jambotemuv
JF-Expert Member
- Feb 7, 2008
- 224
- 62
Naamini 'ga' mwishoni mwa kitenzi yamaanisha kitendekacho mara kwa mara.Hapo umeelezea makosa ya kimaneno, ila pia kuna makosa ya sentensi, mfano nilikwenda nikamkuta hayupo, Juma huwa anakujaga hapa kila siku, bwana harusi alipokelewa kwa matarumbeta, sijampa kwa sababu nilikuwa sina, naomba nikopeshe elfu tano wakati kumbe hitaji la elfu tano unahitaji wewe.
Kwenye magazeti ndio huwa inanisikitisha maana utasema hawana wahariri yaani na matumizi ya lugha za mtaani kwenye shughuli za serikali nayo imeshamiri...kuchomekea kwenye speech ama mazungumzo hakuna shida, shida inakuja pale yale maneno ya mtaani yanayochomekewa kwenye mazungumzo alafu unayakuta kwenye taarifa ya kimaandishi mfano "fyekelea mbali" kwenye taarifa rasmi ya Ikulu iliandikwa kama lugha rasmi vileIla kosa kubwa ambalo limeota mizizi na juzi nimeliona gazeti moja limetumia ni uridhi badala ya urithi;matumizi ya dhi na thi ni janga la kitaifa
Kessy na Mchaky vipi?Kuchanganya 'dh' na 'th' utaona
Kudhibitisha au dhamani.
Ujinga mwingine ni kuyaongezea konsonati majina ya kibantu.
Mfano Lissu badala ya Lisu, Zitto badala ya Zito, Kigwangalla badala ya Kigwangala wajinga.
Badala ya kusema 'anakujaga' unapaswa kusema 'huwa anakuja'. Hiyo ndio huonesha kitendo cha mara kwa mara.Naamini 'ga' mwishoni mwa kitenzi yamaanisha kitendekacho mara kwa mara.
Hivi ni fweza au fedha ?ela badala ya fweza hahahaa
Acha upuuziWasukuma wanafika milioni 6 nchi hii, kwahiyo tuwasamehe tuu na kiswahili cha kisukuma.
Kwenye aya ya mwisho ulipaswa kuandika uandishi na sio uhandishi.Kuna maneno kwa kweli yanaudhi, sio tu kuyasikia bali hata kuyasoma!
Halafu kuna neno aghalabu! Neno hili watumiaji wengi wa Kiswahili hupindua tafsiri yake, kutoka mara nyingi na kudhani ni (huzani?) ni mara chache!! Aidha, mara nyingi matumizi ya neno "tegemea" huacha ukakasi mwingi nyuma yake.
Yote tisa, donda ndugu lipo kwenye "r" na "l". Inakera sana kuona mtu anatamka au kuandika "naludi saa tano manake mala kwa mala huo ndio muda wangu wa kuludi kazini!"
Tusisahau pia neno saa linapotamkwa au kuandikwa kwa wingi kwamba masaa! Hapa utakuta hata Waandishi wa Habari wakisema "Waziri Mkuu alihutubia kwa masaa matatu!
Nilisahau! Ingawaje maneno yapo mengi mno kiasi kwamba siwezi kuyataja japo robo yake lakini wacha tu nilizungumzie hili neno "aidha."
Watumiaji wengi wa Kiswahili wanalitumia neno "aidha" kama "either" la Kiingereza, wakati tafsiri ya neno "aidha" ni "vile vile", "pia" au neno lolote lenye tafsiri sawa na hayo. Hivyo basi, badala ya kusema mathalani, "natarajia kuhamishiwa aidha Morogoro au Dodoma", hapo ulitakiwa kusema "natarajia kuhamishiwa ama Morogoro au Dodoma!"
Lakini mleta mada, nawe unatakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno. Inaleta ukakasi kuona unaandika maneno zaidi ya thelathini na hakuna kituo pahala popote pale kwenye tungo husika.
