uthibitisho mzito ambazo zingeweza kuwa na athari mbaya zaidi juu ya Wahusika na familia zao? Mfano ni kuhusu Mehdi Mpakanjia ambapo almost uliapa kwamba kutokana na vyanzo vyako vya habari, Mohammed Mpakanjia hatunaye tena duniani! Jee lipi baya zaidi: kumzushia binadamu mwenzo kifo bila ya kuwa na uthibitisho kamili au kudadisi uwezo wa kitaaluma wa msomi na mwana taaluma fulani mwenye uhai?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…