Makonda: Atakayenunua makontena yangu atalaaniwa yeye na kizazi chake! Atoa onyo kwa atakayethubutu kununua

Makonda: Atakayenunua makontena yangu atalaaniwa yeye na kizazi chake! Atoa onyo kwa atakayethubutu kununua

Kama TRA inaweza kumuonea kiongozi wa serikali mwenye ushawishi mkubwa vipi kuhusu mtu wa kawaida kabisa asiye na dhamana yoyote?
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda jana alifanya ibada maalum kanisani kwa ajili ya makontena yake yenye samani za shule yanayoshikiliwa na TRA

Katika ibada hiyo Makonda alionya watakao nunua makontena yake watapata laana kali

Pia aliwarushia dongo TRA akisema ni watu wabaya wasio na huruma na kudai kuwa wanamchukia Makonda

"Kama wanachukia Makonda waondoe nembo ya majina yangu kwenye makontena hayo" alisema Makonda

Ni mara nyingine viongozi wa serikali wanasuguana na taasisi za serikali katika kutekeleza majukumu yake huku kiongozi huyo wa mkoa akihisi anaonewa na ni wivu unaofanywa na TRA kisa anafanya vizuri katika mkoa wake

Juzi Paul Makonda alikaririwa na vyombo vya habari kuhusu kupigwa mnada makontena yake,akisema yeye hatishiki na ni mlima hawezi kuyumbishwa na wale wasiomtakia mema katika harakati zake za maendeleo ya Dar es salaam

Kwa hali ilivyo sasa ni dhahiri kuwa Makonda analaumu serikali kumhujumu na hakubaliani na TRA na mambo inayomfanyia
Ukiwa muongo lazima uwe na kumbukumbu! Bashite aliyakana haya Makontena kuwa si yake sasa yapo mnadani kelele zake za nini?
 
Hizo ni mbwembwe tu,mtu yeyote anaweza akazifanya na zisifanye kazi,TRA pigeni mnada hata kwa bei punguzo
 
Naona hii laana ni kutapatapa tu
Sasa Rais akiyanunua je na akayagawa shuleni unafikiri nini kitatokea NOTHING

Ayaache yaende tu akaombe mengine kwa wafadhili na kuwaambia wasisahau ya ushuru

Sent from my SM using Tapatalk
 
SIKU ZAKE ZINAHESABIKA, NA WIKI ZAKE ZINAHESABIIKA, MIEZI YAKE INAHESABIIKA NAA MIAKA YAKE INAHESABIKA
INABIDI AKESHE KILA WAKATI KWA MAANA HAJUI SIKU WALA SAA
 
".............sasa nayaamini maneno ya Nape rasmi, kuwa kwa elimu/ufahamu wa huyu mtu kamwe hawezi elewa mfumo wa siasa na serikali inavyofanya kazi". Yaani RC anashindwa kujua sheria za kodi zinasemaje?????? Anakimbilia kanisani??
 
something fishy,mbna hayo madeksi ya kawaida sana,hata hapa nyumbani yanaweza kutengenezwa,Makonda umeingia katika deal la kuletewa vifaa huku kuna percentage uliahidiwa,otherwise ungeweza kuwapa watanzania kazi hio ya kutengeneza hayo madawati...…..ungejinyamazia tu baada ya kuwekwa uchi...wewe ndio kwanza unatia mkwara
 
Kwa tamko hili la Bashite, Jiwe anasubiri nini kumtumbua alipohoji sabb ya DSM kuzidiwa mapato na Dom wakati huo kuna jini linazuia Makontena yasiuzwe ili serikali isipate kodi yake?
 
Back
Top Bottom