Kwavile umehusisha matumizi mabaya ya Kiswahili na uandishi, basi pia tukumbushane uhandishi sahihi ni pamoja na matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno; yaani punctuation.
2o8 = tuonaneKuchanganya 'dh' na 'th' utaona
Kudhibitisha au dhamani.
Ujinga mwingine ni kuyaongezea konsonati majina ya kibantu.
Mfano Lissu badala ya Lisu, Zitto badala ya Zito, Kigwangalla badala ya Kigwangala wajinga.
Hivi uhandishi unamaanisha ndiyo nini ?Kuna maneno kwa kweli yanaudhi, sio tu kuyasikia bali hata kuyasoma!
Halafu kuna neno aghalabu! Neno hili watumiaji wengi wa Kiswahili hupindua tafsiri yake, kutoka mara nyingi na kudhani ni (huzani?) ni mara chache!! Aidha, mara nyingi matumizi ya neno "tegemea" huacha ukakasi mwingi nyuma yake.
Yote tisa, donda ndugu lipo kwenye "r" na "l". Inakera sana kuona mtu anatamka au kuandika "naludi saa tano manake mala kwa mala huo ndio muda wangu wa kuludi kazini!"
Tusisahau pia neno saa linapotamkwa au kuandikwa kwa wingi kwamba masaa! Hapa utakuta hata Waandishi wa Habari wakisema "Waziri Mkuu alihutubia kwa masaa matatu!
Nilisahau! Ingawaje maneno yapo mengi mno kiasi kwamba siwezi kuyataja japo robo yake lakini wacha tu nilizungumzie hili neno "aidha."
Watumiaji wengi wa Kiswahili wanalitumia neno "aidha" kama "either" la Kiingereza, wakati tafsiri ya neno "aidha" ni "vile vile", "pia" au neno lolote lenye tafsiri sawa na hayo. Hivyo basi, badala ya kusema mathalani, "natarajia kuhamishiwa aidha Morogoro au Dodoma", hapo ulitakiwa kusema "natarajia kuhamishiwa ama Morogoro au Dodoma!"
Lakini mleta mada, nawe unatakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno. Inaleta ukakasi kuona unaandika maneno zaidi ya thelathini na hakuna kituo pahala popote pale kwenye tungo husika.
Kwavile umehusisha matumizi mabaya ya Kiswahili na uandishi, basi pia tukumbushane uhandishi sahihi ni pamoja na matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno; yaani punctuation.
Siyo matumizi sahihiNaamini 'ga' mwishoni mwa kitenzi yamaanisha kitendekacho mara kwa mara.
Awez badala ya Hawezi
Ujaacha badala ya Hujaacha
Uendelei badala ya Huendelei
1.JomonKweli kabisa Mzee kifimbocheza.
Hayo pia yanaiharibu lugha yetu.
Pia kuna vijimaneno vya wanawake lakini cha ajabu waweza kukuta mtoto wa kiume anayatumia.
Tusisahau pia neno saa linapotamkwa au kuandikwa kwa wingi kwamba masaa! Hapa utakuta hata Waandishi wa Habari wakisema "Waziri Mkuu alihutubia kwa masaa matatu!
Kuna watanzania wengi sasa hivi wanasema "nyimbo ya" badala ya "wimbo wa". Mpaka watangazaji kwenye maredio, yaani imekuwa ni kama kawaida kusema hivyo wakati ni makosa.Habari za asubuhi wana JF?
