Makabila haya mtu ukifanikiwa jiandae kujaza ndugu tegemezi kwako ama kukuomba misaada kila mara, ukikataa unaonekana huna undugu

Makabila haya mtu ukifanikiwa jiandae kujaza ndugu tegemezi kwako ama kukuomba misaada kila mara, ukikataa unaonekana huna undugu

Wamanyema ni shida kabisa ,kakangu alioa mmanyema ,huyo wifi alikuwa wa pili kutoka mwisho kwa kuzaliwa ,alivooleqa tu ,ma .kwe na dada zake 3 wakahamia na mdogo wake wa mwisho wa kiume ilikuwa karaha kabisa hawabanduki wanaenda kigoma kusalimi na kurudi baada ya wiki Dar
 
Hapa hatuzungumzii upendo au kujaliana, NO! Tunazungumzia ile tabia ya watu kujazana kwa ndugu, kaka, dada zao bila shughuli rasmi za kimaendeleo.

Hali hii imewafanya ndugu zao wanaowalea wamejikuta wanashindwa kupanga maisha yao kwa kuelemewa na gharama za ulezi wa ndugu. unakuta mtu kakaa hata miaka miwili kwa ndugu na ni kijana mwenye nguvu ila bado hajahama kujitaftia pake na wala hana shughuli za kimaendeleo.

Nyuma ya hii tabia hakukosekani visingizio vya oh tuna umoja, oh tunajaliana, oh sisi wakarimu, n.k lakini haibadilishi uhalisia wa hii tabia ya utegemezi.

Inavyotakiwa inabidi muwe na umoja lakini sio umoja wa kuanza kujazana na kuwa wategemezi. Kuna makabila hayawezagi kuvumilia mtu kuja kukaa awe tegemezi na wala si mgonjwa ama mzee.

Mfano mzuri kama wachaga, wakinga, wakurya, n.k yaani kama wewe ni mgeni ukienda kwa ndugu utapokelewa vizuri tu lakini itabidi uwe umeshatoa taarifa juu ya ujio wako, shughuli iliyokuleta, ratiba yako ikoje, upo mpaka lini, mipango yako n.k. Kama ni kusalimiana wiki 2 zinatosha, sahau kuweka kambi hapo ya kudumu.

Kimbembe kipo kuna makabila wakishaona mwezao katoboa mjini, basi ndugu zake ama ndugu wa mke huhamishia kambi huko. Wanakula na kulala hapo bila kazi maalum 😅😅

Makabila haya kwangu niliyoyaona ni kama;

. Watu wa pwani - wazaramo, wasambaa, wadigo

. Wanyakyusa - hawa huwa wanaendeleza undugu hata ule wa mbali. Yaani hata mke wa mjukuu wa baba mdogo wa babu bado anahesabiwa kama ndugu, kawaida sana kukuta mnyakyusa ana ndugu 100

. Waha, warangi na wagogo,
WAGOGO
 
wabena umewaonea mzee.mbena hana tofauti na mhehe kuna usemi wao wanauita "Ndisina sida' manaake hawana shobo na vitu vya watu ni watu wa kujiridhikia na maisha yao.mimi sio mbena ni mtu wa visiwani huko ila nineishi huko na na nimesoma huko so nawajua vizuri
Ndimgaya sida,[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Nadhani kutokana na utandawazi, mgawanyo wa sifa kwa makabila bado upo kidogo lakini unakwisha kwa kasi sana. Kikubwa ni aina za familia na koo tunazooa bila kujali ni za kabila gani.

Kwa mfano, mimi ni mtu ninayependa kukaa peke yangu muda mwingi, na kabla ya kuoa nilihakikisha natafuta mwanamke wa aina hiyo. Pamoja na hilo kumsisitizia zaidi nilimwambia nilivyo, na yeye akasema tunafanana.

Japo anatoka miongoni mwa makabila au jamii zinazotajwa zaidi kwenye huu uzi kwa utegemezi, ila yeye hayuko hivyo. Ninafahamu pia baadhi ambao wameoa kutoka makabila yasiyo na hizo sifa lakini wamejikuta wanashindwa kupanga maisha yao kwa kuelemewa na gharama za ulezi wa ndugu.

NB: Kinachozungumzwa sio kutosaidia ndugu, ni kutokuwalemaza wasifanye kazi wahamie kusubiri huduma kwa ndugu. Ndugu akiwa na shida atasaidiwa aliko, au akija isipite wiki awe hayupo.
Well said
 
Hapa hatuzungumzii upendo au kujaliana, NO! Tunazungumzia ile tabia ya watu kujazana kwa ndugu, kaka, dada zao bila shughuli rasmi za kimaendeleo.

