Makinda ashangaa wasomi wanaokula bure makwao

Makinda ashangaa wasomi wanaokula bure makwao

Wengi wanabet na kucheza michezo ya bahati nasibu ndio ajira pekee waliyonayo kwa sasa hakuna anaependa kukaa bure mtu amesotea elimu zaidi ya miaka 15 usimchukulia poa you must show some respect to them, wamepambana kuitafuta elimu kwa jasho, shida na taabu angalau wameelimika..
Hela ya kubet wanatoa wap? Hivi unaijua michezo ya betting kweli? Kubet inahitaji pesa hata mimi na bet
 
Wakati kilio cha watu kukosa ajira hasa kwa vijana kikiendelea kushika kasi, Kamisaa wa Sensa Tanzania Bara, Anne Makinda, amesema kuna idadi kubwa ya wasomi wanaoishi kwa wazazi wao wakila bure kwa kutotaka kufanya shughuli za kuingizia kipato.

Makinda ametoa kauli hiyo leo ijumaa, Septemba 23, 2022 ambapo amesema jambo hilo halifurahishi kwa sababu elimu anayopata mtu anatakiwa aitumie kupambana na mazingira.

"Tumeambiwa kuwa elimu ni ufunguo wa maisha na wala sio ufunguo wa ajira, watu wanahangaika kila kukicha kusaka ajira" amesema

Kamisaa Makinda amesema idadi ya watu inazidi kuongezeka kila kukicha na mbaya zaidi wengi hawafanyi kazi.

“Ni jambo la kushangaza kuona wasomi hawapendi kujishughulisha na vitu vya kuwaingizia kipato, hawafanyi hata biashara wakati wasiosoma wanafanya shughuli za kuingiza kipato” amesema.

Ameongeza kuwa Sensa ya watu na makazi iliyofanyika mwezi uliopita itasaidia kupatikana kwa takwimu zitakazotumika kutunga sera mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dk Batilda Burian, alimweleza Makinda kuwa makarani wa sensa wawili walifariki mkoani humo ambapo mmoja alijiua kutokana na matatizo ya kifamilia na mwingine alifariki akiwa katika nyumba ya wageni aliyofikia baada ya mafunzo ya siku 21.

Amesema mwingine alijeruhiwa baada ya kupata ajali wakati akienda kutuma taarifa za Sensa na mguu wake kushoto kusagika na hivyo kukatwa na hivi sasa wanafanya utaratibu wa kumtafutia mguu wa bandia.

Dk Batilda amesema awali walikadiria kuhesabu kaya 490,000 lakini hasa wanakamilisha walihesabu kaya 577,128 sawa na asilimia 118.

Chanzo: Mwananchi
IMG-20220923-WA0181.jpg
 
Acha kabisa anatuchukulia sie mafala...nakwambia ukishatoboa kimaisha unaona wengine wajinga kumbe shukuru familia uliyozaliwa
Waswahili wanasema alie shiba hamkumbuki mwenye njaa, kama ana watoto kaisha waweka kwenye position nzuri.. alafu anaanza kunanga watoto wa wenzake.. Tutaendelea kukaa sana kwa nyumbani hatujaua makwetu na wana tutunza na kutupa chakula cha buree
 
wanaokulaburepiic


Tabora. Wakati kilio cha watu kukosa ajira hasa kwa vijana kikiendelea kushika kasi, Kamisaa wa Sensa Tanzania Bara, Anne Makinda, amesema kuna idadi kubwa ya wasomi wanaoishi kwa wazazi wao wakila bure kwa kutotaka kufanya shughuli za kuingizia kipato.

Makinda ametoa kauli hiyo leo ijumaa, Septemba 23, 2022 alipokuwa akizungumza na kamati za Sensa za Mkoa wa Tabora ambapo amesema jambo hilo halifurahishi kwa sababu elimu anayopata mtu anatakiwa aitumie kupambana na mazingira.

"Tumeambiwa kuwa elimu ni ufunguo wa maisha na wala sio ufunguo wa ajira, watu wanahangaika kila kukicha kusaka ajira," amesema.

Kamisaa Makinda amesema idadi ya watu inazidi kuongezeka kila kukicha na mbaya zaidi wengi hawafanyi kazi.

“Ni jambo la kushangaza kuona wasomi hawapendi kujishughulisha na vitu vya kuwaingizia kipato, hawafanyi hata biashara wakati wasiosoma wanafanya shughuli za kuingiza kipato” amesema.