Kumekuwa na tatizo la kiuandishi kwa watu wengi kuanzia humu JF mpaka kwingineko kote kwenye mitandao ya kijamii mwanzo nilidhani ni kujisahau lakini sasa naona kama imezoeleka na kuonekana kama ni maneno ya kawaida kwenye kiswahili na watu wala hawastuki kuona kama ni makosa,yaani makosa yakirudiwa rudiwa mara nyingi huzoeleka na kuonekana ni usahihi
Naomba nitoe mifano michache ya hayo maneno hapa chini;
Nisamee badala ya Nisamehe
Eshima badala ya Heshima
Asubui badala ya Asubuhi
Mdogo angu badala ya Mdogo wangu
Kiac badala ya kiasi
Awez badala ya Hawezi
Ujaacha badala ya Hujaacha
Uendelei badala ya Huendelei
Utamsikia Mtangazaji anasema Nyimbo hii badala ya kusema wimbo huu
Yako maneno mengi sana yanayopotoshwa na wadau wengi humu ndani,ombi langu tu ndugu zangu tubadilike tuandike maneno kwa usahihi wake kwa sababu humu ndani panapitiwa na wanafunzi kuanzia Shule za Msingi,Sekondari na hata Vyuo wanajifunza nini juu ya tunayoyaandika humu?
Eti hapo ndio tunawadharau Wakenya hawajui Kiswahili hawajui kiswahili wakati sisi wenyewe ndio tunavuruga tu.
Ni hayo tu wadau muwe na Jumapili njema
Asante!
Haha! Sasa we pia umeandika nini!?2po pamoja xaxa ndio mda wa kurekebisha waxomi we2
Mkuu, unajua maana ya slang?hizo ni slang mkuu. kuna lugha rasmi, kuna lugha ya mtaani na kwa sasa mitandao ya kijamii imekuja na utamaduni wake wa jinsi ya kuwasiliana. kuna wakati ukisoma ujumbe mfupi wa simu unaweza usielewe utadhani kilichoandikwa si Kiswahili.
hapa wao wenye majina haya ndio wamejiongezeaKuchanganya 'dh' na 'th' utaona
Kudhibitisha au dhamani.
Ujinga mwingine ni kuyaongezea konsonati majina ya kibantu.
Mfano Lissu badala ya Lisu, Zitto badala ya Zito, Kigwangalla badala ya Kigwangala wajinga.
Mkuu Chige ninaomba msaada wako kuna jamaa yangu mfaransa anajifunza kiswahili. Huwa ananiuliza maswali ya kiufundi nyakati nyingine, ambayo kimsingi ni nje ya taaluma yangu.Kuna maneno kwa kweli yanaudhi, sio tu kuyasikia bali hata kuyasoma!
Halafu kuna neno aghalabu! Neno hili watumiaji wengi wa Kiswahili hupindua tafsiri yake, kutoka mara nyingi na kudhani ni (huzani?) ni mara chache!! Aidha, mara nyingi matumizi ya neno "tegemea" huacha ukakasi mwingi nyuma yake.
Yote tisa, donda ndugu lipo kwenye "r" na "l". Inakera sana kuona mtu anatamka au kuandika "naludi saa tano manake mala kwa mala huo ndio muda wangu wa kuludi kazini!"
Tusisahau pia neno saa linapotamkwa au kuandikwa kwa wingi kwamba masaa! Hapa utakuta hata Waandishi wa Habari wakisema "Waziri Mkuu alihutubia kwa masaa matatu!
Nilisahau! Ingawaje maneno yapo mengi mno kiasi kwamba siwezi kuyataja japo robo yake lakini wacha tu nilizungumzie hili neno "aidha."
Watumiaji wengi wa Kiswahili wanalitumia neno "aidha" kama "either" la Kiingereza, wakati tafsiri ya neno "aidha" ni "vile vile", "pia" au neno lolote lenye tafsiri sawa na hayo. Hivyo basi, badala ya kusema mathalani, "natarajia kuhamishiwa aidha Morogoro au Dodoma", hapo ulitakiwa kusema "natarajia kuhamishiwa ama Morogoro au Dodoma!"
Lakini mleta mada, nawe unatakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno. Inaleta ukakasi kuona unaandika maneno zaidi ya thelathini na hakuna kituo pahala popote pale kwenye tungo husika.
Kwavile umehusisha matumizi mabaya ya Kiswahili na uandishi, basi pia tukumbushane uhandishi sahihi ni pamoja na matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno; yaani punctuation.