Makonda: Atakayenunua makontena yangu atalaaniwa yeye na kizazi chake! Atoa onyo kwa atakayethubutu kununua

Makonda: Atakayenunua makontena yangu atalaaniwa yeye na kizazi chake! Atoa onyo kwa atakayethubutu kununua

Wapinzani uchwara walikuwa wanasema ati makontena yamejaa samani za majumbani pamoja na Toyota SUV moja,lakini kwa sasa yameshafunguliwa wamekuwa wakimya sana...Wapinzani Uchwara acheni fitna.
Na TRA wanaotaka kupiga mnada Ni wapinzani uchwara?
Halafu kwann mwanzo alikataa kama sio yake?

Wewe Na huyo Bashite mna tatizo kubwa kichwani mbaya zaidi mnajiona mpo sahihi
 
Eti Mtu anayekwenda Kanisani kila J'pili hayo ndiyo Maombi yake kwa Mungu kwa Mnunuzi halali (siyo mwizi)
Kiburi cha CCM kinafanya Wajione ni wamiliki wa kila kitu Tanzania..
Awamu ya kishamba sana hii.
Mambo ya awamu yanatoka wapi hapo sasa? Yaani wewe ukijiharishia ndo mamako kahara?
 
Wananchi walivyotaka kuwasomea Albadir waliomdhuru LISSU Vyombo vya dola vilisimama imara kuzuia hilo jambo lisifanyike kwa kuogopa waliohusika kupata madhara,sasa yeye mbona amefanya hiyo Ibada Maalum na hakukatatazwa,hii si double standard?

TRA si ni mamlaka ya Serikali,ina maana na yeye anapingana na Serikali kuwa mamlaka yake isikusanye kodi?

Upuuzi puuzi tu
 
yeah! nimeanza kuamini kuwa siku za makonda Zinahesabika sasa!
 
Taarifa huripotiwa kwenye vyombo vya habari kama runinga, redio, magazeti, majarida na mitandao ya kijamii. Iliporipotiwa taarifa ya uingizwaji na uwepo wa makontena yenye jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda mwanzoni iliripotiwa kuwa Makonda 'aliyakana' makontena hayo.

Baadaye, ripoti zinadokeza kuwa RC Makonda 'aliyatambua' makontena hayo yaliyokuwa mikononi mwa TRA na kudai kuwa yalikuwa na samani za shule za mkoa wa Dar es Salaam. 'Akatishia' hata 'kuwashtaki' TRA kwa Rais. Mambo yakawa kimya hadi sasa inaporipotiwa kuwa TRA wamejaribu kuyapiga mnada bila mafanikio.

Sasa inaarifiwa kuwa RC Makonda amekwenda kanisani 'kufanya maombi maalum' ya kukwamisha mnada wa makontena yake. Ametishia kuwa yeyote ambaye atayanunua atapata laana! Kimsingi, ni Dhahiri sasa kuwa RC Makonda anayatambua na kuyapigania makontena yake. Makontena hayo yana nini hasa? Kwanini yalikuja kwa jina lake?

Namsihi RC Makonda, katika hili la makontena yanayoshikiliwa na TRA, aeleweke. Aiache TRA ifanye kazi yake na si kutaka kuionyesha TRA kama iliyo kwenye 'mission' naye kuyahusu hayo makontena. Mnada ufanyike na mambo mengine yaendelee. Namsihi RC Makonda kuacha pia kuwatisha 'kimaombi' wateja wanaotaka kuyanunua makontena hayo.

Kazi njema wakuu wote!
That's a state's kind of game play. Period...
 
Taarifa huripotiwa kwenye vyombo vya habari kama runinga, redio, magazeti, majarida na mitandao ya kijamii. Iliporipotiwa taarifa ya uingizwaji na uwepo wa makontena yenye jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda mwanzoni iliripotiwa kuwa Makonda 'aliyakana' makontena hayo.

Baadaye, ripoti zinadokeza kuwa RC Makonda 'aliyatambua' makontena hayo yaliyokuwa mikononi mwa TRA na kudai kuwa yalikuwa na samani za shule za mkoa wa Dar es Salaam. 'Akatishia' hata 'kuwashtaki' TRA kwa Rais. Mambo yakawa kimya hadi sasa inaporipotiwa kuwa TRA wamejaribu kuyapiga mnada bila mafanikio.

Sasa inaarifiwa kuwa RC Makonda amekwenda kanisani 'kufanya maombi maalum' ya kukwamisha mnada wa makontena yake. Ametishia kuwa yeyote ambaye atayanunua atapata laana! Kimsingi, ni Dhahiri sasa kuwa RC Makonda anayatambua na kuyapigania makontena yake. Makontena hayo yana nini hasa? Kwanini yalikuja kwa jina lake?

