Makonda aanza kukamata wakusanya madeni (auctioneers) wanaotumwa na mabenki

Makonda aanza kukamata wakusanya madeni (auctioneers) wanaotumwa na mabenki

Bila Benki Kuu na Wizara ya Fedha kuongilia kati, naona mgomo mkubwa unanukia Arusha au Nchi Nzima kutoka kwa mawakala wa mabenki na taasisi za fedha wanaokusanya madeni mara baada ya Makonda kuanza kuwakamata baada ya kutimiza majukumu yao.

Hii itakuwa na athari kubwa kiuchumi kwa kuwa fedha za mabenki, ambazo kimsingi ni za wananchi, zinaweza zisilipwe, kwa kuwa wanaozikusanya wanakamatwa na Mkuu wa Mkoa, hivyo wakopaji watakuwa wanakula bata wakati mabenki yanafilisika.

Baada ya hapo fedha zetu zitakuwa salama katika mabenki?
HIVI INAKUINGIA AKILINI MTUANADAIWA M3NA YUPO ANAENDELEA KULIPA UNAUZA NYUMBA YAKE YA M50 HIVI KAMA NI WEWE UNGEJISIKIAJE NI UONEVU MKUBWA SANA WATU WANAFANYIWA NA HAO WATU WACHA WAKAMATWE TU
 
ukute huelew lolote kwenye huu mkasa ila unavyoelezea , watz sijui nan kawaloga , kwamba mtu ashindwe kulipa deni halafu Makonda aje amkingie kifua huyo mtu ? CHUKI IKIZIDI UTATIWA MIMBOR TU
Kuna njia nyingi za kudhulumu,na vile vile kuna njia nyingi za kudai haki yako na ukapata! Usikariri,uchunguzi utafanyika,na ukweli utajulikana,ni swala la muda tu!!
 
Twende mbele na kurudi nyuma. Wewe umeenda kukopa mkopo wa Tshs 3m. Ukasema naweka nyumba yangu amana kwa ajili ya mkopo, ina thamani ya Tshs 50M. Sasa usiporudisha mkopo hao waliokukopesha wafanyeje? Kwa nini wakati wa kukopa usiweke amana kitu cha thamani ya mkopo?
Tatizo ni wewe mkopeshaji ulikuwa na nia ya kukopesha au kujipatia nyumba? Hili linapimwa kwa

1. Kiwango cha riba
2. Uwezo wa mtu unayemkopesha, Anakopesheka?
3. Taratibu za kumfilisi. Una vibali vyote? Umevipata kwa njia halali?

Sasa kwa dhamana ya M50, na mkopo wa M3. Kuna tatizo. Lazima huyu mtu hana capacity ila ana dhamana, hakopesheki. Kwanini ulimkopesha? Baada ya kumkopesha akashindwa, vibali vya kufilisi umevipataje maana mahakamani kupewa hichi kibali zikifatwa taratibu zote si rahisi.
Kisheria ni kwamba, wakiuza nyumba yako ya Tshs 50m, wataiuza kwa mnada, na wanaweza wapate Tshs 30m. Ila watakupa Tshs 27m baada ya kuchukua zile zao Tshs 3m
Ni kweli ndo maana mabank hawapendi kufilisi, wanapenda ulipe. Microfinance uchwara wanapenda ushindwe kulipa ili nyumba ya M50 iuzwe M10, upewe M7 watu wakaiuze M40 huko baadae.
Kwa hiyo hapa Makonda ndio anakosea. Huu ni utaratibu unakubalika kabisa katika masuala ya mkopo. Huyu mkopaji hakulazimishwa kuweka nyumba kama amana, yeye ndio aliamua, kwaba nikishindwa kurudisha uzeni nyumba yangu.
Kuna miongozo mkuu, mambo kama haya unaweza kuta hata mke ajui kama nyumba ya M50 imekopewa na mume M3 na kuna mafomu kibao ya kujaza ili nyumba iwe mali halali ya taasisi ya fedha na waweze kuiuza.
Sasa watu hapa msifanye assumption kwamba nyumba ya Tshs 50m imeizwa na wakopeshaji wakachukua zote Tshs 50m. Hapana, kama wameuza kwa Tshs 50m, watachukua hela yao tu, ile nyingine wanamrudishia
Hakuna mtu analeta M50, hapo itauzwa 10 au 15. Unadhani wakusanya madeni wanapigia wapi pesa? Kwa akili ya kawaida nyumba ya M50 kwa mkopo wa M3 kuuzwa haiingii akilini unless liriba ni likubwa mno.
 