Ameongeza kuwa Sensa ya watu na makazi iliyofanyika mwezi uliopita itasaidia kupatikana kwa takwimu zitakazotumika kutunga sera mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dk Batilda Burian, alimweleza Makinda kuwa makarani wa sensa wawili walifariki mkoani humo ambapo mmoja alijiua kutokana na matatizo ya kifamilia na mwingine alifariki akiwa katika nyumba ya wageni aliyofikia baada ya mafunzo ya siku 21.

Amesema mwingine alijeruhiwa baada ya kupata ajali wakati akienda kutuma taarifa za Sensa na mguu wake kushoto kusagika na hivyo kukatwa na hivi sasa wanafanya utaratibu wa kumtafutia mguu wa bandia.

Dk Batilda amesema awali walikadiria kuhesabu kaya 490,000 lakini hasa wanakamilisha walihesabu kaya 577,128 sawa na asilimia 118.

Chanzo: Mwananchi
 
Mume wa Anna Mankinda Anaitwa Nani na Anafanya kazi gani?
Nimeuliza tu kwa sababu Moris Makinda ni mtoto wake naye amesoma na anakula bure nyumbani kwake.
 
Mtu aliyepata ajira mara tu baada ya kumaliza elimu wakati wa Nyerere na hadi sasa anapewa privilege na serikali lazima atatoa matamshi hayo...

Hajawahi kusota mtaani huyo
 
Hivi mimi ndo sijui kuzidisha??

kaya 577,000× 5(wastani wa wanakaya)=2,850,000

kwo kwa haraka tuna watu 2850000 tu??

"Dk Batilda amesema awali walikadiria kuhesabu kaya 490,000 lakini hasa wanakamilisha walihesabu kaya 577,128 sawa na asilimia 118."

Aliyekuwa akiongea hayo matamshi ni mkuu wa mkoa wa Tabora, hivyo takwimu hizo ni za mkoa wa Tabora pekee...
 
Unahesabiwa ili usimangawe (jokes).
===
Kuna shida kwenye mitaala yetu maneno ya Mama Makinda yapewe uzito unaostaili. Wahitimu wetu wanashindwa kutumia elimu waliyopata kujitengenezea sehemu za kujiingizia kipato. Hili ni tatizo (serious). Litatuliwe.
 
Ee Myezi Mungu wafanyie wepesi wasomi wote wanaodhalilika kwa kosa ajira, waepushe na masimango wape ujasiri wa kutokujiunga na uhalifu na wajalie afya imara. Amen

Aamina walahi [emoji2972]
Sasa vibarua wanapeana wao kwa wao, wazee hawataki kuondoka kazini!
Vijana wao ndio wachukua nafasi zote, utafikiri hii nchi ni ya Ufalme maana mambo ni kurithiana AIBU walahi [emoji29]
Mwenye Enzi Mungu iangalie hii nchi yako Tanzania [emoji1241] na usikie kilio chetu jamani uwiii [emoji24]
 
Huyu mama kwa hela alizoiba huko CCM_na azoendelea lipwa hapaswi toa kauli kama hii ilhali hana hata ka NGO,,ka kusaidia vijana
 
Unahesabiwa ili usimangawe (jokes).
===
Kuna shida kwenye mitaala yetu maneno ya Mama Makinda yapewe uzito unaostaili. Wahitimu wetu wanashindwa kutumia elimu waliyopata kujitengenezea sehemu za kujiingizia kipato. Hili ni tatizo (serious). Litatuliwe.
Kabla hatujaangalia hiyo mitaala, hebu kwanza tuzitazame tabia za hao wanaowasema watoto wa wakulima wasio na connection.

Wao wamekuwepo serikalini miaka mingi, wana mitaji ya kuwapa watoto wao wakafanye biashara, lakini badala yake, wanawapa nafasi za kazi huko serikalini walipo kwasababu ya kujuana.

Hili linasababisha watoto wa wakulima waendelee kukaa nyumbani kwa wazazi wao kwasababu hawana mitaji, hata hizo habari zao za kuanzisha vikundi ili wapewe mikopo, mara nyingi huwa hazitekelezeki kwasababu ya masharti ya kupewa mikopo.

Makinda kama kweli anamaanisha anachokisema, kwanza namshauri awaambie wenzake serikalini waache kujaza watoto wao, ndugu zao, na marafiki zao, huko maofisini, wawapeleke wakalime ili hizo nafasi wapate watoto wa wale wasio na mitaji.

Haiwezekani nyie mnacho halafu mnaendelea kujiongezea tu, wakati wale wenzenu hawana, halafu mnawasimanga kwa kukosa kwao, hii ni akili iliyochoka kufikiri.
 
Back
Top Bottom