Namsihi RC Makonda, katika hili la makontena yanayoshikiliwa na TRA, aeleweke. Aiache TRA ifanye kazi yake na si kutaka kuionyesha TRA kama iliyo kwenye 'mission' naye kuyahusu hayo makontena. Mnada ufanyike na mambo mengine yaendelee. Namsihi RC Makonda kuacha pia kuwatisha 'kimaombi' wateja wanaotaka kuyanunua makontena hayo.

Kazi njema wakuu wote!
kuna kamchezo kanataka kufanyika hapa.

kwa utaratibu wa TRA, kama mali inayoshikiliwa ikishindikana kupigwa mnada kwa sababu iwayo yote (kitu anachokipigania Makonda kitokee), commissioner mkuu wa TRA anayo mamlaka ya kuigawa hiyo mali kwa taasisi yoyote ya kiserekali kama msaada.

serekali na taasisi zake zipo chini ya rais. commissioner mkuu TRA ni mteule wa rais. mwenye mali ni kipenzi cha rais.

jiunge nami kwenye ku connect dots.....
 
Ayo makontena yana nini mbona jamaa anaweweseke kama ni vifaa vya shule si wafungue makontena tuone kweli
 
Mambo ya awamu yanatoka wapi hapo sasa? Yaani wewe ukijiharishia ndo mamako kahara?
Awamu hii ndiyo Imewapa viburi Wote hawa..Mfano wako haufanani na Comment yangu.
 
GSM wamemtosa na sasa hana marafiki watoa hela kwani ni kigeugeu
 
Kwan makonda ni nan hasa kias kwamba awanyime uhuru taasisi kubwa ya kiserikali kufanya kazi zake kwa uhuru?

Kuna mambo mengine viongoz Wetu wanafanya kias kwamba unajiuliza uyu mpaka leo anafanya nin kwann asipangiwe kazi nyingine ya kufanya au apigwe tuu chin..!!!!

Uyo jamaa kwa jinsi magu anavyo mlea ipo siku atakuja toa kauli za dhiaka kwa rais na uwongoz wake....

Sent using Jamii Forums mobile app
Usiumize kichwa mkuu hao wanajuana nje ndani
 
Makonda anapambana kwaajili ya wananchi husan wa DSM.Jitihada zake zimeonekana kwa mambo mengi lakin kunawatu wamejaa chuki dhidi yake .

Namtia Moyo Makonda, Endelea kupambana kwakua watu wanaona juhudi zako atakama baadhi wanachukia mafanikio yako ila wanaelewa mchangowako.
Kumbuka ata wana wa Israel walilazimisha Baraba mhalifu mkubwa achiwe huru ila Yesu aliye watendea mema muda wote asulubiwe hayo ndio ya ulimwengu huu. Chapakazi braza mwisho utavishwa taji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda jana alifanya ibada maalum kanisani kwa ajili ya makontena yake yenye samani za shule yanayoshikiliwa na TRA

Katika ibada hiyo Makonda alionya watakao nunua makontena yake watapata laana kali

Pia aliwarushia dongo TRA akisema ni watu wabaya wasio na huruma na kudai kuwa wanamchukia Makonda

"Kama wanachukia Makonda waondoe nembo ya majina yangu kwenye makontena hayo" alisema Makonda

Ni mara nyingine viongozi wa serikali wanasuguana na taasisi za serikali katika kutekeleza majukumu yake huku kiongozi huyo wa mkoa akihisi anaonewa na ni wivu unaofanywa na TRA kisa anafanya vizuri katika mkoa wake

Juzi Paul Makonda alikaririwa na vyombo vya habari kuhusu kupigwa mnada makontena yake,akisema yeye hatishiki na ni mlima hawezi kuyumbishwa na wale wasiomtakia mema katika harakati zake za maendeleo ya Dar es salaam

Kwa hali ilivyo sasa ni dhahiri kuwa Makonda analaumu serikali kumhujumu na hakubaliani na TRA na mambo inayomfanyia
Nilichogundua katika Uzi huu..wengi mna wivu na muheshimiwa makonda, !!
 
Hivi mtu akiyanunua kisha akapata madhara mfano akatoweka, tutajuaje kuwa ni 'laana' ama ni man made 'laana'?
 
TRA na nyie muwe na huruma.
Kama kweli ni Mali za shule kodi za nini?
Mara ya mwisho kutoa sadaka. nyie tra ni lini?kaeni muyamalize vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo hakufuata utaratibu wa sheria, rejea barua kutoka TRA kwenda kwa Waziri Mpango.
DdvbcQ1UwAAdCSc.jpg
 
Back
Top Bottom