Twende mbele na kurudi nyuma. Wewe umeenda kukopa mkopo wa Tshs 3m. Ukasema naweka nyumba yangu amana kwa ajili ya mkopo, ina thamani ya Tshs 50M. Sasa usiporudisha mkopo hao waliokukopesha wafanyeje? Kwa nini wakati wa kukopa usiweke amana kitu cha thamani ya mkopo?

Kisheria ni kwamba, wakiuza nyumba yako ya Tshs 50m, wataiuza kwa mnada, na wanaweza wapate Tshs 30m. Ila watakupa Tshs 27m baada ya kuchukua zile zao Tshs 3m. Ndio maana katika amana za namna hii, ni bora wewe uuze nyumba mwenyewe, unaweza kupata fedha zaidi.

Kwa hiyo hapa Makonda ndio anakosea. Anashughulika na haya mambo kisiasa. Huu ni utaratibu unakubalika kabisa katika masuala ya mkopo. Huyu mkopaji hakulazimishwa kuweka nyumba kama amana, yeye ndio aliamua, kwamba nikishindwa kurudisha uzeni nyumba yangu.

Sasa watu hapa msifanye assumption kwamba nyumba ya Tshs 50m imeuzwa na wakopeshaji wakachukua zote Tshs 50m. Hapana, kama wameuza kwa Tshs 50m, watachukua hela yao tu, ile nyingine wanamrudishia
Umefafanua vyema. Anachofanya Makonda ni kujijenga kisiasa.
 
Ttzo akili zenu zimekaa kinyonge na kimaskini kwaiyo hamuwezi ata kuwaza mambo madogo

Wanyonge jifunzeni sheria na jinsi gan sheria na taratibu zinafanya kaz lasivyo mtatumika sana kwa manufaa ya watu wengne kujijengea majina ila mwisho wa sku hamjasaidika

Kesi iko mahakaman mkuu wa mkoa ni nan wakutoa maamuzi ya kesi mahakaman.

Umekopa pesa bank na zaman umeweka nyumba mwisho wa kulipa mkopo umefka ujalipa umeongezewa mda wa kulipa deni ujalipa nyumba inakuja kuuzwa unaendaje kumshika dalali auctioneer kwa sheria ipi

Wanyonge acheni kutumika km kondomu
 
Sikatai kuwa kunaweza kuwa na controversies kwenye issue nzima. Ninachopinga ni ufanyakazi kazi wa aina hii, kufanya mbele ya kamera ili ujikombe. Kuna shida gani mgogoro kama huu kama utatatuliwa ofisini baada ya kusikiliza pande zote? Na zaidi, hili ni tatizo sugu la nchi nzima. Tumefikaje hapa? Kutoka ofisini na kusikiliza kesi moja moja itasaidia nini badala ya kutengeneza mifumo ya ku deal na mambo kama haya ifanye kazi?
Kiongozi yote yakifanyikia ofisini unazani kutakua na umuhimu wa vyombo vya habari? Na lazima yapo mengi tu yanafanyikia uko ofisini na baadhi tu kama haya yanayokea kwenye mitandao. Tanzania kubwa hii na matatizo ya hivi yapo mengi tu. La muhimu ni mifumo tu iimaliswe ya kuweza kushughulikia matatizo kama hayo.
 
Tumia kichwa kufikiri,sio kubebea mabeseni ya maparachichi
Chiembe kuna virus unakosa mdogo wangu. Unatuahibisha sana. Punguza uchawa. Just imagine, mtu amekopa million tatu tu, na dhamani ya nyumba ya million 50.Na kibaya zaidi ameanza, kulipia. Unauzaje nyumba yake? Hiyo ni dhuluma kubwa. Na pia unauza bila kuwa, na kibali cha kufanya kazi hiyo. Huo ni utapeli, dhuluma na ujambazi. Ww, unashabikia uchafu na upumbavu unaofanywa, na wahuni. Je, na ww ni mhuni? Makonda ana point tatu tayari.
Tumia kichwa kufikiri,sio kubebea mabeseni ya maparachichi
 
Bila Benki Kuu na Wizara ya Fedha kuongilia kati, naona mgomo mkubwa unanukia Arusha au Nchi Nzima kutoka kwa mawakala wa mabenki na taasisi za fedha wanaokusanya madeni mara baada ya Makonda kuanza kuwakamata baada ya kutimiza majukumu yao.

