Maketa: Tendo la ndoa kinyume cha maumbile ni chanzo cha ndoa nyingi kuvunjika

Maketa: Tendo la ndoa kinyume cha maumbile ni chanzo cha ndoa nyingi kuvunjika

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Afisa Ustawi wa Jamii wa Jiji la Dar es Salaam, Joyce Maketa, amesema kwamba miongoni mwa mambo yanayovuruga ndoa hadi kupelekea wanandoa kuachana inasababishwa na wanaume kuomba mahusiano kinyume na maumbile.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Septemba 6, 2022, jijini Dar es Salaam, kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio mara baada ya taarifa kuonesha kwamba kila mwezi ndani ya jiji la Dar es Salaam takribani ndoa 300 zinavunjika.

"Kumekuwa na mahusiano mapya (Kwa wanandoa) yanayopelekea wakati mwingine kuomba kuwa na mahusiano kinyume na maumbile hicho kimekuwa ni moja ya kitu ambacho kimekuwa kikivuruga ndoa nyingi na watu mwisho kuachana, tuachane na hizo tabia tunazozi-copy na tuishi maisha yanayompendeza Mungu,"amesema Joyce

====

Haya yanajiri baada ya kamati ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya jamii kutoa ripoti Septemba 5, 2022 iliyoelezea kuwa mkoa wa Dar es salaam unaongoza kwa uvunjifu wa ndoa nyingi nchini ambapo wastani wa ndoa 300 huvunjika kila mwezi.

Kamati hiyo ilibaini pia kuwepo kwa mmomonyoko mkubwa wa maadili na ukatili mkubwa wa kijinsia hasa ule unaohusisha watoto.

EATV
 
Afisa Ustawi wa Jamii wa Jiji la Dar es Salaam, Joyce Maketa, amesema kwamba miongoni mwa mambo yanayovuruga ndoa hadi kupelekea wanandoa kuachana inasababishwa na wanaume kuomba mahusiano kinyume na maumbile.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Septemba 6, 2022, jijini Dar es Salaam, kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio mara baada ya taarifa kuonesha kwamba kila mwezi ndani ya jiji la Dar es Salaam takribani ndoa 300 zinavunjika.

"Kumekuwa na mahusiano mapya (Kwa wanandoa) yanayopelekea wakati mwingine kuomba kuwa na mahusiano kinyume na maumbile hicho kimekuwa ni moja ya kitu ambacho kimekuwa kikivuruga ndoa nyingi na watu mwisho kuachana, tuachane na hizo tabia tunazozi-copy na tuishi maisha yanayompendeza Mungu," amesema Joyce
 
FB_IMG_16624505233542905.jpg
 
Kuvunjika kwa ndoa hazikuanza, Nabii Ibrahim almwambia mwanae abadili kizingiti cha nyumba(aowe mke mwingine) kisa hakua na maadili mke uliotokana na ugumu wa maisha.
 
Back
Top Bottom