Pre GE2025 Makonda amjibu Waziri Bashe, asema atamhoji sababu yeye ndiye anakitafutia kura chama

Pre GE2025 Makonda amjibu Waziri Bashe, asema atamhoji sababu yeye ndiye anakitafutia kura chama

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
View attachment 2888158View attachment 2888159


Imekuwa wiki ya kutupiana vijembe kati ya mahasimu wa muda mrefu Husein Mohamed Bashe na Paulo Christian Makonda, mahasimu hao wa muda mrefu toka 2014 wakiwa katika makundi ya kuusaka urais wa 2015, Makonda ambae ni kijana wa Sitta adui mkubwa wa Mzee Lowasa walianza kutupiana maneno makali muda mrefu.

Makonda akiwa ziarani siku ya jana amemjibu waziri wa kilimo Bashe kuwa atamhoji tu kwasababu yeye ndio anakitafutia kura chama hicho.

Bashe alinukuliwa mwisho wa wikii hii akiwajia juu wafanyabiashara wa sukari kwa kufanya lobbying kwa Paul Makonda ili aondoe bei elekezi.

Rai Yangu: Ni vyema vyombo vya maamuzi visiingilie ugomvi huu kwasababu ni kutunishiana misuli kwa vijana wala hakuna jambo serios sana, asitokee wa kuonewa maana wote wanaviziana muda mrefu tu, asionewe mtu.
Migogoro mikubwa nchi hii inahusu ardhi. Polisi, Mahakama.

Ni hivi, kigogo anachukua ardhi yako, ardhi ya mama yako, ardhi ya yatima, mjane, analindwa na polisi, mahakama.

Unafanyaje?
 
Hii kauli sijaielewa chama kikubwa kuliko serikali? Yaani CCM ni Kubwa kuliko wananchi wenye nchi yao ?
Wananchi ndio walioichagua serikali kupitia chama ambacho ni CCM.kwa hiyo serikali ikifanya vibaya ,wanchi wao watakuja kukiadhibu chama kupitia sanduku la kura kwa kushindwa kutekeleza ahadi zake na mkataba wake unaoitwa ilani ya uchaguzi.kwa hiyo ni lazima chama kihakikishe ya kuwa kinasimamia vyema serikali yake katika utekelezaji wa ilani.
 
Chama ndio chenye serikali kwa hiyo hakiwezi kukaa kimya kinapoona mahali kuna changamoto nyingi zinazopigiwa kelele na wananchi. Chama ni lazima kitake ufafanuzi kwa waziri yeyote yule akiwepo Mheshimiwa Bashe.kwa hiyo kama Bashe anajiona ni mkubwa kuliko chama na viongozi wake akiwepo makamu mwenyekiti au katibu Mkuu n.k. basi atafute chama chake au ajiuzulu uwaziri ili Mheshimiwa Rais ateue mtu mwingine atakaye shirikiana na chama chetu.
Kuna sehemu nimesema chama kinapaswa kukaa kimya? Si umeona ulivyo na matatizo ya kuelewa?

Narudia tena, Makonda kama mtumishi wa Chama hana mamlaka yoyote ya kuwasimamisha watumishi wa Umma au kuwapigia simu majukwaani na kutaka maelezo yao na kuwapa amri.

Chama kinafanya hivyo kupitia vikao. Nyie endeleeni kuhalalisha ujinga kwakuwa ni wajinga ila msilazimishe watu kuamini na kuuishi ujinga wenu.
 
Itakua ni ufala kumtumbua Bashe kwa ajili ya falla Bashite.
Bashe anajua anachokifanya lkn Bashiboy anasaka tonge na umaarufu
Mheshimiwa Makonda ni maarufu sana na mwenye jina kubwa sana katika nchi hii.kwa hiyo hana sababu ya kutafuta umaarufu mwingine zaidi ya huo alio nao kwa sasa.
 
Kuna sehemu nimesema chama kinapaswa kukaa kimya? Si umeona ulivyo na matatizo ya kuelewa?

Narudia tena, Makonda kama mtumishi wa Chama hana mamlaka yoyote ya kuwasimamisha watumishi wa Umma au kuwapigia simu majukwaani na kutaka maelezo yao na kuwapa amri.

Chama kinafanya hivyo kupitia vikao. Nyie endeleeni kuhalalisha ujinga kwakuwa ni wajinga ila msilazimishe watu kuamini na kuuishi ujinga wenu.
Mwambie Basi Bashe kama hataki kuulizwa na chama na kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayogusa wizara yake basi ajiuzulu hataleo tu ili Mheshimiwa Rais wetu mpendwa ateue mtu mwingine.
 