Hii itakuwa na athari kubwa kiuchumi kwa kuwa fedha za mabenki, ambazo kimsingi ni za wananchi, zinaweza zisilipwe, kwa kuwa wanaozikusanya wanakamatwa na Mkuu wa Mkoa, hivyo wakopaji watakuwa wanakula bata wakati mabenki yanafilisika.

Baada ya hapo fedha zetu zitakuwa salama katika mabenki?
Kwenye hili makonda yupo sawa,
 
HIVI INAKUINGIA AKILINI MTUANADAIWA M3NA YUPO ANAENDELEA KULIPA UNAUZA NYUMBA YAKE YA M50 HIVI KAMA NI WEWE UNGEJISIKIAJE NI UONEVU MKUBWA SANA WATU WANAFANYIWA NA HAO WATU WACHA WAKAMATWE TU
Hamna uonevu hapa. Nani alikulazimisha kuweka rehani nyumba ya Tshs 50m kwa ajili ya mkopo wa Tshs 3m? Mkopeshaji anakuambia tupe mali isiyohamishika kama rehani, unasema sina ila nina nyumba peke yake. Sasa usipolipa wao wafanyeshe? Una choice mbili; kuuza nyumba yako mwenyewe, au wao watakuuzia hiyo nyumba.

Kama huna rehani inayolingana na mkopo basi usiweke nyumba kuwa rehani. Vitu vya kisheria misiwe mnavipa ufumbuzi wa kihisia.
 
Kwa hili namuunga mkono Madereva, yuko sahihi.
Kamata na tia ndan hao wahuni.
Hayo ni mawazo ya mtu asiejua sheria. Hulazimishwei kuweka nyumba yako rehani, au kuwaachia wao ndio waiuze unaposhindwa kurudisha hela yao. Mkopaji ndie aliesema "naweka rehani nyumba yangu". Maana yake nini?
 
Hayo ni mawazo ya mtu asiejua sheria. Hulazimishwei kuweka nyumba yako rehani, au kuwaachia wao ndio waiuze unaposhindwa kurudisha hela yao. Mkopaji ndie aliesema "naweka rehani nyumba yangu". Maana yake nini?
Maana yake wee muuzaji acha utapeli na uhuni.
 
Ttzo akili zenu zimekaa kinyonge na kimaskini kwaiyo hamuwezi ata kuwaza mambo madogo

Wanyonge jifunzeni sheria na jinsi gan sheria na taratibu zinafanya kaz lasivyo mtatumika sana kwa manufaa ya watu wengne kujijengea majina ila mwisho wa sku hamjasaidika

Kesi iko mahakaman mkuu wa mkoa ni nan wakutoa maamuzi ya kesi mahakaman.

Umekopa pesa bank na zaman umeweka nyumba mwisho wa kulipa mkopo umefka ujalipa umeongezewa mda wa kulipa deni ujalipa nyumba inakuja kuuzwa unaendaje kumshika dalali auctioneer kwa sheria ipi

Wanyonge acheni kutumika km kondomu
Umaskini na ujinga ni vitu viwili vinaenda sambamba. Maskini wengi hawataki kabisa kujifunza mambo mbalimbali na mwishowe kama unavyosema wanaishia kutumika na wanasiasa. Kuna nyuzi za wapuuzi wengi humu JF hulalamika eti riba imeongezwa kwenye mkopo utadhani huo mkopo haukuwa na makubaliano yoyote mwanzoni...
 
Wateja waliokopa kwenye kampuni ya Heritage financing limited, ya mkoani Arusha, wafike kumuona makonda!
Wameuziwa nyumba Kila kona
Wawahi mapema Paul Makonda baba wa upendo atashuka na hawa wahuni...hata wa wateja wa AKIBA BANK waliouziwa nyumba zao na vitisho vingi waenda kwa makonda
 
Back
Top Bottom