Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Uwezo wa watanzania ni kulalamika kwa vitendo, kwa kutumia ushahidi wa video zilizopita. Yaani ilimradi walalamike, waweke hisia zao wazi ndio huwa furaha yao kuu. Tangu JPM alale usingizi wake wa milele, kuna wanaoishi kwa hasira na majonzi yasiyosemeka. Kila ambacho Mama atakifanya kitaonekana kama kimefanywa na JK kwa mlango wa nyuma.
Bodi mpya ya TANESCO baada ya kuwa imeshajulikana hadharani zimeibuka nongwa za kila aina. Yanasemwa mengi na yote yanamtia hatiani Mama Samia kwa njia moja au nyingine. Kwamba hawezi kuteua watu mpaka apate kwanza baraka za JK.
Kuna pande mbili za wanaosemwa sana mitandaoni. Kwamba wawe wabunifu maana kwa hatua ya kwanza kabisa mpaka wao wakarudishwa na kupewa vyeo vya juu ni ubunifu ulioacha alama wa siku zilizopita. Pia maoni hasi juu ya kwanini wapewe vyeo walivyonavyo sasa japo walishachafuka, ni ukweli kwamba uaminifu wao sio mzuri mpaka leo. Kwamba madudu yao yanaendelea kufuata siku zote, rekodi zao zimeshachafuka na uchafu huo unatokana na rekodi zao za nyuma zinavyosomeka.
Hawa wenye wepesi wa kulalamikia juu ya rekodi hizo chafu za hawa wateule wapya wa Mama Samia wanachoshindwa kufahamu ni kuwa hata JPMa alipowaondoa hawa wa sasa aliwaweka wale alionao na sauti juu yao. Aliondoa kundi moja la wapigaji akaja na kundi jingine lenye kufanya uchafu ule ule lakini hakukuwa na uwazi wa vyombo vya habari wa kuweza kuuanika.
Hivyo jamii haijatendewa haki kwani inafahamu uchafu wote wa watendaji wa zamani wa JK lakini haifahamu uchafu wa wale waliokuwa ni wa JPM. Hayati hakuwa msafi kama tunavyojaribu kujulishwa kwenye media, la hasha. Uchafu wa watu wa JK unatokana na maamuzi yake na utayari wa kuweka kila kitu wazi.
Hivyo ni matarajio ya wadau wa sekta ya umeme kuwaona watendaji waliokuwa wachafu na bado ikaonekana wanafaa kupewa vyeo hivyo, wakiwa na uhuru na utendaji wenye ufanisi kuliko ile awamu ya kwanza walipochafuka na kuchafuliwa zaidi watu wakiaminiswa ni wachafu kumbe ni uchafu wa kisiasa unaopewa kipaumbele kuliko ule halisia.
Waitumie hii fursa ya pili waliyopewa na Mama Samia kwa kuwaonyesha wenye wasiwasi na utendaji kazi wao kwamba ni mawazo potofu kuamini kuwa wanatakiwa watiliwe shaka milele yote.
Kuna watu wamenuna na muda wote kosa dogo wapo tayari lionekane ni kubwa sana, hii ni kutokana na kuishi tofauti na matarajio yao. Ghafla tu wamelazimika kuwa wapole huku wakichekea machoni tu, wanalolishauri linaweza kuonekana ni la kweli na la dhati ya moyoni kumbe linao mtego wa hatari ndani yake.
Wajumbe wapya wa bodi ya TANESCO, wapige kazi kadri wawezavyo pasipo kujaziwa mabegani zile shauku na mioyo ya hasira kutoka kona mbalimbali za wanajamii.
Bodi mpya ya TANESCO baada ya kuwa imeshajulikana hadharani zimeibuka nongwa za kila aina. Yanasemwa mengi na yote yanamtia hatiani Mama Samia kwa njia moja au nyingine. Kwamba hawezi kuteua watu mpaka apate kwanza baraka za JK.
Kuna pande mbili za wanaosemwa sana mitandaoni. Kwamba wawe wabunifu maana kwa hatua ya kwanza kabisa mpaka wao wakarudishwa na kupewa vyeo vya juu ni ubunifu ulioacha alama wa siku zilizopita. Pia maoni hasi juu ya kwanini wapewe vyeo walivyonavyo sasa japo walishachafuka, ni ukweli kwamba uaminifu wao sio mzuri mpaka leo. Kwamba madudu yao yanaendelea kufuata siku zote, rekodi zao zimeshachafuka na uchafu huo unatokana na rekodi zao za nyuma zinavyosomeka.
Hawa wenye wepesi wa kulalamikia juu ya rekodi hizo chafu za hawa wateule wapya wa Mama Samia wanachoshindwa kufahamu ni kuwa hata JPMa alipowaondoa hawa wa sasa aliwaweka wale alionao na sauti juu yao. Aliondoa kundi moja la wapigaji akaja na kundi jingine lenye kufanya uchafu ule ule lakini hakukuwa na uwazi wa vyombo vya habari wa kuweza kuuanika.
Hivyo jamii haijatendewa haki kwani inafahamu uchafu wote wa watendaji wa zamani wa JK lakini haifahamu uchafu wa wale waliokuwa ni wa JPM. Hayati hakuwa msafi kama tunavyojaribu kujulishwa kwenye media, la hasha. Uchafu wa watu wa JK unatokana na maamuzi yake na utayari wa kuweka kila kitu wazi.
Hivyo ni matarajio ya wadau wa sekta ya umeme kuwaona watendaji waliokuwa wachafu na bado ikaonekana wanafaa kupewa vyeo hivyo, wakiwa na uhuru na utendaji wenye ufanisi kuliko ile awamu ya kwanza walipochafuka na kuchafuliwa zaidi watu wakiaminiswa ni wachafu kumbe ni uchafu wa kisiasa unaopewa kipaumbele kuliko ule halisia.
Waitumie hii fursa ya pili waliyopewa na Mama Samia kwa kuwaonyesha wenye wasiwasi na utendaji kazi wao kwamba ni mawazo potofu kuamini kuwa wanatakiwa watiliwe shaka milele yote.
Kuna watu wamenuna na muda wote kosa dogo wapo tayari lionekane ni kubwa sana, hii ni kutokana na kuishi tofauti na matarajio yao. Ghafla tu wamelazimika kuwa wapole huku wakichekea machoni tu, wanalolishauri linaweza kuonekana ni la kweli na la dhati ya moyoni kumbe linao mtego wa hatari ndani yake.
Wajumbe wapya wa bodi ya TANESCO, wapige kazi kadri wawezavyo pasipo kujaziwa mabegani zile shauku na mioyo ya hasira kutoka kona mbalimbali za wanajamii.