Wanatuadaha Kwa mambo Yao ya kipuuzi huku ya kwao yakitimia na kuendelea kuzitafuna Kodi zetu tukija shtuka tumepigwa siku mingi wao wanagonga chiazi za mvinyo wa bei ghali toka ufaransa!!
Watu wengi sana hawawezi kuliona hili.
 
View attachment 2888158View attachment 2888159


Imekuwa wiki ya kutupiana vijembe kati ya mahasimu wa muda mrefu Husein Mohamed Bashe na Paulo Christian Makonda, mahasimu hao wa muda mrefu toka 2014 wakiwa katika makundi ya kuusaka urais wa 2015, Makonda ambae ni kijana wa Sitta adui mkubwa wa Mzee Lowasa walianza kutupiana maneno makali muda mrefu.

Makonda akiwa ziarani siku ya jana amemjibu waziri wa kilimo Bashe kuwa atamhoji tu kwasababu yeye ndio anakitafutia kura chama hicho.

Bashe alinukuliwa mwisho wa wikii hii akiwajia juu wafanyabiashara wa sukari kwa kufanya lobbying kwa Paul Makonda ili aondoe bei elekezi.

Rai Yangu: Ni vyema vyombo vya maamuzi visiingilie ugomvi huu kwasababu ni kutunishiana misuli kwa vijana wala hakuna jambo serios sana, asitokee wa kuonewa maana wote wanaviziana muda mrefu tu, asio
 
Aliyemrudisha Bashite kwenye siasa ndo atajibu kwa Mungu wetu wa mbinguni. Sick!!!!!
 

Bashe ni akili kubwa, ni mtu makini anayejua kusimamia anachoamini, kubwa zaidi sio mnafiki.

Makonda ni akili ndogo, mtu anayeweza kutumika vizuri na baada ya matumizi akatupwa mbali. Yeye hajali, yeyote mwenye madaraka anaweza kumtumia kwa kazi yoyote.

Hakuwezi kuwa na vita kati ya akili kubwa na akili ndogo, hapo ni mmoja anaanika ujinga wake na mwingine anaanika ubora wake.

makonda anakubalika na wananchi kuliko bashe!!

Makonda anagusa hisia za watu

Hakunaga mashindano ya hisia na Akili mzee !!
Hisia muda wote hushinda akili[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Mwenezi ndie boss wa mawazir wote hawataki watenganishe serikali na chama
 
Bashe anakiburi sana mwendie Makonda ananyota Kali sana mwanza uko kashangiliwa kuliko ata Nchimbi
 
Mwenezi ndie boss wa mawazir wote hawataki watenganishe serikali na chama
Waziri anayeona hawezi kuagizwa na chama basi Aachie uwaziri haraka sana ili Mheshimiwa Rais wetu mpendwa ateue mtu mwingine.maana chama kina watu wengi sana wanaoweza kuwa mawaziri.kwa hiyo asije waziri akajiona kama Mungu mtu.

Nampa angalizo Bashe kuwa asilete ujuaji na dharau kwa chama.asije hisi ana akili sana.kama anataka akae pembeni .
 
Bashe anakiburi sana mwendie Makonda ananyota Kali sana mwanza uko kashangiliwa kuliko ata Nchimbi
Tena siyuletee kiburi hapa.mheshimiwa Makonda ananitafutia Mheshimiwa Rais kura za ushindi mwakani.halafu yeye anaanza kuleta majibu ya dharau mpaka eti anapindisha mdomo.kama hataki basi akae pembeni huko.
 
View attachment 2888158View attachment 2888159


Imekuwa wiki ya kutupiana vijembe kati ya mahasimu wa muda mrefu Husein Mohamed Bashe na Paulo Christian Makonda, mahasimu hao wa muda mrefu toka 2014 wakiwa katika makundi ya kuusaka urais wa 2015, Makonda ambae ni kijana wa Sitta adui mkubwa wa Mzee Lowasa walianza kutupiana maneno makali muda mrefu.

Makonda akiwa ziarani siku ya jana amemjibu waziri wa kilimo Bashe kuwa atamhoji tu kwasababu yeye ndio anakitafutia kura chama hicho.

Bashe alinukuliwa mwisho wa wikii hii akiwajia juu wafanyabiashara wa sukari kwa kufanya lobbying kwa Paul Makonda ili aondoe bei elekezi.

Rai Yangu: Ni vyema vyombo vya maamuzi visiingilie ugomvi huu kwasababu ni kutunishiana misuli kwa vijana wala hakuna jambo serios sana, asitokee wa kuonewa maana wote wanaviziana muda mrefu tu, asionewe mtu.
Bashe keshachoka uwaziri. Anatamani kuwa back bencher
 
Back
Top Bottom