Hali hii imewafanya ndugu zao wanaowalea wamejikuta wanashindwa kupanga maisha yao kwa kuelemewa na gharama za ulezi wa ndugu. unakuta mtu kakaa hata miaka miwili kwa ndugu na ni kijana mwenye nguvu ila bado hajahama kujitaftia pake na wala hana shughuli za kimaendeleo.

Nyuma ya hii tabia hakukosekani visingizio vya oh tuna umoja, oh tunajaliana, oh sisi wakarimu, n.k lakini haibadilishi uhalisia wa hii tabia ya utegemezi.

Inavyotakiwa inabidi muwe na umoja lakini sio umoja wa kuanza kujazana na kuwa wategemezi. Kuna makabila hayawezagi kuvumilia mtu kuja kukaa awe tegemezi na wala si mgonjwa ama mzee.

Mfano mzuri kama wachaga, wakinga, wakurya, n.k yaani kama wewe ni mgeni ukienda kwa ndugu utapokelewa vizuri tu lakini itabidi uwe umeshatoa taarifa juu ya ujio wako, shughuli iliyokuleta, ratiba yako ikoje, upo mpaka lini, mipango yako n.k. Kama ni kusalimiana wiki 2 zinatosha, sahau kuweka kambi hapo ya kudumu.

Kimbembe kipo kuna makabila wakishaona mwezao katoboa mjini, basi ndugu zake ama ndugu wa mke huhamishia kambi huko. Wanakula na kulala hapo bila kazi maalum 😅😅

Makabila haya kwangu niliyoyaona ni kama;

. Watu wa pwani - wazaramo, wasambaa, wadigo

. Wanyakyusa - hawa huwa wanaendeleza undugu hata ule wa mbali. Yaani hata mke wa mjukuu wa baba mdogo wa babu bado anahesabiwa kama ndugu, kawaida sana kukuta mnyakyusa ana ndugu 100

. Waha, warangi na wagogo,
Roho ya kimaskini. Tafuta pesa jamaa hili sio tatizo ikiwa Nazo. Angalia waarabu na wahindi utakuta ukoo mzima unaishi nyumba moja na hamna kweree. Ila wewe na uchoyo wako wa kimaskini uko na mkeo na vitoto viwili lakini ni migogoro tu. Hats mkeo hamuongei vizuri.... Tufuta pesa roho mbaya iraondoka yenyewe
 
Waha siyo lazima wawe ndugu. Maadamu ni kabila moja, utajuta kuzaliwa
Hii nzuri. Maisha ni kuishi pamoja. Aisee mi niko kawaida financially ila naishi na kubeba watu kibao af hata sijutii naona raha sana. Tatizo watu mnataka kusaidia ile uje usaidiwe. Kama unakopesha yaani. Hayo maisha yanawafanya mtembee na mawazo na visasi mioyoni mwenu Hanna amani yaani mwishi wa siku mnakufa kwa shinikizo la damu au mnapooza. Angalia wachaga na wakinga ndio wanaongoza kwa kupalalyze. Acheni hizo
 
Hii nzuri. Maisha ni kuishi pamoja. Aisee mi niko kawaida financially ila naishi na kubeba watu kibao af hata sijutii naona raha sana. Tatizo watu mnataka kusaidia ile uje usaidiwe. Kama unakopesha yaani. Hayo maisha yanawafanya mtembee na mawazo na visasi mioyoni mwenu Hanna amani yaani mwishi wa siku mnakufa kwa shinikizo la damu au mnapooza. Angalia wachaga na wakinga ndio wanaongoza kwa kupalalyze. Acheni hizo
Visasi vya wapi na kwa nani ndugu yangu?🙊
 
Halafu unapata pesaaa mingi! japo unalisha kundi la watu!! pia ni ufahari kutegemewa na watu wakubwa kwa wadogo! wengiiii!! najisikiaga sana....

nilipo huku nje ya nchi ili mradi tu uwe Mtanzania ninakutunza bila shida na km unaanza maisha njoo kwangu ila usiwe mwizi nina uwezo wa kujua Mwizi ni yupi! lkn shambani kama kawaida!

usiwe mvivu kufanya kazi, za shamba /viwandani, hapa nina Mgahawa wangu utakula humo lkn lipa , nitakulipa posho ya chakula na kazi za kufua vyuma na kuosha magari! kama mia tano hivi! na shamba!

kulima shambani na kuvuna, ujenzi km hujui kujenga utakuwa kibarua wa mafundi kwenye kampuni yangu ya ujenzi!! mambo yako yakiwa safi tambaa!...ukiumwa wkt uko kwangu unatibiwa hospitalini kwangu unalipia!

Ukiona kulala chini huwezi nina milki Hostel utaenda hapo utalipia hela kidogo!! hata ndugu wa damu wakija kwangu mwendo ni ni ivoivo tu! so sinaga hasara!
Mmmmmhhh!
 
Back
Top Bottom