KWELI Makamu wa Rais akishika nafasi ya Rais kwa muda wa miaka 3 au zaidi ataruhusiwa kugombea kipindi kimoja tu

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Mie nimesoma lkn kama sijaelewq vile,kwa maana hiyo samia ataruhusiwa kuwa mgombea 2025 na katiba?. Kama jibu ni ndio,basi taifa hili bado lina kazi kubwa,na tutafika tumechoka mno.
 
Pamoja na kwamba katiba iliyopo ina mapungufu mengi ila kuna mambo yako wazi na yanaeleweka vizuri.Hayo mengine yanaropokwa kwasababu ya uwepo wa chawa wanaojali matumbo yao badala yakuzingatia weledi.
 
Naona Wananchi tunaandaliwa Kisaikolojia kwamba aliyepo ataendelea hadi 2030 huko 🙌
 
Asije kurudia "Nilisema katiba ni kijitabu tu..."
 
Miongoni mwa Awamu zilizopita, Awamu hii ya Tano ndio iliyojiwekea Historia kubwa Nchini.

Hakika hili litakuwa ni somo la Siasa(case study)huko mbeleni.

Mfano:Kuna nguvu kubwa iliyotumika, imetumika kuhadaa Umma kushusu mihula. Ni dhahiri huu ni muhula wa Awamu ya Tano.

Sababu kubwa ni kufunika fikra za kwamba "Tunaweza" kama Taifa kuwa na misimamo thabiti dhidi ya Ukoloni Mamboleo, Usimamizi wa Rasilimali zetu Uchumi wetu and so forth, bila ya kuwa tegemezi wa Misaada na Mikopo yenye masharti magumu.

Sababu zingine ni vita za Kiuchumi ambazo baadhi ya waliopo madarakani wameamua kutelekeza kwa visingizo vilivyotokana na kampeni kubwa kuwahi kutokea katika karne hii, Kampeni za kinafiki, Kampeni hasi za kumchafua Raisi alikuwepo madarakani.

Maua yamfikie aliyeleta mada hii Jamii Check, kwani, karibia tutawajua masaliti, manafiki na wasiopenda Nchi yetu Tanzania
 
Hamtakiwi kuwa na shaka maana hata yule alitaka aongezewe ila kafa
 
Ukweli ambao watu hampendi kuusikia ni huo,
Hii miaka ni ya mpito, ambayo ni ya Rais magufuli,
Rais Samia akigombea 2025 ataongoza miaka mitano, hiyo ikiisha ndio atatakiwa agombee tena miaka mingine 5 yaani 2030 agombee tena ndio atimize miaka yake 10,
Hii anamalizia sera na maono ya magufuli, ili atuvushe baada ya kifo cha marehemu magufuli,
Huo ndio ukweli ambao mnatakiwa muishi nao wala msiogope,
 
Kama hivyo aruhusu wapinzani wane kina Kipara waakapambane kwenye kura za maoni kule CCM- NEC
 
Matusi mengi huwa mnajitakia tu....... Haya mbwa wewe umeandika nini hapa sasa
 
Elimu elimu elimu. Wazazi tupeleke watoto shule.
 
😂 katiba haisemi hivyo samia amerithi miaka 3 ya rais aliepita hivyo anamuhula mmoja tu wakugombea angekuwa amerithi miaka 2 hapo ndo angekuwa anamihula 2 yakugombea.
 
Hii ina maana fomu zitatolewa kwa wote kama utaratibu ulivyo mnapogombea awamu ya kwanza. Si ndio hivyo?
 
Yani Mwigulu hadi 2035? Hapana asee hatutakubali. 2035 mbali sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…